Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 154,929
- 459,607
Takwimu mpya za Benki Kuu ya Tanzania (BoT) zinaonyesa ongezeko la asilimia 5 katika wastani wa kipato cha Mtanzania kwa mwaka ikichangiwa na kukua kwa uchumi wa kanda ya Dar es Salaam, kanda ya ziwa na kanda ya kaskazini.
Katika ripoti ya BoT ya ufanisi wa uchumi katika kila kanda iliyotolewa Oktoba 5 mwaka huu inaonyesha kuwa wastani wa kipato cha Mtanzania (GDP per Capita) mmoja mmoja kimeongezeka kutoa wastani wa Sh2.70 milioni hadi Sh2.84 milioni.
Wastani wa kipato cha wakazi wa Dar es Salaam kimeongezeka zaidi kuliko maeneo mengine ya nchi kutoka Sh4.81 milioni hadi Sh5.39 milioni mwaka 2022 sawa na ukuaji wa asilimia 12, hivyo ilikinganishwa na mwaka uliopita kila mkazi wa Dar es Salaam aliongeza Sh500, 000 katika mapato yake ya mwaka.
Katika ripoti ya BoT ya ufanisi wa uchumi katika kila kanda iliyotolewa Oktoba 5 mwaka huu inaonyesha kuwa wastani wa kipato cha Mtanzania (GDP per Capita) mmoja mmoja kimeongezeka kutoa wastani wa Sh2.70 milioni hadi Sh2.84 milioni.
Wastani wa kipato cha wakazi wa Dar es Salaam kimeongezeka zaidi kuliko maeneo mengine ya nchi kutoka Sh4.81 milioni hadi Sh5.39 milioni mwaka 2022 sawa na ukuaji wa asilimia 12, hivyo ilikinganishwa na mwaka uliopita kila mkazi wa Dar es Salaam aliongeza Sh500, 000 katika mapato yake ya mwaka.