Makanisa na vinanda/miziki kama kawaida yao

Makanisa na vinanda/miziki kama kawaida yao

Kuna kanisa mtaa mmoja huku nilipo, Sijajua hawa ni walokole ama! Mtaa mzima hapa ni kelele kwenda mbele. Miziki inapigwa kama wako disco mazee! Aise wanakera mno na makelele yao, serikali naomba muwashugulikie hawa watu, tembeeni mikoa yote mpaka vijijini.
Hah hah haha....
Huzijui bar zenye kupiga makelele, magari ya matangazo, misikiti, kumbi za sherehe , kumbi za madisco nk.
Nchi yetu haina sheria ya kudhibiti mijikelele
 
Haya madisco kwenye kumbi za starehe na bar zinakera kwelikweli. Watu miaka nenda miaka rudi hakuna anayelalamika , watu wameridhika. Lakini linalohusu Mungu malalamiko ni mengi!!
Nashangaa
 
Hili ni janga la taifa kwakweli,,,

Mwanzoni wakati sijapata hadha ya jambo hili nilikuwa naona watu wanaolalamika kuhusu kelele za makanisa ya kilokole kama ni watu wenye chuki za kidini. Mimi ni mkristo tena mpentecoste, fpct,

Lakini tangu mwezi wa tatu mwaka huu na Mimi nimeanza kuonja adha na madhila ya kuishi karibu na makanisa ya kilokole yenye makelele kupita kiasi.

Nimejenga karibu na kanisa la EAGT (Evangelist Assembles of God Tanzania) , mwanzoni wakati wa mchungaji wa zamani marehemu, walikuwa wanaabudu kwa ustaarabu bila makelele mengi au adha kwa majirani, hata wakipiga makelele basi ni jumapili tu au siku ya ijumaa ambapo ufanya mkesha basi.

Lakini tangu mchungaji huyo afariki dunia, kulitokea mabadiriko ya utawala na kugombania uongozi, waumini wengi walilihama kanisa hilo nawamekuja waumini wapya, sasa tangu hapo hatulali, kila siku ni kelele kubwa kupita kiasi mpaka huwezi kupumzika nyumbani kwako tena nikila Siku 24/7.

Mbaya zaidi wameanzisha utaratibu wa kuanza kufanya ibada usiku wa manane kuanzia saa kumi usiku (alfajiri) mpaka saa kumi na mbili na nusu asubuhi wakiita ibada ya "Morning glory" tena kwa makelele makubwa sana kiasi cha kufanya watu tunashindwa kulala usiku ukizingatia tuna watoto wadogo , wazee na wagonjwa! Tumeshawafuata na kuwaomba wafanye ibada zao kwa sauti ya wastani lakini wapi, ndio kwanza wanafungulia maspeakers mpaka mwisho!

Kiukweli hili jambo linaumiza sana akili na afya.mpaka wengine tulio na nyumba za kupangisha tunakimbiwa na wapangaji kwasababu ya kukwepa kelele za ibada!! yaani nyumba yako lakini unatamani kuhama kukwepa kelele!! Hata ningekuwa na uwezo wa kuibeba nyumba yangu nikaiweke eneo lingine ningefanya hivyo kukwepa makelele kupita kiasi!! Unaamka umechoka, una usingizi na kichwa kinauma kwa kelele za hao jamaa waliokesha usiku mzima!!

Kwanini haya madhehebu yanayotumia utaratibu huu wa ibada yasifungulie sauti ya wastani ili kutowabughudhi wakazi wanaozunguka kanisa husika?! Au watumie sound proof kupunguza kelele, hatukatazi wala hatuwezi kuzuia watu wasiabudu kwa imani yao lakini wasiwe kero kwa jamii inayozunguza nyumba zao za ibada, mbona wakatoliki, walutheri, waanglican na waorthodox hawasumbui watu kwa makelele kupita kiasi wanafanya ibada zao kistaarabu tu?! Kwani bila makelele kupita kiasi Mungu hasikii ibada yao?! Ajabu zaidi waumini wanakuwa humo ndani ni wanne tu! Lakini makelele ya maspeakers utadhani kuna mkutano wa adhara na watu laki mbili.

Jamanii eeh Uhuru wako unapoishia ndipo uhuru wa wenzako unapoanzia, tuheshimu faragha ya kupumzika kwa wenzetu, au tuwe kama Rwanda ambapo kagame alizuia kelele za aina hii?! Au wajenge mbali na makazi ya watu ili wapige kelele zao masaa 24/7 bila kuwasumbua watu hasa usiku wakati watu wamepumzika!
 
Hah hah haha....
Huzijui bar zenye kupiga makelele, magari ya matangazo, misikiti, kumbi za sherehe , kumbi za madisco nk.
Nchi yetu haina sheria ya kudhibiti mijikelele

Kwahiyo buji, makanisa na wao wameiga sio! Niliwahi kusikia baadhi ama wengiwao vijana wanajifunzia bongo fleva makanisani, wakitoka pale washakomaa.
 
Kuna kanisa mtaa mmoja huku nilipo, Sijajua hawa ni walokole ama! Mtaa mzima hapa ni kelele kwenda mbele. Miziki inapigwa kama wako disco mazee! Aise wanakera mno na makelele yao, serikali naomba muwashugulikie hawa watu, tembeeni mikoa yote mpaka vijijini.
Naomba kuuliza hivi haya mafundisho aliyafundisha Yesu ? Yaani vinanda,kuimba na yale yote yanayo patikana katika miziko hiyo iitwayo "Miziki ya Injili".
 
Naomba kuuliza hivi haya mafundisho aliyafundisha Yesu ? Yaani vinanda,kuimba na yale yote yanayo patikana katika miziko hiyo iitwayo "Miziki ya Injili".

