Makamba azungumza kwa mara ya Kwanza Bungeni.

Makamba azungumza kwa mara ya Kwanza Bungeni.

Hana lolote huyu
atakaa kunukuu vifungu vya biblia na msaafu mahali ambapo apatakiwi references tena kwa makosa

Huyu ndio anaprove failure ya Kikwete, Mimi sijui Kikwete alikuwa akifikilia nini eti kumpa mpaka ubunge mtu kama huyu.

Nadhani Kikwete haelewi maana na umuhimu wa nafasi za ubunge wa kuteuliwa na ndio maana anatoa tu kwa watu ambao hawafanyi mambo yanayotakiwa kutokana na kuteuliwa kwao

bwaha ha hah hahah hahahahahahaaaaaaaaaaaa
kuna tetesi nilisikia eti jeshini alikuwa mpishi...
kwi kwi kwi kwi kwi kwi kwiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Niliwahi kuipata hiyo email hapo chini na sikuitilia maanani..Lakini haya yamenikumbushia na mineonlea niilete hapa.

KASHFA NZITO YA KIKWETE. !!!!!


Baada ya kusoma kwa makini kwa siku nne mfululizo, kwenye forum yetu hii tukufu, na baada ya kuona kuwa uongozi wa forum hii tukufu umeamua kuwa kila anayeona uovu wa viongozi wa kisiasa na haswa wenyeviti wa vyama vya siasa ana haki ya kuleta ujumbe wake hapa bila kubugudhiwa kitu ambacho nakiheshimu sana kwenye ujenzi wa demokrasia na pia haki ya kupata habari kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya muungano ya Tanzania ibara ya 18.

Na pia nimeguswa kuandika ujumbe huu kutokana na kile nilichokiona kwenye gazeti la majira la jana (front page) na pia kauli iliyotolewa na katibu mkuu wa CCM ndugu Makamba kuunga mkono hoja iliyowekwa hapa forum na wanachadema! Kama ilivyorushwa kwenye taarifa ya habari ya channel ten jana saa moja jioni .

Makamba alisema kuwa viongozi wa upinzani waache kurusha mawe ile hali wao wako wakiishi kwenye nyumba za vioo!nimeshtuka na kuogopa kama huyu ndio anatakiwa kuonyesha njia ya kuweza kufikia maisha bora kwenye taifa hili , nashindwa kuamini kuwa huyu ndio dereva wa chama tawala !

Leo nimeona niweke ushahidi wangu hapa juu ya ufisadi wa ziada na au uovu uliotendwa na JK pamoja na timu yake wakati wa kuwania kuteuliwa na chama chake, na pia jinsi alivyotumia cheo chake cha waziri wa mambo ya nje kuendekeza ngono na kulisababishia taifa hili madhara makubwa ikiwa ni pamoja na mahusiano ya kidiplomasia kuwa mabaya.

Naanza kuweka hoja zangu na ushahidi wake kama ifuatavyo,

1.Kikwete wakati anagombea kuteuliwa kuwa mgombea wa CCM ,aliunda timu za aina mbalimbali ila kwa hapa nazungumzia timu yake ya uharamia ambayo aliiunda, aliunda timu ya kuwafanyia maasi wagombea wenzake na mojawapo ni hii iliyokuwa inaongozwa na mtu anayeitwa Gogo kutoka kule Bagamoyo.

Huyu alinunuliwa gari aina ya Nissan patrol ,na ndio mwanzo alitumika kupita kwenye misikiti mbalimbali na kutengeneza mtandao wa kiislamu,ila huyu Gogo ndio alihusika na aliongoza kikosi kilichohusika kumpora mke wa mzee Malecela fedha taslimu zaidi ya milioni mia mbili wakati anatoka dar kwenda dodoma kwa ajili ya kampeni. ENEO LA GAIRO.

Gogo akiwa na vijana wenzake walimteka mama Kilango nje kidogo ya mji wa morogoro na kumpora fedha hizo na pia kumfanyia mambo ya ajabu ambayo kwa mtu mzima kama mimi siwezi kuyaandika hapa.(ushahidi upo na nitautoa muda wowote kama utahitajika hapa ,niandikie kwenye PM yangu.)

2.Akiwa waziri wa mambo ya nje mwaka 2004 alipokwenda nchini marekani kuiwakilisha nchi kwenye kikao cha UN alifanya ngono na aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wa Uganda kitu kilichowafanya kutokuweza kuhudhuria mkutano kwa siku mbili mfululizo, na ndipo rais museven alimwandikia rais mkapa rasmi malalamiko yake na pia alimtimua kazi waziri huyo .

