sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,407
- 19,264
Ni nani ambae hakumbuki ule mtelezo wa app ya tala iliyokuwa ikitoa mkopo swafi kabisa wa elf 20 lakindi kwa mbongo ikawa ni kama zawadi.
Wabongo walichukulia kama zawadi hawakua na muda wa marejesho, haya meseji za vitisho zilivyoanza kutumwa ndio kwanza mtu anaweza pozi la 4 huku akishushia kinywaji na kucheka.
Kwa wenzetu huko wabishi Nigeria, haya matukio yaliwahi kutokea na watu walitumia fursa hizo kujipatia pesa za kula bata badala ya mikopo, mesej za vitisho tupa kule.
Sasa klichopo kwa sasa kuna dawa hii imesaidia kwa kiasi kikubwa (sio 100%) kufanya mtu alipe, unapewa mkopo hata laki 5 kupitia app lakini kwa namna wanayoijua watakusanya namba zako kuanzia wazazi, ndugu, ustadh / mchungaji, mme / mke wako, watoto wako, majirani, hadi ma ex, n.k.
Ukichelewa kurudisha mkopo wanatuma mesej kwa hao watu. Meseji wanaweza kutuma kama hii kwa mama yako
Habari yako, tunatoa onyo la mwisho kwa xxx arejeshe mkopo aliouchukua kwetu, jitihada za kumtafuta alipe zimeshindikana na ameonyesha wazi kabisa ni jeuri, hivi sasa ni mkimbizi anaekwepa mkono wa sheria kwa kukaidi ombi la kwenda kituo cha polisi kujisalimisha, tumeamua tukutumie meseji hii ili uweze kumsihi alipe deni lake ili tumalizane naye, meseji hii umeipokea kwasababu xxx aliweka namba yako wewe kama mtu wa alipokuwa anachukua mkopo"
Mesej hio kuna baadhi ya vitu ni uongo tu kama hapo kwenye kutafutwa na polisi, watu wako wataanza kukusihi ulipe na wanaweza kukusaidia kabisa lakini ni aibu, heshima yako itakuwa imeshuka mno, kuna kipindi hata mkikutana unaanza kuambiwa kama umekula maana wanadhani umefulia, mda mwengine unapigiwa simu na ndugu wakutaftie kibarua maana wanajua huna kazi labda, kwa ex wako ndio uakuwa kituko tu hasa pale walipoandika umeweka namba yake kama mtu wa karibu anakuona boya tu, mchungaji / ustadh nae atakwambia unahitaji maombi n.k. yaani hwahima yako inashuka watu wanakuona upo hoi kiuchumi.
Wabongo walichukulia kama zawadi hawakua na muda wa marejesho, haya meseji za vitisho zilivyoanza kutumwa ndio kwanza mtu anaweza pozi la 4 huku akishushia kinywaji na kucheka.
Kwa wenzetu huko wabishi Nigeria, haya matukio yaliwahi kutokea na watu walitumia fursa hizo kujipatia pesa za kula bata badala ya mikopo, mesej za vitisho tupa kule.
Sasa klichopo kwa sasa kuna dawa hii imesaidia kwa kiasi kikubwa (sio 100%) kufanya mtu alipe, unapewa mkopo hata laki 5 kupitia app lakini kwa namna wanayoijua watakusanya namba zako kuanzia wazazi, ndugu, ustadh / mchungaji, mme / mke wako, watoto wako, majirani, hadi ma ex, n.k.
Ukichelewa kurudisha mkopo wanatuma mesej kwa hao watu. Meseji wanaweza kutuma kama hii kwa mama yako
Habari yako, tunatoa onyo la mwisho kwa xxx arejeshe mkopo aliouchukua kwetu, jitihada za kumtafuta alipe zimeshindikana na ameonyesha wazi kabisa ni jeuri, hivi sasa ni mkimbizi anaekwepa mkono wa sheria kwa kukaidi ombi la kwenda kituo cha polisi kujisalimisha, tumeamua tukutumie meseji hii ili uweze kumsihi alipe deni lake ili tumalizane naye, meseji hii umeipokea kwasababu xxx aliweka namba yako wewe kama mtu wa alipokuwa anachukua mkopo"
Mesej hio kuna baadhi ya vitu ni uongo tu kama hapo kwenye kutafutwa na polisi, watu wako wataanza kukusihi ulipe na wanaweza kukusaidia kabisa lakini ni aibu, heshima yako itakuwa imeshuka mno, kuna kipindi hata mkikutana unaanza kuambiwa kama umekula maana wanadhani umefulia, mda mwengine unapigiwa simu na ndugu wakutaftie kibarua maana wanajua huna kazi labda, kwa ex wako ndio uakuwa kituko tu hasa pale walipoandika umeweka namba yake kama mtu wa karibu anakuona boya tu, mchungaji / ustadh nae atakwambia unahitaji maombi n.k. yaani hwahima yako inashuka watu wanakuona upo hoi kiuchumi.