Makapuku Forum

Mama mzazi wa marehemu Esther, Rachel Izengo amesema jina la mtoto wake ni Esther Ramadhani Isugilo na siyo Samira Mathias ambalo lilizoeleka mtaani.

Esther amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumatatu Septemba 18, 2023 kwa madai ya kuchinjwa na mpenzi wake aliyefahamika kwa jina moja la Amos.

Mapema leo asubuhi mmliki wa nyumba aliyokuwa amepanga Esther ambako kulifanyika mauaji hayo, Yohana Nhembelo alisema ndugu wameomba chumba kilichofanyika kisifanyiwe usafi hadi watakapofika na kukiangalia.

Amesema amepata taarifa ya kifo cha mtoto wake kupitia kwa majirani saa 10.00 usiku wa kuamkia leo akiwa mkoani Shinyanga ambako ndiko anakoishi.

Amesema alianza safari muda huo na kufika jijini Dodoma saa 8:00 leo ili kujua sababu ya kifo cha binti yake ambaye ni mtoto wa kwanza kati ya watoto watatu alionao.

“Nimesikitishwa sana na kifo cha mwanangu cha kuchinjwa kwa sababu ni kifungua mimba na sikutarajia kama atakufa kwa kifo kama hiki. Binti yangu alikuwa ni mtu wa watu,”amesema huku akiangua kilio baada ya kushuhudia chumba kichofanyika mauaji hayo.

Ndugu wa marehemu wamesema baada ya kuangalia hali ya mwili wa mtoto wao ndipo watafanya uamuzi wazike wapi.

Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Martin Otieno amesema kuwa chanzo cha mauaji ya wapenzi hao waliokutwa wamefariki dunia usiku wa kuamkia ni wivu wa mapenzi.

Kamanda huyo amesema mwanaume aliyejulikana kwa jina moja la Amos alimchoma kisu maeneo ya shingoni Esther maeneo ya shingoni kama mara tatu na kupelekea koromeo kutoka nje na akawa amemchoma kwenye mkono begani kisha yeye kujichoma kisu kwenye kitovu na kupelekea utumbo wote kutoka nje.
 
Watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni wapenzi wamekutwa wamekufa huku mwanamke akiwa amechinjwa na mwanaume ambaye hajafahamika jina akiwa na jeraha kubwa tumboni lililosababisha utumbo kutoka nje.

Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia leo Jumatatu Septemba 18, 2023 katika Mtaa wa Oysterbay, Kata ya Dodoma Makulu kwenye chumba ambacho mwanamke aliyeuawa Samira Mathias alikuwa amepanga.

Akizungumza na Mwananchi katika eneo la tukio mwenye nyumba hiyo, Donald Nhembelo amesema alisikia kelele za kuomba msaada kutoka kwenye chumba cha mpangaji wake (Samira) saa 7.00 usiku.

Amesema baada ya kufika kwenye chumba hicho alisikia sauti ya mwanaume akiomba msaada ndipo alipouliza Samira yuko wapi na kujibiwa kuwa hawezi kuongea na yeye hawezi kusimama.

“Aliniomba nivunje mlango ili nimsaidie. Nilivunja ubao uliopo juu ya mlango (Venti) na kuingiza mkono kwa ndani na kufungua mlango na nilipowasha taa ndipo nilikuta Samira yuko juu ya kitanda amenyamaza,”amesema.

Amesema damu zilikuwa zimetapakaa kitandani na sakafuni huku mwanaume aliomba msaada ambaye hamfahamu akiwa amelala chini huku utumbo wake ukiwa nje.

Amesema baada ya kuona hali hiyo, aliripoti polisi ambao walifika kwenye eneo hilo ambao baadaye waliondoka na miili ya watu hao.

Balozi wa mtaa wa Oysterbay, Isaya Mabigiri amesema amepata taarifa za uwepo wa tukio kutoka kwa mwenye nyumba hiyo na alipokwenda alikuta miili ya watu.

 

X wangu
 
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imelikataa pingamizi la mbunge wa zamani wa viti maalum (CCM), Vicky Kamata la kupinga mtoto wa ‘mumewe’, asiteuliwe kuwa msimamizi mirathi na mali za marehemu, Dk Servacius Likwelile zenye thamani ya zaidi ya Sh4 bilioni.

Machi 19, 2016, Vicky Kamata aliyekuwa mbunge kwa vipindi viwili vya Bunge la 9 na Bunge la 10, alifunga ndoa na aliyekuwa katibu mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dk Servacius Likwelile ambaye, alifariki dunia Februari 19, 2021.

Katika hukumu ya shauri la kuomba kuwa msimamizi wa mirathi ya Dk Likwelile iliyofunguliwa na mwanae, Raymond, iliyotolewa Septemba 15, 2023, na Jaji Augustine Rwizile, amesema Vicky hakuwa mke aliyeolewa kihalali na marehemu.

Kwa hiyo Mahakama imeamuru mali ambazo Vicky alikuwa akipinga kuingizwa katika orodha ya mali za marehemu akidai ziliingizwa kimakosa, zijumuishwe katika orodha ya mali za marehemu.

Mali hizo ni nyumba iliyopo kiwanja namba 116 iliyopo Mbweni, Kinondoni jijini Dar es Salaam ambayo alisema walichuma pamoja na nyumba mbili zilizopo huko Mpiji Magoe jijini humo kwenye eneo lenye ukubwa wa hekari 9.5 ambayo alidai ana hisa asilimia 50.

Mbali na hizo, ipo nyumba viwanja namba 387 na 389 iliyopo kitalu D Sinza iliyopo kwa jina lake, nyumba iliyopo Kibamba kwa jina la mtoto wake Gloria Likwelile na viwanja namba 318,319,320 na 321 vilivyopo Mpigi Magoe Ubungo.

Viwanja hivyo vinamilikiwa na kampuni ya Beda Group Limited na Beda Farms Limited ambavyo Vicky alidai kuwa na asilimia 50 ya hisa na pia alipinga gari aina ya Toyota Prado namba T731 CQR na pikipiki Toyota namba MC 588 AHT.

Katika hukumu hiyo iliyopatikana katika mtandao wa mahakama jana Jumanne, September 19, 2023, mtoto wa marehemu aitwaye Raymond Likwilile ameteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi na atatakiwa kabla ya kupewa barua, atimize takwa la kanuni namba 66 la mirathi.

Jaji Rwizile alisema tangu kufariki kwa Dk Likwelile familia yake haijawahi kuwa na utulivu ambapo kuliibuka vita ya kisheria kati ya watoto wa marehemu na Vicky aliyekuwa akionekana mke halali wa ndoa wa marehemu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…