Yesu hajafundisha haya maujinga.
 
Wanaserebuka kwa Bwana Yesu, sema kila kitu lazima kiwe na limit, nadhani serikali pia inapaswa kuwawekea mipaka hawa watu maana wakati mwingine ni dico 24/7 mpaka huwa najiuliza hao waumini huwa wanaenda makazini saa ngapi
Kazini kufanya nn Sasa na wanahudumu kwa bwana?!
 
Kuna kanisa mtaa mmoja huku nilipo, Sijajua hawa ni walokole ama! Mtaa mzima hapa ni kelele kwenda mbele. Miziki inapigwa kama wako disco mazee! Aise wanakera mno na makelele yao, serikali naomba muwashugulikie hawa watu, tembeeni mikoa yote mpaka vijijini.
Naamini kanisa linatakiwa lifanye mambo ambayo yanavuta watu kwa Yesu, siyo yanayokera watu.
Nashukuru kanisa langu mambo yanapangwa vizuri hadi una enjoy kusikiliza.
Wanaopiga kelele ni kwa sababu hwafuati biblia.
Soma kafungu kote hapo chini ujifunze zaidi

Mt 6:5-15 SUV​

Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi. Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi. Basi msifanane na hao; maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba. Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni. Utupe leo riziki yetu. Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu. Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.] Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
 
Hili ni janga la taifa kwakweli,,,

Mwanzoni wakati sijapata hadha ya jambo hili nilikuwa naona watu wanaolalamika kuhusu kelele za makanisa ya kilokole kama ni watu wenye chuki za kidini. Mimi ni mkristo tena mpentecoste, fpct,

Lakini tangu mwezi wa tatu mwaka huu na Mimi nimeanza kuonja adha na madhila ya kuishi karibu na makanisa ya kilokole yenye makelele kupita kiasi.

Nimejenga karibu na kanisa la EAGT (Evangelist Assembles of God Tanzania) , mwanzoni wakati wa mchungaji wa zamani marehemu, walikuwa wanaabudu kwa ustaarabu bila makelele mengi au adha kwa majirani, hata wakipiga makelele basi ni jumapili tu au siku ya ijumaa ambapo ufanya mkesha basi.

Lakini tangu mchungaji huyo afariki dunia, kulitokea mabadiriko ya utawala na kugombania uongozi, waumini wengi walilihama kanisa hilo nawamekuja waumini wapya, sasa tangu hapo hatulali, kila siku ni kelele kubwa kupita kiasi mpaka huwezi kupumzika nyumbani kwako tena nikila Siku 24/7.

Mbaya zaidi wameanzisha utaratibu wa kuanza kufanya ibada usiku wa manane kuanzia saa kumi usiku (alfajiri) mpaka saa kumi na mbili na nusu asubuhi wakiita ibada ya "Morning glory" tena kwa makelele makubwa sana kiasi cha kufanya watu tunashindwa kulala usiku ukizingatia tuna watoto wadogo , wazee na wagonjwa! Tumeshawafuata na kuwaomba wafanye ibada zao kwa sauti ya wastani lakini wapi, ndio kwanza wanafungulia maspeakers mpaka mwisho!

Kiukweli hili jambo linaumiza sana akili na afya.mpaka wengine tulio na nyumba za kupangisha tunakimbiwa na wapangaji kwasababu ya kukwepa kelele za ibada!! yaani nyumba yako lakini unatamani kuhama kukwepa kelele!! Hata ningekuwa na uwezo wa kuibeba nyumba yangu nikaiweke eneo lingine ningefanya hivyo kukwepa makelele kupita kiasi!! Unaamka umechoka, una usingizi na kichwa kinauma kwa kelele za hao jamaa waliokesha usiku mzima!!

Kwanini haya madhehebu yanayotumia utaratibu huu wa ibada yasifungulie sauti ya wastani ili kutowabughudhi wakazi wanaozunguka kanisa husika?! Au watumie sound proof kupunguza kelele, hatukatazi wala hatuwezi kuzuia watu wasiabudu kwa imani yao lakini wasiwe kero kwa jamii inayozunguza nyumba zao za ibada, mbona wakatoliki, walutheri, waanglican na waorthodox hawasumbui watu kwa makelele kupita kiasi wanafanya ibada zao kistaarabu tu?! Kwani bila makelele kupita kiasi Mungu hasikii ibada yao?! Ajabu zaidi waumini wanakuwa humo ndani ni wanne tu! Lakini makelele ya maspeakers utadhani kuna mkutano wa adhara na watu laki mbili.

Jamanii eeh Uhuru wako unapoishia ndipo uhuru wa wenzako unapoanzia, tuheshimu faragha ya kupumzika kwa wenzetu, au tuwe kama Rwanda ambapo kagame alizuia kelele za aina hii?! Au wajenge mbali na makazi ya watu ili wapige kelele zao masaa 24/7 bila kuwasumbua watu hasa usiku wakati watu wamepumzika!
Kwangu wapo hao walokole na mikesha yao huku wakiliankwankutumia microphone....kuomba kwa kunena, na siku ya J2 usiombe....saa 12 asubuhi unaamshwa na mziki wao wa kelele.....mbaya zaidi wamejenga kwa mjumbe wetu wa nyumba kumi....kila tukilalamika hakuna kitu....nilichofanya nami ni kununua speaker zangu mbili na amplifier ya ukweli.....wakianza tu nami nalianzisha mara nne yao.....inabidi wazime kabosa.....sasa tunalala na kwa amani....tunaheshimiana.....

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Hiz Azana pia nazo znatusumbua asubuh
 
Back
Top Bottom