Makapuku Forum

Mpira wa miguu kilele chake huwa ni ushindi [kupata alama tatu au kwenye mashindano ni kufuzu hatua inayofuata], kwenye Ligi tumechukua alama tatu dhidi ya Mtibwa Sugar, Dodoma Jiji na Coastal Union.

Kwa hiyo ukija kwenye malengo, bado tupo kwenye malengo ambayo ni kushinda mechi kadiri tuwezavyo. Watu wanataka timu ifunge magoli mengi, msimu uliopita tulifunga magoli mengi na hatukuwa mabingwa.

Huyu ambaye anasema tunashinda lakini hatuna furaha, itakuaje kama tutaendelea kushinda na kuwa mabingwa, atakuja kusema hana furaha ya ubingwa? Acha tuendelee kuishi kwenye malengo makuu ambayo ni kushinda kila mechi.

- Ahmed Ally, Meneja Habari na Mawasiliano Simba.
 
David de Gea anaweza kustaafu soka ikiwa hatapokea ofa ya kurejea uwanjani pindi dirisha la mwezi Januari litakapofungwa, hii ni baada ya miezi kupita akiwa hana timu tangu alipoondoka Manchester United mwishoni mwa mwezi Juni.

Ripoti ya #Goal inasema Mchezaji mwenzake wa zamani wa Man Utd, Cristiano Ronaldo amekuwa akijaribu kumshawishi ajiunge na Al Nassr, lakini kipa huyo bado ana msimamo wa kutaka kuendelea kucheza Ligi ya Mabingwa na yuko tayari kusubiri hadi dirisha la uhamisho la Januari litakapofunguliwa.

NB: Hadi sasa De Gea hana timu licha ya awali Bayern Munchen na Madrid kuonesha nia lakini hakuna ofa rasmi iliyotumwa.

cc [90 Min & Goal]
 
Hofu kubwa ilitanda kwa mashabiki waliokuwa uwanjani na hata wale waliokuwa wakifatilia kupitia runinga baada ya Henock Inonga kuumia, wengi walikuwa wakifikiri amevunjika.

Lakini kwa bahati nzuri Inonga hakuvunjika, amepata kidonda kilichotokana na msuguano uliojitokeza. Baada ya kukimbizwa hospitali alishonwa nyuzi 13 na usiku uleule aliruhusiwa kutoka hospitali kurudi nyumbani.

Kwa hiyo ataendelea kusafisha kidonda β€˜dressing’. Je, atarejea lini uwanjani? Kuna uwezekano mkubwa akaukosa mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Power Dynamos lakini baada ya hapo ananasi kubwa ya kuwa sehemu ya kikosi dhidi ya TZ Prisons [Ligi Kuu] na Al Ahly [African Football League].

- Amhed Ally, Meneja Habari na Mawasiliano Simba.
 
Baada ya Jean Baleke kupasia kamba mara tatu β€˜hat-trick’ dhidi ya Coastal Union, amefikisha magoli matano [5] na kuongoza kwenye orodha ya wafungaji wa Ligi Kuu ya NBC 2023|24.

Baleke amempita Feitoto ambaye alikuwa anaongoza akiwa na magoli matatu ambayo aliyafunga kwenye mzunguko wa kwanza wa Ligi Azam FC ilipocheza dhidi ya Tabora United mchezo ambao haukuchezwa kwa dakika zote 90 baada ya kumalizwa kwa sababu za kikanuni.

MAGOLI MATANO YA JEAN BALEKE
[emoji460]️[emoji460]️[emoji460]️ vs Coastal Union
[emoji460]️ vs Dodoma Jiji FC
[emoji460]️ vs Mtibwa Sugar

Ikiwa Ligi ya NBC imechezwa kwa mizunguko mitatu, tayari wachezaji wawili wameshaondoka na mipira ya Bodi ya Ligi [Feitoto na Baleke] baada ya kila mmoja kufunga hat-trick!
 
Farhan Jr

Kuna watu wanatuaminisha MOHAMED HUSSEIN amechoka lakini mpaka sasa ana assists MBILI za Ligi Kuu na anaongoza sambamba na wachezaji wengine wenye assists mbili, anaendelea alipoishia msimu uliopita.

Wengine wanatuamunisha SHOMARI KAPOMBE amedrop wakati mpaka sasa ana mechi nyingi bora pamoja na assist MOJA sawa na nyota wengi ambao sio Mabeki, anaendelea alipoishia.

Wengine wanasema ROBERTINHO miyeyusho lakini ni Kocha ambaye hajapoteza mchezo wowote wa Ligi Kuu tangu aje na ana NGAO tayari.

Huu ubaya wa ghafla sana umetokea wapi??

Is this a script??
 
Farhan Jr

Kocha kapewa malengo gani? Kubeba ubingwa Ligi Kuu, kubeba FA CUP na nusu fainali Klabu bingwa! Tayari ana NGAO! Mtihani uliopo kwake ni Utamaduni wa Mashabiki wa Simba na timu yao, wengi wapo tayari hata wafungwe ila wacheze mpira mzuri, lakini dunia imebadilika Ligi Kuu ina Makocha wazuri na kila timu inafanya homework yake.

ATLETICO MADRID ndio kipimo cha mpira matokeo, ndipo sehemu aliposimamia Robertinho! Inapotokea open game atacheza mpira ila inapotokea timu zinapishana atasaka matokeo yake na kucheza kwa hesabu, that's football.

Mashabiki wanataka nini? Wanataka alama tatu ama mpira mzuri? Jibu ni kuwa Mpira mzuri na matokeo mazuri, lakini sio rahisi kwenye mpira na dunia ya kisasa ya football, kuna wakati hupati hiyo chance.
 
Farhan Jr

Lomalisa kachezewa rafu mbaya sana sana, leo tena Henock Inonga kachezewa rafu mbaya sana sana, football ni mchezo hatari sana! Nampongeza sana Refa Aragija leo katoa umeme kama ambavyo hata yule wa jana alipaswa kutoa umeme, wachezaji lazima walindane.

Rafu mbaya sana kwa Henock, mbaya sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…