Makapuku Forum

Makapuku Forum

[emoji599] Brazil imemwondoa winga Antony kwenye kikosi baada ya staa huyo wa Manchester United kudaiwa kumpiga aliyekuwa mpenzi wake na sasa anachunguzwa.
.
Kwenye kikosi hicho cha Brazil [emoji1054] nafasi yake imechukuliwa na straika wa Arsenal, Gabriel Jesus kwa ajili ya mechi mbili za kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia.
.
Na hilo limekuja baada ya polisi wa Sao Paulo huko Brazil kutoa ripoti hiyo miezi mitatu iliyopita. Mpenzi wake wa zamani Antony, mrembo Gabriela Cavallin aliripoti polisi tukio la kupigwa, kutishiwa maisha pamoja na kuumizwa mwilini. Na sasa mrembo huyo ameweka bayana meseji za mchezaji huyo zilizokuwa za vitisho.
.
Antony amekana kutenda kosa hilo na kusisitiza atapambana kusafisha jina lake. Lakini, hilo halimwingia akilini kocha wa timu ya taifa ya Brazil, Fernando Diniz, aliyeamua kumwondoa kwenye kikosi na kumuita Jesus.
Screenshot_20230906_072530_Instagram.jpg
 
HAWAUJUI UTAMU
.
00—Kati ya timu zote 32 zilizofuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu, Lens ndio timu pekee ambayo haina mchezaji hata mmoja aliyewahi kucheza katika mashindano hayo. Mastaa wote katika kikosi hicho ama wamecheza Ligue 1 pekee, au mashindano mengine ya klabu Ulaya lakini sio UEFA Champions League.
Screenshot_20230906_072626_Instagram.jpg
 
[emoji187] Wasiwasi wangu umemalizwa na jambo linaloitwa wakati. Wakati umetuonyesha kwamba Banda hakuwa mchezaji wa ajabu kama ilivyozungumzwa. Banda ni aina ya wachezaji ambao waliurudisha nyuma kidogo ubora wa Simba. Yeye pamoja na mwenzake Pape Sakho hawakuweza kuziba pengo la mchezaji kama Luis Miquissone pale alipoondoka.

Waliletwa kwa ajili ya kuziba pengo la Mmakonde lakini mpaka Mmakonde anarudi hakuna mchezaji aliyeweza kuziba pengo lake kirahisi. Muda mfupi alioutumia uwanjani alionekana kujijali zaidi mwenyewe kuliko timu. Ni hadithi ile ile ya mchezaji kama Larry Bwalya. Wakati Clatous Chama alipoondoka hakuweza kuibeba Simba mabegani kwake mpaka Chama akarudi na kuendeleza utawala wake.

Ndicho ambacho kimetokea kwa kina Banda na Miquissone. Baada ya kuitazama vizuri Simba hii nimegundua kwamba kama Miquissone akiendelea kujifua na kupambana na UBONGE alio nao huku akiwa fiti zaidi, basi kuna uwezekano mkubwa Simba ikarudi tena kwake pamoja na kwa rafiki yake Chama.”

- Edo Kumwembe.
Screenshot_20230906_072720_Instagram.jpg
 
[emoji187] ANAITWA Peter Banda alipewa ‘Thank you’ yake ndani ya klabu ya Simba. Inanikumbusha namna alivyoingia nchini kwa mbwembwe akipewa jina la ‘Wonder Kid’. Kwamba ni kijana mdogo mwenye maajabu.
.
Ilinishangaza kuona kijana mdogo wa umri wake anaruhusiwa kutoka Ulaya kuja kucheza Afrika halafu katika nchi ya dunia ya tatu inayoitwa Tanzania. Inatokea nadra kwa vijana wa umri wake kurudi kama wana ubora uwanjani.
.
Unaweza kukubali kwa mchezaji kama Saido Ntibanzokiza. Kwa mujibu wa Wikipedia inaonyesha kwamba Saido ana miaka 36. Hata kama alidanganya miaka yake lakini haishangazi kuona amerudi tena nyumbani Afrika kumalizia soka lake. Lakini inashangaza kwa mchezaji mwenye umri wa miaka 22 kama Banda kuja kucheza Tanzania akitokea Ulaya. Hii ilikuwa dalili tosha kwamba hakuwa na ubora huo kama ulivyozungumzwa wakati wa ujio wake.

