Makamu wa Rais hakutumia busara kujitangaza kuwa yeye ni shabiki wa Yanga

Dini hata usiposema tutajua tu,ile ni imani,imani haina usiri,
Simba na Yanga zina nguvu kuliko dini kwa hapa nchini,kisiasa ni kosa na tubaelekea pabaya,maana wanasiasa wameanza kutumia simba na yanga kutupumbaza
Astaghfirullah,
Unaweza kuta hata FaizaFoxy Malaria 2 walikuwa kwenye kigoma cha yanga jana
 
Tatizo ni wewe unayechukulia usimba na uyanga kama uadui.
Kuna watu ni Yanga lakini wazazi ni simba, vipi hao, wawe wanapigana?
Je kiongozi akisema yeye ni shabiki wa Timu fulani, maana yake anaipendelea hiyo timu?
Vipi kwa Kagame ambaye ni shabiki wa Arsenal? Maana yake mashabiki wa timu zingine za EPL wamuone Kagame kama adui?
 
Kama hauna D mbili huwezi kuelewa,hakuna Rais Tanzania aliyewahi kusema yuko timu gani,wanajua madhara yake kisiasa
 
Tatizo ni wewe unayechukulia usimba na uyanga kama uadui.
Kuna watu ni Yanga lakini wazazi ni simba, vipi hao, wawe wanapigana?
Je kiongozi akisema yeye ni shabiki wa Timu fulani, maana yake anaipendelea hiyo timu?
Vipi kwa Kagame ambaye ni shabiki wa Arsenal? Maana yake mashabiki wa timu zingine za EPL wamuone Kagame kama adui?
 
Umetanguliza ushabiki kuliko uhalisia. Hivi unategemea siku Mwiguru au Kigwangala wawe maraisi watashindwa kuonyesha timu wanayoshabikia?

Makamu wa Rais mara kadhaa amejionyesha wazi kuwa ni shabiki wa Yanga. Wakati wa kumuaga Waziri mkuu alikuwa anaaga kwa kutumia style ya Mayele.
 
Hawatadeclare trust me watacheza na maneno,huwajui wanasiasa
 
Mpango anajulikana ni Yanga hajaanza siku ya wananchi kujitambulisha
 
Wenzake sio wajinga ambao hawasemagi hadharani,ameingia kwenye siasa hana hata miaka 15,aulize wenzake
Toka akiwa waziri wa fedha alishasema yeye ni Yanga sasa kuna jipya lipi makamu yupo sawa hana unafiki
 
Fatilia akiwa waziri wa fedha alivyokuwa anataniana na waziri mkuu Yanga ikishinda halafu uje useme hivi tena
 
Kisiasa sio nzuri,ni kwa faida yake tu
Huna hoja. Hawezi kosa kura kwa kuwa ni Simba au Yanga. Nimeshuhudia kampeni za uchaguzi toka Mwinyi mpaka leo sijawahi ona watu wakitumia ushabiki wa mpira kupiga kura. Na hata ingekuwa hivyo huo ni upuuzi wa wapuuzi. Mpira ni burudani tu ni kama kunywa tusker wakati wenzio wanatumia kilimanjaro.
 
Fatilia akiwa waziri wa fedha alivyokuwa anataniana na waziri mkuu Yanga ikishinda halafu uje useme hivi tena
Humu Kuna vitoto vijinga halafu vinaona vinajua balaa. Tulia Simba, Tarimba Yanga, Kassim Majaaliwa Simba, Zitto Simba... Haya atwambie kujulikana kwao kumewaathiri vipi kisiasa.
 
Kikwete ni Yanga tangu zamani na Majaliwa ni Simba!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…