Makamu Waziri Mkuu - kuwa upande wa WAKULIMA anza na haya:

Makamu Waziri Mkuu - kuwa upande wa WAKULIMA anza na haya:

Kabende Msakila

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2020
Posts
1,809
Reaction score
1,692
SALAAM!
# Wakulima wa tumbaku wa hapa Biharamulo (Kalenge) kutolipwa fedha za mauzo ya tumbaku musimu huu - ni takriban 100,000USD wanaidai KAMPUNI iitwayo Mkwawa Leave Tobacco Ltd;

# Rushwa - usafiri na usafirishaji hususan magari yafanyayo safari za Nyakanazi - Kakonko ambapo kila dereva wa gari ndogo (Probox) hutoa gate pass kila siku 30,000/=;

# Madaraja ya tumbaku ya wizi na unyonyaji kwa Wakulima. Fikiria mche wa tumbaku huwa na vishada visivyozidi 30 lkn grades za tumbaku zipo 64.

# Wafanyabiashara wa mafuta - hawa wkt mwingine huhifadhi mafuta ili yaadimike kisha wauze kwa bei ghali. Lkn pia upande wa Serikali kutoza kodi kubwa inachochea w/biashara hao kupigana ya chini kwa chini sambamba na migomo.

# Matumizi kengeufu ya political vote au self help scheme. Hizi fedha za miradi ya kujitegemea kwa Wakuu wa Wilaya, Wakuu wa Mikoa na Wabunge nyingi hutumika visivyo - 90% huelekezwa ktk huduma za kijamii huku uzito mdogo ukiwekwa ktk huduma za kiuchumi. Hatuwezi achana na umasikini.
 
Back
Top Bottom