Hili linaifanya nchi yetu kutokuwa na mahusiano mazuri na serikali ya Uganda na haswa kati ya Kikwete na Museven na hili limechangia kwa kiasi kikubwa hata kutokufikiwa kwa shirikisho kwani Museven anaamini kuwa hawawezi kujadili mambo serious na JK kutokana na kutokwenda kuwakilisha nchi na badala yake ikawa ni kwenda kufanya ngono na waziri aliyetumwa na nchi nyingine bila hata aibu.

3.Kikwete akiwa na swahiba wake wa karibu anayeitwa Jack Gotham,wakiwa maeneo ya millennium towers hotel kijitonyama ,walimchukua binti wa mfanyibiashara mmoja wa jijini ambaye alikuwa anasoma shahada ya kwanza chuo kikuu cha DSM na kufanya naye ngono hapohapo hotelini na kumfanya kuchelewa kwenda kwenye ziara za kampeni kwani kipindi hiki kilikuwa ni wakati wa mchakato wa kampeni ukiwa unaendelea.

Huyu anaacha hata masuala ya maana na kwenda kumchukua binti wa rafiki yake ambaye amemchangia kiasi kikubwa cha fedha za kampeni zake na kufanya naye ngono.

4. Fedha chafu.
Kikwete aliingiza nchini kiasi kikubwa sana cha fedha chafu kutoka kwenye nchi za uarabuni na nyingine alizitoa Jamhuri wa Kidemokrasia ya Congo (DRC)kutoka kwa Joseph Kabila na fedha hizi ziliingizwa kupitia mkoani Kigoma na nyingine ziliingilia mkoani Mwanza .
Ujumbe wa watu wa kongo uliongozwa na Luten Jenerali Peter Gessimba Gabonne akiwa na wasaidizi wake watatu ambao walikuwa ni viongozi wa jeshi tiifu kwa Kabila.


Fedha hizi zilitolewa kwa masharti kuwa endapo angeshinda ni lazima ahakikishe kuwa Kabila naye anashinda kule Congo kitu ambacho alikifanya na hata kutumia pesa za taifa hili kwa ajili ya uchaguzi wa congo kwa wale mnaokumbuka Asha Rose Migiro alisema kiasi cha pesa zilizotolewa na misaada mingine ……..

5. Ngono.
JK akiwa na maswahiba wa mwanae wa karibu waitwao Benno (huyu kwa sasa anagombea ujumbe wa NEC ndani ya chama chetu),Said (huyu ni msaidizi maalumu wa kumsaidia mzee Makamba) ,Mussa (huyu alikuwa ni kiongozi mwandamizi wa mbio za mwenge mwaka huu), na Sisko (huyu ni chief protocol wa ikulu)wakiwa kwenye club mojawapo jijini dar,(ipo mkabala na red cross-barabara ya Alhassan mwinyi) kabla ya mchakato wa kampeni kuanza rasmi walimchukua binti anayeitwa Hadija ……aliyekuwa anasoma UDSM (Third year Sociology) na pia ni mfanyibiashara wa mjini Arusha, ila alikuwa pia ni mke wa aliyekuwa meneja msaidizi wa kituo kimoja cha kimataifa nchini , na kufanya naye ngono .

Kitendo hiki kilimfanya Hadija kuachika /kuachwa na mumewe na kumnyanganya magari pamoja na mtaji kitu kilichopelekea binti huyu kuishi kwa taabu hadi JK alipoweza kushinda urais wa nchi na kumpangishia nyumba maeneo ya Kijitonyama ambako anaishi hadi sasa.
Pia JK alimwamuru Benno ambaye ni afisa mwajiri wa jumuiya ya UVCCM kumwajiri bint huyu makao makuu na kwa sasa ameajiriwa kama katibu wa uhamasishaji wa taifa cheo ambacho hakipo hata kwenye katiba ya umoja huo, kwa toleo la 2003 ambalo ninalo hapa.

6. Ngono ,
Alifanya ngono iliyoligharimu taifa hili zaidi ya shilingi milioni mia nne Na themanini, (480 milioni) akiwa kule Zanzibar Hotel Kempinski pale alipokuja na mkewe mpya kutoka uarabuni na kukaa naye kwenye mapumziko hayo ambayo yaliliingizia taifa hasara hiyo kwa muda wa siku 9 tuu.
Mkuu wetu wa nchi anatumia rasilimali zetu kwa ajili ya kujistarehesha yeye binafsi na wanawake zake kutoka huko uarabuni.