- Edo Kumwembe.
Screenshot_20230906_072826_Instagram.jpg
 
[emoji599] SIMBA 3 AL AHLY 3
.
[emoji983] Apr 09, 2021
[emoji1093] Al Ahly 1-0 Simba [emoji1241]
.
[emoji983] Feb 23, 2021
[emoji1241] Simba 1-0 Al Ahly [emoji1093]
.
[emoji983] Feb 12, 2019
[emoji1241] Simba 1-0 Al Ahly [emoji1093]
.
[emoji983] Feb 02, 2019
[emoji1093] Al Ahly 5-0 Simba [emoji1241]
.
[emoji983] Ago 29, 1985
[emoji1093] Al Ahly 2-0 Simba [emoji1241]
.
[emoji983] Ago 22, 1985
[emoji1241] Simba 2-1 Al Ahly [emoji1093]
Screenshot_20230906_072924_Instagram.jpg
 
Hatua ya mamlaka ya uteuzi kutengua nafasi ya mteule muda mchache baada ya kumteua au kumbadilishia wadhifa, imetajwa na baadhi ya wachambuzi kuwa ni kiashiria cha kuwapo kwa changamoto katika mifumo ya uteuzi.

Msingi wa hoja ya wachambuzi hao ni tukio la Agosti 30, mwaka huu, baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kumteua Profesa Kennedy Gaston kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kuapishwa Septemba Mosi.

Lakini siku tatu baadaye, Septemba 3, ikiwa ni saa 48 tangu alipokuwa ameapishwa, akateuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Hii si mara ya kwanza; ilitokea pia kwa Mbunge wa Misungwi, Alexander Mnyeti aliyeteuliwa Agosti 30 kuwa Naibu Waziri wa Kilimo, lakini kabla ya kuapishwa alihamishiwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi.
Screenshot_20230906_073112_Instagram.jpg
 
Vikosi vya Jeshi la Russia vimeanza mbinu za kufunika ndege zake za mashambulizi kwa matairi ya gari, jambo ambalo wataalamu wanasema linaweza kuwa ni jaribio la muda la kuzilinda dhidi ya mashambulizi ya ndege zisizo na rubani za Ukraine.

Picha ya setilaiti kutoka kambi ya jeshi ya nchi hilo, inaonyesha ndege mbili za mashambulizi ya kimkakati (Tu-95) zikiwa na matairi ya gari kwa upande wa juu.

Japokuwa bado haijatambulika kwa mara moja sababu ya uhakika ya kufanya hivyo lakini kituo cha runinga cha CNN kimefanya mahojiana na mtaalamu wa vita ya anga ambaye amesema huenda ni mbinu moja wapo wa kupunguza makali ya ndege hizo zisizo na rubani za Ukraine.

"Inaweza kupunguza kuonekana kwa juu lakini bado zitaonekana chini ya kamera za maalumu ya infrared," aliiambia CNN.

Screenshot_20230906_073214_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Inapendeza kuona namna flani timu hii inapambana kujitegemea, kwa mara ya kwanza ilifanyika SIMBA DAY msimu huu bila fedha kutoka mifuko ya watu bali Wadhamini wa klabu na vyanzo vingine vya mapato, inapendeza kuona hatua kwa hatua timu inaanza kuondoka kwenye minyororo ya utegemezi kwa 100% ni hatua nzuri kuelekea nchi ya ahadi.

Mashabiki wa Simba ongezeni kasi ya kudownload App ya SIMBA APP, ongezeni kusubscribe Youtube mkatengeneze numbers, hii ina maana kubwa kwa maslahi ya klabu! Changamoto ni Maudhui kuwa madogo, ubunifu na vifaa, nadhani CEO twist kidogo wekeza tu kwakuwa Vijana walioaminiwa wapo vizuri changamoto ni vifaa.

