Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 154,929
- 459,607
Mahakama ya Wilaya ya Mufindi imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela, Sostenes Vakuka baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kubaka.
Vakuka (32), mkazi wa kijiji cha Ihowanza, Kata ya Malangali ametiwa hatiani kwa kumbaka mwanamke mwenye miaka 20, ambaye ni mke wa mtu.
Hukumu hiyo imetolewa jana Desemba 6, 2023 na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Mufindi, Edward Uphoro.
Katika kesi hiyo, ilidaiwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Februari 25, 2023 saa moja usiku katika Kijiji cha Ihowanza akiwa nyumbani kwa mwanamke huyo ambapo alimuingilia kinguvu bila ridhaa yake, huku akimuuliza ni nani amemruhusu kuishi katika nyumba hiyo.
Siku ya tukio inaelezwa mume wa mwanamke huyo alikuwa amekwenda dukani kununua mahitaji.
Vakuka (32), mkazi wa kijiji cha Ihowanza, Kata ya Malangali ametiwa hatiani kwa kumbaka mwanamke mwenye miaka 20, ambaye ni mke wa mtu.
Hukumu hiyo imetolewa jana Desemba 6, 2023 na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Mufindi, Edward Uphoro.
Katika kesi hiyo, ilidaiwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Februari 25, 2023 saa moja usiku katika Kijiji cha Ihowanza akiwa nyumbani kwa mwanamke huyo ambapo alimuingilia kinguvu bila ridhaa yake, huku akimuuliza ni nani amemruhusu kuishi katika nyumba hiyo.
Siku ya tukio inaelezwa mume wa mwanamke huyo alikuwa amekwenda dukani kununua mahitaji.