7.Ubadhirifu.
Aliweza kujichukulia eneo ndani ya mbuga za wanyama kule Serengeti na sasa anajenga hotel ya kisasa nah ii anaijenga yeye kwa ubia na mke wake huyo wa uarabuni akishirikiana na mashemeji zake hao , swali la kujiuliza ni je?huu mkataba hautaishia kwenye kuliuza taifa hili?
Mke anaenda kupewa mahari ya rasilimali zetu? Kama kila rais akioa ni sharti atoe sehemu ya mbuga zetu je? Mpaka lini tutakuwa tunachezea taifa kwa faida za kuoa ama kupata ngono!

Huyu ndio mwenyekiti wa chama chetu na bado tunamwona kama malaika aliyetoka mbinguni kama sio kuzimu!

Nitakuja na taarifa pia za kina juu ya ndugu Nchimbi ambaye naambiwa kuwa anaweza kuwa ndio katibu mkuu wa chama chetu, jambo ambalo mimi nalipinga kwa nguvu zote kwani huyu naye anaendelea kufanya mambo ya aibu na wanafunzi wa vyuo mbalimbali vya umma nchini.

Ni mimi mwanachama mtiifu na mpenda maendeleo ya chama chetu kitukufu.
 
Kuna mtu mwenye picha ama data za hao kina GOTHAM NA GOGO?
Maana huu kama si UMAFIA NI NINI?

Halafu bao MNASEMA TUNA UONGOZI VALID?
 
We need something new hii mbona ilisha expire ages ago!
 
HANSARD YA ALICHOSEMA MAKAMBA .




MHE. YUSUFU R. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekaa muda mrefu sana bila kuzungumza, nilikuwa shuleni, maana sisi tuliozoea kuzungumza kwenye mikutano ya "pasua baba" ukiingia hapa unaweza kuharibikiwa. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hii ni mara yangu ya kwanza kuzungumza katika Bunge hili Tukufu, naomba nichukue nafasi kwanza ya kumshukuru Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuniteua kuwa Mbunge. Deni la fadhila hulipwa kwa fadhila. Nina deni kubwa sana kwake, natafuta namna ya kulilipa, sijui… lakini nafikiri namna nzuri ya kulipa deni hili ni kujitahidi kwa uwezo wangu wote kutumia nchi yetu na Chama changu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesoma Maandiko Matakatifu ndani ya Biblia yanasema, "anayetamani Uaskofu, anatamani kazi njema". Sasa leo nazungumza Spika hayupo, lakini nafikiri yatamfikia. Kama anayetamani Uaskofu anatamani kazi njema, basi anayetamani Uspika naye anatamani kazi njema, lakini ni ngumu. Kwa hiyo, nataka nichukue nafasi hii kumpongeza Spika na mimi naridhika na namna anavyotuongoza. Nafurahi hasa kwa kuzingatia kwamba ni Spika anayetoka Chama changu! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba vile vile nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mizengo Pinda kwa kuteuliwa kuwa Waziri Mkuu. Siku njema, huanza mapema, ameanza vizuri! Labda niseme tu kwamba pengo la jino la dhahabu limezibwa kwa jino la dhahabu! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Nabii Yeremia anapewa unabii, aliogopa sana, lakini Mwenyezi Mungu akamwambia usiogope, nitatia maneno yangu katika kinywa chako na wewe utazungumza kwa niaba yangu, ndipo Yeremia akapewa utume. Kwa hiyo, hayupo hapa, lakini nataka nimwambie kwamba asiogope, huyo anayemteua kwa kawaida huweka maneno katika kinywa chake ambaye ni Rais na Chama chake. Kwa hiyo, mimi nafikiri atafanya vizuri, tumtie moyo! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, uniruhusu vile vile na mimi niwashukuru Wabunge wa Chama changu. Ninapotembelea Jimbo langu la Uchaguzi, ninawakuta huko wanajitahidi sana katika kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Mimi nataka niwaondoe hofu, tukienda namna hii, 2010 kazi ni rahisi. Tukiendelea namna tunavyokwenda hivi sasa, kazi yetu mwaka 2010 ni rahisi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, naomba na mimi niseme mambo machache na wala sitasema mambo makubwa sana. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, mtaniwia radhi, Mzee Ngombale alipokuwa anachangia hapa Bungeni, alisema anaipongeza Serikali ya Awamu ya Nne kwa kazi nzuri inayoifanya na hasa Mheshimiwa Rais kwa kusimamia utekelezaji wa Ulani ya Uchaguzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, siku mbili baada ya hotuba ya Mzee Ngombale, alisimama Mbunge mwingine (kwa staili ile ya waandishi wa habari, jina ninalo) akasema sisi wenzenu wa Kambi ya Upinzani, masikio tunayo, macho tunayo na midomo tunayo. Haya tunayoyasema tunayaona, haya tunayoyasema tunayasikia, akamaliza. Lakini na mimi nataka niseme, asubuhi yake gazeti liliandika "Mzee Ngombale awekwa kitanzini".

