Makampuni na Mawakala wa pikipiki za TVS, Hero, Bajaj nk, mnatukosea sana Watanzania!

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
26,961
Reaction score
77,890
Inafika kipindi mtu akisikia pikipiki ya TVS au Hero, anachowaza ni zile za bodaboda.

Tunajua mnatoa vyuma vizuri tu kwa bei rafiki, lakini kwanini hamzileti Tanzania?

Mfano hii pikipiki ukiambiwa ni TVS unakataa, na ukaambiwa mpya ni $3,000 tu kabla ya usafiri na kodi.

Kwamba hatuwezi kununua au mnahisi Watanzania wengi hatuna flavor ya pikipiki kama usafiri binafsi?

Kwa mfano mkazi wa Dar, wengi tu wangependezwa na kununua pikipiki za kisasa zenye muonekano mzuri, wazitumie kama chombo kikuu cha usafiri au usafiri wa backup incase kukiwa na foreni au weekend.

Wafanyabiashara/Mawakala mnaotoa bike India mngejaribu na hii fursa.

Tunaishia kuuziwa used Honda za 2013 kwa million 10+ na watoto wa mjini.
 
Yaani badala ya kutuletea pikipiki, wenyewe wanatuletea vibao vya kukunia nazi!! Hizi ni dharau za hali ya juu sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…