Pre GE2025 Makalla: Wakurugenzi hawatasimamia Uchaguzi, ahoji hofu ya CHADEMA kuhusu Uchaguzi licha ya marekebisho ya mfumo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Itikadi, Uenezi na Mafunzo, CPA Amos Makalla, Amos Makalla ameshangaa hofu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ya kutotaka kushiriki uchaguzi mkuu kwa madai ya kufanyika mabadilko wakati Serikali imeshafanya marekebisho makubwa kwenye mifumo ya uchaguzi.

Your browser is not able to display this video.
Pia, soma
 

..uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 umefanyika baada ya marekebisho lakini umerudia dhuluma na udhalimu wa 2019, na 2020.

..kilichojitokeza katika uchaguzi wa mitaa wa 2024 ni uthibitisho kwamba yanahitajika mabadiliko makubwa zaidi ya yale ambayo serikali imeyafanya.
 
Sheria ili Imesema hivyo Bwana
CPA Makala?
No reform no electing
 
Hata ukiangalia hiyo clip kwa wananchi wanaomsikiliza unawaona kabisa hata sura zao muonekano wao wanamshangaa Makalla anachoongea. Wanajiuliza kwa nini tunadanganywa na sisi tunakubali? Hawana la kufanya masikini afadhali wasinzie. Hata maji ya kunywa hawana. CCM hawana huruma.
 
Ufanisi walioupata CCM kwenye chaguzi za 2019 na 2020 utawasukuma kutumia mbinu zile zile if nothing changes

Itakuwa ni ukichaa kwa wapinzani kukubali kwenda kwenye uchaguzi katika mazingira yaleyale kama lengo ni kuitikisa CCM na kuzoa viti vingi zaidi vya Ubunge pamoja na kura za Urais

Madness is doing the same thing repeatedly and expect different results. Kama lengo ni kutaka CCM iwarushie viti vichache vya ubunge na kura kadhaa za Urais ili angalau wapate ruzuku, then wajipange kushiriki
 
Makala, Makala, Makala umesahau ahadi ya Kinana, Rais mwenyewe, Mchengerwa na kilichotokea uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka jana tuu😳😳😳😳😳
CCM ni hodari sana kwa porojo ila matendo yao ni aibu tupu hasa swala la uongozi
 
Ndo hapo sasa.

Haya mabadiliko wanayoyasema yangekuwa na mashiko endapo uchaguzi wa mwezi Novemba mwaka jana tusingeona zile engua engua za Wagombea wa CHADEMA.

Kwa kifupi walichofanya ni hadaa tu.
 
Mwenye barua ya kusema Wakurugenzi hawatasimamia Uchaguzi,aiweke hapa!
 
Kwanini CCM mnahangaika na Chadema tuu?
Chama kina mbunge mmoja tuu lakini CCM hampati hata muda wa kutawadha!
 
Kama yeye na chama chake wanajifanya au hawataki kuelewa kinacho zungumziwa, acha wananchi waelezwe na ndio watakao fanya uamzi.

Hakuna tena cha kuwaburuza wananchi kwa kutumia ulaghai; kama mnavyojifanyia ulghai nyinyi wenyewe ndani ya chama chenu, hata katika mambo rahisi kama kumchagua mpeperusha bendera wa chama kwenye uchaguzi mkuu.

Huyu Makala sasa anajionyesha kuwa hazimtoshi kichwani, kiasi kwamba hata uchaguzi wa serikali za mitaa nao anadai ulikuwa huru na wa haki.

Sasa CCM wanataka kurudia njia hiyo hiyo kudai uchaguzi mkuu nao utakuwa wa haki na huru.

Hivi hawa watu kweli zimo za kutosha vichwani kujaribu kuwaeleza waTanzania upuuzi ulio wazi kiasi hiki?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…