Sasa na mimi nataka niseme, unaweza ukawa na macho, unaweza ukawa na masikio, lakini unapoona mambo mazuri yanayofanywa na Serikali ya CCM, unaweza ukayafumba tu usione. Unaweza ukawa na masikio, lakini ukayaziba, ukayatia hata na pamba ili usisikie mambo mazuri yanayozungumzwa juu ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi. Hata ukaambiwa kwamba pale Dodoma kinajengwa Chuo Kikuu, unaweza lile jengo ukalipa kisogo usilione. Unaweza hata kitabu kizuri hiki cha bajeti tuliyosomewa leo, mipango mizuri hii ya kilimo usiione, ukaona Ibara moja ndogo tu ambayo kwako unaona ina upungufu, ukakazana na hiyo, ukashindwa kujua kwamba hotuba yote hii imetengenezwa kwa kuzingatia Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ndugu zangu kuwa na masikio si hoja, kuwa na macho si hoja. Sasa ninachotaka kusema ni kwamba ukijua kulaumu, ujue kusifu, vinginevyo wenzako watakwambia una kilema, maana yale unayoyasema hayafanyiki, yanafanyika hata kwenye Jimbo lako, watu wako wanaona, wewe huoni! Nafikiri mmenielewa! Nasema ukijua kulaumu, ujue kusifu, vinginevyo utaambiwa una kilema!

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, nataka sasa nimpongeze Mheshimiwa Rafiki yangu Wasira kwa hotuba nzuri na ili nisije nikasahau, basi naunga mkono.

Mheshimiwa Mwenyekiti, humu ndani tunaye bingwa wa kuandika maandiko mbali mbali ya Chama cha Mapinduzi. Tulianza mwaka 1972 na Siasa ni Kilimo, kitabu ninacho hapa. Lakini kabla ya 1972 kulikuwa na Mwongozo wa 1971 umezungumza kilimo. Azimio la Iringa limezungumza kilimo, Sera za CCM katika miaka ya 1990, zinazungumza kilimo, Ilani ya Uchaguzi ya Chama chetu inazungumza kilimo. Sasa naomba mniruhusu nilitazame lile Azimio la Iringa la Mwaka 1972, Ibara ya 36, inasema hivi; "Watumishi wa kilimo hawawezi kuwepo katika kila kijiji wakati ule ule wanapohitajika, lakini maarifa ya kilimo lazima yaenezwe kila mahali hivi sasa, 1972".

