Pre GE2025 Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Othman Masoud: Hakuna hata kero moja ya Muungano ya maana iliyotatuliwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Heri ya Mwaka Mpya wanajukwaa!

Tuje hapa. Kumbe zile kelele nyingi za kudai kwamba kero za Muungano zimeanza kutatuliwa kwa kasi kumbe ilikuwa danganya toto. Mbona hii sasa ni tabu tupu!
=========================

“Kwa upande wa kero za Muungano, hakuna hata kero moja ya maana iliyotatuliwa. Aidha, waliojipa mamlaka Zanzibar hawaonekani na shauku ya kudai kutatuliwa kwa kero za muda mrefu na hata zile zinazoathiri maisha ya watu kila siku.

Soma Pia: - Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?


Ni dhahiri kwamba kama Zanzibar itaachwa iendelee na mfumo na hali ya sasa ya uendeshaji wa nchi, haitokuwa na mustakbal mwema na inaweza kufikia kuirithisha Zanzibar kwa kizazi kijacho ikiwa imekosa misingi madhubuti ya kiuchumi, utawala mwema na uzalendo kwa watu wake. Zanzibar inaweza kurithishwa mfumo uliojaa ufisadi na kukosa weledi wa uendeshaji Serikali na hivyo kuhatarisha mustakbal wake. Ni kwa sababu hizo ndio maana nasema, Zanzibar inahitaji kunusuriwa”- Othman.

Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, na Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Taifa, Othman Masoud Othman akitoa salamu za Mwaka Mpya 2025.
 
Hiyo ni gia ya kutaka kuinyonya zaidi Tanganyika kuliko inavyonyonywa kwa kasi ya sasa.

Mafuta yameondolewa katika mambo Ya muungano kana walivyodai; mikopo wanapata kwa formula waloyoiafiki na hawalipi mikopo hiyo anayelipa ni Tanganyika; misaada inayokuja Tanzania wanapata lion share bado haridhiki.

Kila kitu cha zanzibar ni mali ya zanzibar lakini vitu vya Tanganyika ni mali ya wote bado hafurahii.
 
Wanzanzibar wanawashwa sana na hichoo kisiwa chaoo wangese sana wazazibar wote
Wewe endelea tu kutumia zile dawa zako za huo ugonjwa wako wa akili ukiziwacha utarudishwa tena Mirembe pole sana
 
Kumeanza Kuchangamka 2025 Mpaka October Vumbi Litatimka
Uchaguzi Unakuja Karata Zichangwe Vema, Mtu Hataki Kulamba Mav*
 
Chama walichopigania kwa jasho damu na mateso makubwa Maalim Seif,Mloo na Babu Duni kinaenda kufa mikononi mwa huyu mtu asiye na ushawishi wowote
 
Kero kubwa ya muungano ni muungano wenyewe. Uvunjike Kila mtu awe na Amani wabaki kupambana unguja na Pemba .
 
Wanzanzibar wanawashwa sana na hichoo kisiwa chaoo wangese sana wazazibar wote
Kabla ya 1994 kulikuwa na tanganyika kwahiyo ukivunjika Muungano hauwezi kuishi bila ya Zanzibar ?
 
Wazanzibari kwa awamu hii ya mzanzibari mwenzenu kuitawala bara, mnafaidi mno tena mno. Hayo majenzi ya :-
1. Barabara zote kuwa za lami.
2. Mabandari makubwa na ya kisasa kama Mangapwani.
3. Viwanja vya ndege vya kisasa.
4. Fyovers kila Kona mpk kwenye chochoro za kwenda mashambani.
5. Majengo yote ya shule na hospitali kubadilishwa kuwa MAGHOROFA.
6. Viwanja vya michezo vya kisasa.

Yote haya yamewezekana kwasabb mzanzibari mwenzenu anachepusha fedha toka bara kuja huko Zanzibar.

Bora mkae kimya.
 
Kwahisani ya Gazeti la Mwananchi

Mwaka 2023 kuoijengwa jengo la Uhamiaji kubwa Zanzibar wakati wa sherehe za Mapinduzi
Mwaka 2025 Kunajengwa jengo jingine na CHUO CHA UHAMIAJI katika seherehe za Mapinduzi

Mwaka 1964 kulikuwa na Maafisa Uhamiaji 25 kwa Zanzibar yote
Mwaka 2024 kuna Maafisa Uhamiaji 805 kwa Zanzibar yote

Kuna port of entry 4 kwa maana Bandari na Airport 2 Unguja na Pemba. Kuna port of entry zaidi ya 20 Kwa Tanganyika. Je, Wafanyakazi wa Uhamiaji wa JMT ni kiasi gani kwamba Zanzibar ina 805?

Mapato ya Uhamiaji kutoka Zanzibar hayaingii katika JMT. Majengo na Watmishi ni kutoka JMT ambayo ni Tanganyika

Shughuli za Uhuru wa Tanganyika ziliahirishwa kwa ajili ya gharama. Shughuli za Mapinduzi zinafanywa tena kwa Gharama za Tanganyika, kwa kusafirisha viongozi na Miradi Mikubwa inayodhaminiwa na JMT

Hizi kelele za kuonewa zifike mwisho, tunahitaji Tanganyika

JokaKuu Mag3
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…