the guardian 17
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 395
- 570
Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango amewataka wananchi wa Kijiji cha Kasumo wilayani Buhigwe mkoani Kigoma kuutambua na kuuthamini mchango wa Serikali katika maendeleo ya huduma za kijamii wilayani humo.
Makamu wa Rais amesema hayo alipotembelea ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Kahimba iliyopo katika kijiji hicho, na kuongeza kuwa kwa muda mrefu Wanakasumo na maeneo jirani walikuwa wakisafiri umbali mrefu kufuata huduma za kijamii, lakini sasa huduma hizo zimesogezwa karibu zaidi na wananchi.
Dkt. Mpango amesema ujenzi wa barabara za lami, madaraja, zahanati, shule na huduma za maji ni jitihada za Serikali katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, hivyo wananchi wanapaswa kushukuru kwa kumpigia kura za ndio katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Kwa wanafunzi walioanza kusoma katika shule hiyo ya sekondari ya Wasichana Kahimba, Dkt. Mpango amewataka kutumia vizuri nafasi waliyopata kwa kusoma kwa bidii ili shule hiyo iweze kutoa wataalamu wazuri kama ilivyo kwa shule nyingine kubwa nchini.
Makamu wa Rais ameahidi kutoa zawadi shuleni hapo kwa wanafunzi watano wa kwanza katika mitihani ya mwisho ya kila mwaka pamoja na kwa walimu watakaofaulisha vema masomo yao, ikiwa ni motisha ya wanafunzi hao kusoma kwa bidii.
Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Source: TBC Digital
Makamu wa Rais amesema hayo alipotembelea ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Kahimba iliyopo katika kijiji hicho, na kuongeza kuwa kwa muda mrefu Wanakasumo na maeneo jirani walikuwa wakisafiri umbali mrefu kufuata huduma za kijamii, lakini sasa huduma hizo zimesogezwa karibu zaidi na wananchi.
Dkt. Mpango amesema ujenzi wa barabara za lami, madaraja, zahanati, shule na huduma za maji ni jitihada za Serikali katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, hivyo wananchi wanapaswa kushukuru kwa kumpigia kura za ndio katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Kwa wanafunzi walioanza kusoma katika shule hiyo ya sekondari ya Wasichana Kahimba, Dkt. Mpango amewataka kutumia vizuri nafasi waliyopata kwa kusoma kwa bidii ili shule hiyo iweze kutoa wataalamu wazuri kama ilivyo kwa shule nyingine kubwa nchini.
Makamu wa Rais ameahidi kutoa zawadi shuleni hapo kwa wanafunzi watano wa kwanza katika mitihani ya mwisho ya kila mwaka pamoja na kwa walimu watakaofaulisha vema masomo yao, ikiwa ni motisha ya wanafunzi hao kusoma kwa bidii.
Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Source: TBC Digital