Makapuku Forum

Walah unachovuta acha dogo🙆
 
Good Morning kwa wapambanaji wote na wazalendo wote Obe Lee Mtu Chake Carasco Putin makaveli10 mshamba_hachekwi

Good morning kwa warembo wote mnaomiliki iphone na majumba yenu hapa dasalama Makiwendo Shunie tunawapenda sana maboss lady wetu.

Good morning kwa makapuku msio na hela mnaotumia itel na alcatel kuswampia humu ndani, mnaoishi kwenye nyumba ya kupanga na unadaiwa kodi Atoto amkaaaaaa kumekuchaaaaaaa unalala una raha gani? 😂
 
Aloooh [emoji1787]
 
Daaah imebidi nicheke kwanza [emoji1787] sina nyumba sina iphone ebu
 
Spika wa Bunge la Marekani, Kevin McCarthy jana Jumanne Septemba 12, 2023 alitangaza kuwa analiagiza Bunge hilo kufungua hati ya uchunguzi wa kumuondoa madarakani Rais Joe Biden kutokana na shughuli za kibiashara za familia yake kuhusishwa na rushwa.

Endapo agizo hilo litafanikiwa itakuwa ni histotia kwa nchi hiyo ikiwa ni miezi michache imesalia kuelekea Uchaguzi Mkuu wan chi hiyo wa mwaka 2024.

McCarthy amesema: "Uchunguzi wa Bunge hadi sasa unatoa picha ya utamaduni wa ufisadi katika familia ya Rais Biden"
Wakati hayo yakiendelea pia wanachama wa chama pinzani cha Rais Biden, Republican wanafuatilia kwa karibu biashara na shughuli za mtoto wa Rais, Hunter Biden.

"Haya ni madai ya matumizi mabaya ya madaraka, kizuizi na rushwa, na yanastahili uchunguzi zaidi wa Bunge," amesema McCarthy huku akitangaza kuwa analielekeza Bunge likiongozwa na Kamati ya Uangalizi kufungua uchunguzi rasmi wa mashtaka hayo.

Wakati hayo yanaendelea taarifa kutoka Ikulu ya Marekani kupitia msemaji wake, Ian Sams ilijibu mashambulizi hayo kwa kuyaita ni ya kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu.

"Hizo ni siasa mbaya kuelekea Uchaguzi Mkuu. Wanachama wa Republican waliopo bungeni wamekuwa wakimchunguza Rais kwa miezi tisa, na hawajapata ushahidi wowote wa kufanya makosa," alisema msemaji Ian Sams.
 
Rais Samia Suluhu Hassan ameteuliwa kuwa Mjumbe wa Bodi ya Ushauri ya Kituo cha Dunia cha Uhimilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi (GCA).

Hatua hiyo inamfanya Rais Samia kuwa mkuu wa nchi wa pili ndani ya bodi hiyo inayojumuisha wajumbe watano, akiwemo Rais wa Senegal, Macky Shall.

Mbali na marais hao, wajumbe wengine katika bodi hiyo ni Moussa Mahmat ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Akinumwi Adesina na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Kristalina Georgieva.

Hata hivyo, nafasi hiyo inamfanya Rais Samia kuwa na nguvu ya kupeleka hoja moja kwa moja kuzishinikiza nchi zilizoendelea zitekeleze ahadi ya kutoa fedha za uhilimivu wa athari za mabadiliko ya tabianchi kwa nchi zinazoendelea kama inavyoelezwa na wadau.

Taarifa ya uteuzi huo, imetolewa na Mwenyekiti wa bodi hiyo, Ban Ki-Moon walipokutana na Rais Samia katika mikutano wa wakuu wa nchi kuhusu mabadiliko ya tabianchi, uliofanyika Nairobi nchini Kenya.

Akizungumza na Mwananchi Digital leo Septemba 12, 2023 Meneja wa Mipango wa Shirika la linalojishughulisha na athari za mabadiliko ya tabianchi (ForumCC), Msololo Onditi amesema uteuzi huo ni tija kwa Tanzania.

Tija hiyo inatokana na kile alichoeleza, mkuu huyo wa nchi atakuwa na nguvu ya kuwasilisha moja kwa moja hoja za kuzishinikiza nchi zilizoendelea kutoa fedha za kuhimili athari za mabadiliko ya tabianchi.

“Kwa nafasi hiyo atakuwa na sauti ya kupaza kwa nchi zilizoendelea kutoa fedha za uhimili wa athari za mabadiliko ya tabianchi kwa nchi zinazoendelea kama zilivyoahidi,” amesema.

Lakini wadhifa huo, Onditi amesema unaifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zitakazokuwa na fursa ya kupata taarifa ya fedha za mabadiliko ya tabianchi haraka na kujiandaa kuzipokea.

 
Jeshi la Polisi wilayani Kiteto, mkoani Manyara, linawashililia watu saba kwa tuhuma za mauaji ya mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la John Joseph (45), na kujeruhi watu wengine nane wakukima na wakazi wa Kijiji cha Ndirigishi.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Septemba 11, 2023 katika Kijiji cha Ndirigishi, baada ya watu hao kuwashambulia kwa fimbo na hivyo kudaiwa kusababisha kifo cha mtu mmoja na wengine nane wakilazwa hospitali ya Kiteto.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa, ACP George Katabazi, amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Leyo Koseimi (28), Emmanuel Ndega (28), Mingoko Paredi na (60), wakazi wa Ndirigishi.

Wengine ni Nyoroi Sendu (27), mkazi wa Ndirigishi, Mrulo Miaka (50) mkazi wa Ndirigishi, Paulo Mgema (30) na Silali Madumba (70) mkazi wa Mbande Ndirigishi.

"Marehemu na wenzake walishambuliwa kwa fimbo sehemu mbalimbali za miili yao na watuhumiwa hao wakiwa shambani," amesema ACP George Katabazi.

Amesema kiini cha tukio hilo ni tabia za watu kujichukulia sheria mkononi kwa baadhi ya jamii ya kifugaji maasai ambapo marehemu na wenzake walikuwa wanaandaa shamba eneo la hifadhi ya Emboley Murtangos.

"Mbinu walizotumia ni kuvamia wakulima hao kwenye vibanda, mahema waliyojenga shambani na kisha kuwashambulia jambo linalodaiwa kushababisha kifo cha mkulima huyo huku wengine nane wakilazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kiteto.

Kamanda Katabazi amewataka watu kuacha kujichukulia sheria mkononi akisema watafikishwa mahakamani muda na wakati wote na kuongeza mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali hiyo ya wilaya, na mara baada ya taratibu kukamilika utakabidhiwa ndugu zake kwa maziko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…