Makamu wa Rais Dr. Philip Mpango awasili Marekani, Kushiriki Mkutano wa UNGA 77

Makamu wa Rais Dr. Philip Mpango awasili Marekani, Kushiriki Mkutano wa UNGA 77

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amewasili Jijini New York nchini Marekani ambapo anatarajia kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Baraza Kuu la 77 la Umoja wa Mataifa (UNGA).

Makamu wa Rais anatarajiwa kuhutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa katika Ukumbi wa Mikutano wa Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani tarehe 22 Septemba 2022.

Aidha Makamu wa Rais ataongoza Ujumbe wa Tanzania katika Mikutano mbalimbali inayohusu Uchumi, Elimu, Afya, Demokrasia na Malengo ya Maendeleo Endelevu ambayo Tanzania imealikwa na nchi washirika, Taasisi za kimataifa na Asasi binafsi.
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amewasili Jijini New York nchini Marekani ambapo anatarajia kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Baraza Kuu la 77 la Umoja wa Mataifa (UNGA).

Makamu wa Rais anatarajiwa kuhutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa katika Ukumbi wa Mikutano wa Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani tarehe 22 Septemba 2022.

Aidha Makamu wa Rais ataongoza Ujumbe wa Tanzania katika Mikutano mbalimbali inayohusu Uchumi, Elimu, Afya, Demokrasia na Malengo ya Maendeleo Endelevu ambayo Tanzania imealikwa na nchi washirika, Taasisi za kimataifa na Asasi binafsi.
Hili la rais yuko UK, makamu yuko NY kwa maoni yangu ni muendelezo wa lile tatizo la upangaji wa vipaumbele vyetu, baada ya kumuona Rais Samia amekwenda UK, then mimi nilimpangia ratiba hii Rais Samia kuhudhuria mazishi ya malikia Elizabeth II

Shughuli ya mazishi ya Malkia inaisha leo, kesho ilikuwa atoke UK na kutimba NY kama mwenzie Ruto. Unless ilikuwa ni mipango ya muda mrefu iliishapangwa VP atamuwakilisha UNGA, ratiba ya msiba ndio ikaingilia!.

Ila tukubali, tukatae, kwenye cost cutting za trips trips JPM alikuwa mzuri!, kwa umasikini wetu, we didn't have to send two different delegations to two separate events ambazo ziko just two days apart, one delegation would have been enough to cover both events.

P
 
Hivi Raisi Hichilema na yule.magufuli wa Tunisia Kais Said wamekwenda kumuaga mwendazake.malkia?
 
Hili la rais yuko UK, makamu yuko NY kwa maoni yangu ni muendelezo wa lile tatizo la upangaji wa vipaumbele vyetu, baada ya kumuona Rais Samia amekwenda UK, then mimi nilimpangia ratiba hii Rais Samia kuhudhuria mazishi ya malikia Elizabeth II

Shughuli ya mazishi ya Malkia inaisha leo, kesho ilikuwa atoke UK na kutimba NY kama mwenzie Ruto. Unless ilikuwa ni mipango ya muda mrefu iliishapangwa VP atamuwakilisha UNGA, ratiba ya msiba ndio ikaingilia!.

Ila tukubali, tukatae, kwenye cost cutting za trips trips JPM alikuwa mzuri!, kwa umasikini wetu, we didn't have to send two different delegations to two separate events ambazo ziko just two days apart, one delegation would have been enough to cover both events.

P

UNGA 77 "Habari za UN" kutoka makao makuu ya UN New York City.



Pata taarifa ya habari, makala, habari kwa picha , mahojiano na matukio kuhusu masuala ya kibinadamu, SDGs na mengine mengi kutoka Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa.
 
Huku wananchi wanaumia tozo.Huku viongozi wanasafiri tu.Badala ya kubana matumizi na hizo safari zao zisizokuwa na maana. Mkutano wa UN hata balozi alie kule anawakilisha .Siku hizi na Youtube wengine fuatilieni live.Mfyuuuuuuu.
 
14 September 2022

NISHATI MBADALA, AGENDA MOJAWAPO UNGA-77

Ushirikiano wa UNDP, UN ,UNCDF, na wananchi wa Ikungi Tanzania waleta mabadiliko chanya



Kuanzia wiki hii viongozi wa ulimwengu wanamiminika jijini New York Marekani kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kushiriki Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA 77.

Mambo kadhaa yatajadiliwa ikiwemo
  • Amani,
  • Haki za binadamu,
  • Uchumi na
  • Kuilinda sayari dunia dhidi ya uharibifu unaochochea majanga.
Ulimwengu tayari umebaini kuwa changamoto zimefungana na hivyo majawabu yanapaswa kutafutwa kwa kushirikiana.

Katika maeneo ambayo ushirikiano umefanyika ili kutafuta ufumbuzi wa jambo, matunda yameonekana.

Mathalani nchini Tanzania, shirika la mitaji la Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na wananchi wa wilaya ya Ikungi, mkoani Singida, wanaendelea na mradi wa kutatua changamoto ya umeme na maji, masuala mtambuka ambayo yanagusa sekta nyingine kama elimu, afya, uchumi na mazingira.

Mradi wa umeme wa nishati ya jua kupitia ufadhili wa shirika la mitaji la Umoja wa Mataifa, UNCDF umeanza kuzaa matunda kwa wananchi kama anavyosimulia Jongo Sudi wa redio washirika Ruangwa FM.
 
Huku wananchi wanaumia tozo.Huku viongozi wanasafiri tu.Badala ya kubana matumizi na hizo safari zao zisizokuwa na maana. Mkutano wa UN hata balozi alie kule anawakilisha .Siku hizi na Youtube wengine fuatilieni live.Mfyuuuuuuu.
Rafiki yangu.... wewe jali maisha yako na familia yako. Ukiumiza kichwa kufikiria ya nchi hii utatuachia watoto yatima
 
Back
Top Bottom