Mheshimiwa Mwenyekiti, Azimio hilo hilo la Iringa linasema "kazi za viongozi (Ibara ya 36) ni nne:- Ya kwanza, wajifunze wao wenyewe kanuni za kilimo". Hizi humu ndani, tujifunze sisi wenyewe kanuni za kilimo. Sina hakika Wasira unazijua kwa kiasi gani! Nimemtaja ni rafiki yangu, hatanipeleka kokote! Pili, "wawaeleze wananchi kwa nini Kilimo cha kizamani hakifai tena na kuwafanya wakulima wawe na hamu ya kujifunza na kutumia maarifa mapya". Tatu; "kuhakikisha pembejeo na zana nyingine zinawafikia wakulima kwa wakati unaofaa". Hivyo ndivyo tunavyoelekezwa kwamba sisi wenyewe tujifunze kanuni za kilimo bora. Sasa ukisoma hotuba iliyotolewa hapa ukurasa wa 20, Ibara ya 31, Waziri anatuambia mwaka 2007/2008 wataalam wa ugani 309 waliajiriwa, lakini lengo ni 2500.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nafikiri hata ukifikisha lengo hili la 2500, mimi kwangu nafikiri namna nzuri ambayo tunaweza tukafanya… nchi hii ina viongozi wengi sana, viongozi wa CCM wanaanzia kwenye Shina, Kata, Wilaya, Mkoa. Kwa maelekezo ya kitabu hiki ni kwamba sisi wenyewe lazima tuongoze kwa mfano. Hivi ukilitazama shamba la rafiki yangu Siraju, ni mfano? Watu wako wanaweza wakaja wakajifunza kwenye shamba lako? Usikasirike! Wewe mtani wangu! Shamba la rafiki yangu Lowassa, ng'ombe nakubali, maana ng'ombe wako nimewaona. Lakini shamba lako je? Shamba la rafiki yangu Kapuya ni mfano? Nataka nichukue nafasi hii, Waheshimiwa Wabunge wenzangu, tunaandika sana, tunasema sana, lakini tatizo ni kwenda kutekeleza yale ambayo tunayasema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma kitabu cha Mathayo 23 kinasema; "maneno ya Makuhani hawa na Mafarisayo, yasikilizeni kwa sababu wamekaa katika kiti cha Musa, lakini kwa mfano wa matendo yao msifuate. Wananena, hawatendi, wanawatwika watu mizigo mikubwa, wenyewe hawagusi hata kwa vidole". Ndani ya Quran maneno hayo yamo, kwa wale wenzangu waliobobea, wakina Siraju. Yanasema: "Yaa aiyuhalladhina amanu limatakuluna malatafaaluna". "Enyi mlioamini mbona mnasema maneno ambayo ninyi wenyewe hamtendi?". Sasa sisi tunazungumza kilimo, mashamba yetu mabaya na wananchi wanatusikiliza hapa! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya CCM katika miaka ya 1990 inasema hivi; "Serikali inatakiwa kutambua na kuwaenzi wakulima kwa mfano. Pili, kuanzisha mashindano ya kilimo, tatu; kuwatumia wakulima bora kuwafundisha wakulima wengine. Kwamba hata wale wakulima bora ambao tayari kwenye maeneo yetu tulionao wanaweza kuwa Maafisa Ugani kwa kuwafundisha wakulima wengine, wapo? Kwenye mashindano ya Nane Nane, TASO inaendesha mashindano, wanapatikana wakulima bora kutoka kila vijiji na kata, lakini je, wanaporudi kule, tunawaenzi? Je, tunawatumia kuwafundisha wengine? Hatufanyi! Lakini maandiko yako pale, kila mtu akiandika, anaya-quote, kuyatekeleza hamna! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ilani ya Uchaguzi ya 2005, 31(e) inazungumza zawadi, tuzo kwa Mikoa na Wilaya. Inasema hivi; "Serikali itatakiwa kuhimiza kutoa vivutio, zawadi na tuzo kwa Mikoa na Wilaya ambazo wakulima wake wataweza kuongeza maradufu tija na mazao yanayovunwa katika heka katika kipindi cha Ilani hii. Msisitizo utawekwa kwenye mazao ya mahindi, mpunga, migomba, kunde, tumbaku, chai". Inaendelea; "viongozi waongoze mapinduzi ya kilimo kwa kutena wao wenyewe". Ni sura ya 9 ya Ibara ya 132.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo Mikoa ambayo tayari imekwishaonyesha mfano katika uzalishaji wa mahindi; Rukwa, Mbeya, Iringa na Ruvuma. Mimi sikumbuki, labda Wiziri atakapomaliza atuambie, mmewatia moyo kwa tuzo gani!

(Hapa kengele ya pili ililia kuashiria kumalizika muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Makamba, hiyo ni kengele ya pili, mchango wako ni mzuri sana, lakini muda tu.

MHE. YUSUFU R. MAKAMBA: Nilikwisha unga mkono hoja!

MWENYEKITI: Tunashukuru sana kwa hilo!

MHE. YUSUFU R. MAKAMBA: Asante sana! (Makofi)
 
Jamani muelewe kuwa huyo keshaongea na NEC...NEC ni mafisadi..Sasa watu wanataka wasikie nini?
Yani watu wanasema hiki ni kinyesi lakini hakina noma kwani sahani ni safi?

Mwanzo ulikuwa huu...Lakini maajabu kuna wanaofikiri atasema la maana.
Labadatusubiri tu pumba za kuwabana kwenye kampeni..Lakini kimtizimo...Ufisadi walioufanya wala haina haja ya sisi kupewa habari nyingine zozote zile zenye kuhusiana na wanachosema ccm bungeni...Kwani si ni mchezo wa kuigiza ama?

