Kenya 2022 Makamishina IEBC: Jumla ya kura zilizohakikiwa ni 100.1% ndio tunauliza hiyo ziada sawa na kura 143,000 imetoka wapi?

Kenya 2022 General Election
Cha kushangaza ni kuwa Odinga ana nakala ya matokeo ya urais ya vituo vyote vya uchaguzi na kura alizozipata anajua kuwa hazijatosha, ndiyo maana hana tuhuma ya kuibiwa kura, na hata akiulizwa kura zako ni ngapi hawezi kusema!
 
Raila si ni engineer, yule? Anashindwaje kujiridhisha mwenyewe before aje kulalamika? It means ndiyo watakuwa wakifanya hesabu za fedha ya miradi kwenye mikataba, siyo? Kama ndivyo, basi hafai kuwa president.
 
Kilikuwa na ulazima gani wa kukadiria kwa 2 decimal point?
 
Cha kushangaza ni kuwa Odinga ana nakala ya matokeo ya urais ya vituo vyote vya uchaguzi na kura alizozipata anajua kuwa hazijatosha, ndiyo maana hana tuhuma ya kuibiwa kura, na hata akiulizwa kura zako ni ngapi hawezi kusema!
Tatizo alishaaminishwa na kuamini 100% kwamba yeye ndiye the 5th! Unajua mshtuko wa ghafla si jambo la kitoto. Mara nyingi, katika hali hiyo, huwa akili zina-tendency ya kuhamia DRC (siyo Democratic Republic of Congo, bali Department of Retrogressive Cognition).
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya 0.01 na 0.01%.

0.01% = 0.0001 = 1/10,000

0.01% ya 14,000,000 = 1/10,000 = 1,400
Siyo 0.01% ni 0.1% ambayo kimsingi ni sawa na kura 14000
Soma hapo juu, mkuu
 
Hata ungekua ww ndo Chibukati uache hela ya bure kwa kumtangaza Baba ambae akiingia anaweza kukuletea figisu zaidi?
 
Kilikuwa na ulazima gani wa kukadiria kwa 2 decimal point?
Hiyo ni kawaida kwenye summary, vinginevyo asilimia za Ruto ni 50.489885989% na Odinga ni 48.849059388%. Wote walipandishiwa decimal point ya 2 kuwa 9 kwa Ruto, na kuwa 5 kwa Odinga. Hakuna mgombea kati ya Ruto na Odinga aliyeathirika kwa kutumia decimal point mbili!. Kama asilimia za kura za wagombea wote zikijumlishwa bila ku-round-off to two decimal points jumla inakuja 100%.

Nilitegemea Odinga aseme kuna kura zangu kadhaa nimeibiwa kitu ambacho hawezi kuthubutu!! Akubali tu kuwa mzee mzima kapigwa mweleka pamoja na mbeleko ya Uhuru Kenyatta! (ambaye kwa aibu pia yuko kimyaaaa!!)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…