Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 154,929
- 459,607
[emoji187] Najua kwamba Simba na Yanga wanaombeana mabaya. Sijui ilianzia lini lakini kwa umri wangu chuki kubwa zaidi iliendelezwa katika lile pambano la fainali za CAF mwaka 1993. Simba dhidi ya Stella Abidjan. Mgeni rasmi alikuwa Mzee Rukhsa. Mwenyezi Mungu amrehemu. Kabla ya mechi nchi nzima ilikuwa imesisitiziwa kwamba tunapaswa kuwa wazalendo kwa sababu Simba walikuwa wanakaribia kutuletea kombe la kwanza kubwa nchini.
.
Mfumo wa tiketi ulikuwa huu huu kwahiyo hakukuwa na namna ya kuweza kuwazuia YANGA kuingia uwanjani. Ujumbe tu kutoka kwa Rais na watu wazito ni kwamba Yanga walipaswa Kuishangilia Simba. Walipokuja uwanjani hawakuishangilia Simba wala Stella lakini Boli Zozo alipoifungia Stella bao la pili na kufanya matokeo kuwa 2-0 ndipo Yanga walipolipuka na kuimba kwa furaha wakisema “uzalendo umetushinda”.[emoji23]
.
Kuanzia hapo kila kitu kimekuwa wazi. Hakuna unafiki tena. Na umekuwa mwendo wa visasi kiasi kwamba katika dunia hii ya utandawazi watu wamekuwa wakivaa hadi jezi za timu pinzani. Si zinauzwa nchini na watu wanalipa kodi kuziingiza? Hakuna tunachoweza kuzuia kwa sasa. Afadhali tungezuia huko mwanzoni kwa kukemea mambo kadhaa. Na sasa nadhani imekuwa kama chachu tu kwa timu zetu kufanya vizuri.
.
Ukiwafunga Mamelodi unawafunga mdomo Mamelodi na Simba. Ukiwafunga Al Ahly unawaziba midomo Al Ahly na Yanga. Ni kazi ngumu lakini lazima wachezaji wetu waifanye. Hakuna namna kwa sababu hakuna tunachoweza kubadili kama Dk. Ndumbaro alivyosema na baadaye kutolewa taarifa rasmi kwamba “alitania tu.” Acha mashabiki waende uwanjani kushangilia wapinzani. Kitakachowanyamazisha ni ubora tu wa timu ya nyumbani.
.
Unadhani Yanga walifurahi kuona Simba wanakwenda robo fainali mara nne mfululizo? Ubora wa Simba ya Jose Luis Miquissone yule na wahuni wenzake uliwalazimisha. Baadaye wenyewe walichoka kwenda kushangilia wapinzani wa Simba. Ni hadithi ya Yanga kufika fainali za Shirikisho. Watu walioumia zaidi duniani ni Simba lakini hawakuwa na la kufanya. Ubora wa Yanga na kina akina Aziz Ki uliwalazimisha. Huu ndio ukweli halisi. Ukweli ambao lazima usemwe.
— Edo Kumwembe [via Jicho la Mwewe]
.
Mfumo wa tiketi ulikuwa huu huu kwahiyo hakukuwa na namna ya kuweza kuwazuia YANGA kuingia uwanjani. Ujumbe tu kutoka kwa Rais na watu wazito ni kwamba Yanga walipaswa Kuishangilia Simba. Walipokuja uwanjani hawakuishangilia Simba wala Stella lakini Boli Zozo alipoifungia Stella bao la pili na kufanya matokeo kuwa 2-0 ndipo Yanga walipolipuka na kuimba kwa furaha wakisema “uzalendo umetushinda”.[emoji23]
.
Kuanzia hapo kila kitu kimekuwa wazi. Hakuna unafiki tena. Na umekuwa mwendo wa visasi kiasi kwamba katika dunia hii ya utandawazi watu wamekuwa wakivaa hadi jezi za timu pinzani. Si zinauzwa nchini na watu wanalipa kodi kuziingiza? Hakuna tunachoweza kuzuia kwa sasa. Afadhali tungezuia huko mwanzoni kwa kukemea mambo kadhaa. Na sasa nadhani imekuwa kama chachu tu kwa timu zetu kufanya vizuri.
.
Ukiwafunga Mamelodi unawafunga mdomo Mamelodi na Simba. Ukiwafunga Al Ahly unawaziba midomo Al Ahly na Yanga. Ni kazi ngumu lakini lazima wachezaji wetu waifanye. Hakuna namna kwa sababu hakuna tunachoweza kubadili kama Dk. Ndumbaro alivyosema na baadaye kutolewa taarifa rasmi kwamba “alitania tu.” Acha mashabiki waende uwanjani kushangilia wapinzani. Kitakachowanyamazisha ni ubora tu wa timu ya nyumbani.
.
Unadhani Yanga walifurahi kuona Simba wanakwenda robo fainali mara nne mfululizo? Ubora wa Simba ya Jose Luis Miquissone yule na wahuni wenzake uliwalazimisha. Baadaye wenyewe walichoka kwenda kushangilia wapinzani wa Simba. Ni hadithi ya Yanga kufika fainali za Shirikisho. Watu walioumia zaidi duniani ni Simba lakini hawakuwa na la kufanya. Ubora wa Yanga na kina akina Aziz Ki uliwalazimisha. Huu ndio ukweli halisi. Ukweli ambao lazima usemwe.
— Edo Kumwembe [via Jicho la Mwewe]