Viongozi wa serikali sasa kujieleza CCM

By Habari Tanzania | Published Today | Habari za Kitaifa | Unrated

na Rahel Chizoza, Dodoma



CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeanzisha utaratibu mpya wa kuwaita watendaji wa serikali kutoa taarifa za kiutendaji za serikali katika vikao vya Halmashauri Kuu ya chama hicho.
Akiongea na waandishi wa habari mjini hapa jana, Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, alisema lengo la hatua hiyo ni kuwawezesha wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM kufahamu ni kwa kiasi gani ilani ya uchaguzi ya chama hicho inatekelezwa na watendaji wa serikali.

Makamba alisisitiza kuwa kipimo pekee cha kuona jinsi ilani ya uchaguzi ya CCM inavyotekelezwa katika Awamu ya Nne ni kupokea taarifa na kuona mafanikio yaliyofikiwa katika malengo ya kuleta maendeleo ya nchi katika kipindi hicho.

Makamba alisema katika kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM kilichofanyika mwanzoni mwa wiki na kuongozwa na Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete, jumla ya taarifa saba za serikali, ziliwasilishwa na kujadiliwa na kamati hiyo.

Mojawapo kati ya taarifa zilizowasilishwa ni taarifa ya mpango wa kuingiza shule za sekondari wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 2006, ambapo taarifa hiyo ilionyesha kuwepo kwa mafanikio kwa asilimia 89.

Alisema kwa mujibu wa taarifa hiyo ya elimu katika kipindi cha miezi sita, jumla ya shule 1,040 za sekondari zimejengwa nchini kote na kuwawezesha wanafunzi wengi waliokuwa wamefaulu na kukosa nafasi ya kuendelea, kupatiwa nafasi za masomo.

Alisema wanafunzi waliofaulu darasa la saba ni 468,252, lakini waliopata nafasi kwa mujibu wa shule zilizokuwapo wakati huo ni 235,905. Hali hiyo iliifanya serikali kuandaa utaratibu maalumu wa kuhakikisha wanafunzi wote waliofaulu wanapatiwa nafasi ya kuendelea na masomo ya sekondari.

Alibainisha kuwa mwaka 2005, wakati Serikali ya Awamu ya Nne inajiandaa kuingia madarakani, kulikuwa na shule za sekondari 1,202 nchi nzima, lakini kwa kipindi cha miezi 18 tangu serikali hiyo ishike hatamu, kumekuwapo na ongezeko la shule 2,269 na kufanya jumla ya shule za sekondari nchini ifikie 3,471.

Makamba alisema sambamba na ongezeko hilo la shule za sekondari, kumekuwa pia na ongezeko la walimu ambapo jumla ya walimu 6,668, sawa na asilimia 68.95, walipatiwa ajira mpya, ambapo serikali inaendelea na mpango wa dharura wa kuajiri walimu wapya 3,305 ili kutimiza malengo iliyojiwekea.

Kwa upande wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Makamba alisema kitaanza Septemba mwaka huu na kitadahili wanafunzi 1,000, ambapo idadi hiyo itaongezeka mwaka hadi mwaka na kufikia wanafunzi 40,000 ambao wamekusudiwa kujiunga.

Alisema hivi sasa miundombinu ya kuanzia katika chuo hicho ipo tayari, sanjari na uongozi wa chuo, ambapo alibainisha kuwa vikao vya CCM havitakuwa vikifanyikia katika ukumbi wa Chimwaga kwa sasa, badala yake vitafanyikia kwenye kumbi nyingine.

Halmashauri Kuu ya CCM pia ilipokea taarifa ya mapinduzi katika kilimo ambayo ilibainisha kuwa jumla ya sh trilioni 2.5 zitatumika katika kuleta mapinduzi ya kilimo nchini katika kipindi cha mwaka 2006/2007 hadi 2012/2013.

Kupitia mpango huo wa mapinduzi ya kilimo, wananchi watawezeshwa kutumia zana za kisasa zaidi katika kilimo hivyo kuzalisha zaidi na kuondokana na tatizo la uhaba wa chakula.

Makamba alisema kuwa kwa mujibu wa mpango huo, kiwango cha eneo lililo chini ya kilimo cha umwagiliaji kitaongezwa kutoka hekta 250,000 hivi sasa na kufikia hekta milioni moja ambazo zitawawezesha wananchi kuzalisha hata kama hakuna mvua za kutosha katika msimu wa kilimo.
 
Back
Top Bottom