YANGA wameanza kutengeneza namba kupitia Youtube, ni wake up call! Mashabiki tupunguze stori nyingi, tufanye jezi bei, tufanye tiketi bei! Basi hata BUKU MBILI ya APP? Au MB kadhaa za Youtube ya SIMBA? Tupunguze stori stori na siasa nyingi, dunia ni digital! Shida kubwa ya Mashabiki wa Simba tukiambizana ukweli utasikia UNATUMIKA, UNATUGOMBANISHA.

Leo hii namba zinatuhukumu haswa Youtube, lets get it done! Tupunguze stori! Tuingizie pesa klabu, kama una smart download App na nenda Youtube, na kitengo cha Kaka @ahmedally_ zidisheni maudhui zaidi, tuwe na ukubwa kila eneo kuliko kuvimbia huku na namba tunapigwa baadhi ya maeneo, LETS MAKE IT POSSIBLE.

Target yetu, revenue za Youtube, renevue za APP, huku Instagram na Twitter hakuna hela zaidi ni informations tu! Sina shaka na uwezo wa HOMEBOY @thobias17sebastian sina shaka na uwezo wa @babchicharito2407 Au Shemeji @rabbihume issue ni INVESTMENT HATUNA[emoji109]

Screenshot_20230906_073858_Instagram.jpg
 
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imetangaza kupanda kwa bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli hapa nchini zitakazotumika kuanzia Jumatano September 06, 2023 saa 6:01 usiku ambapo kwa mwezi September 2023, bei za rejareja za mafuta katika Mkoa wa Dar es Salaam petrol ni Tsh. 3213 kwa lita, dizeli Tsh. 3259 na mafuta ya taa 2943.

EWURA imesema mabadiliko ya bei za mafuta kwa mwezi September 2023 yaliyoonesha kupanda kwa bei yanatokana na kupanda kwa gharama za mafuta katika soko la dunia kwa hadi 21%, gharama za uagizaji wa mafuta hadi 62% ikilinganishwa na mwezi August 2023 na maamuzi ya kisiasa katika nchi zinazozalisha mafuta kwa wingi (OPEC+).

Itakumbukwa bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli hapa nchini kwa mwezi uliopita zilizoanza kutumika kuanzia Jumatano August 02, 2023 saa 6:01, bei za rejareja za mafuta katika Mkoa wa Dar es Salaam petrol ilikuwa ni Tsh. 3199 kwa lita, dizeli Tsh. 2935 na mafuta ya taa 2668.
View attachment 2740482
Wenye ist ndo wakatii wetu huu
 
Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana, ameziagiza kamati za siasa za CCM, kuwafuatilia na kuwachukulia hatua Wanachama walioanza kupitapita kusaka ubunge na udiwani akisema wanaofanya hivyo wanakiuka kanuni, utaratibu na miongozo ya uchaguzi ndani ya CCM.

Kinana ameyasema hayo September 05, 2023, Wilayani Hai, Kilimanjaro katika Mkutano Mkuu wa Jimbo la Hai, uliohusu utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025, Jimboni ambapo
amesema watakaobainika wanajipitisha kusaka ubunge na udiwani hawatapitishwa na vikao vya maamuzi kugombea nafasi hizo hata kama wataongoza katika kura za maoni

“Nataka nitumie fursa hii kuziagiza kamati za siasa za CCM nchi nzima, zikisaidiwa na kamati za maadili nchi nzima, kuwafuatilia wale ambao wameanza kuzungukazunguka kutafuta ubunge, udiwani, uenyekiti wa mtaa au kitongoji kuanzia sasa”

“Hatuna nafasi ya kuhangaishwa na Watu wanaotafuta uongozi kipindi hiki, wasubiri hadi mwezi wa saba mwaka 2025, Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) itaamua tarehe ya kwenda kuchukua fomu, kabla ya hapo unavunja kanuni"

"Aliyeanza kampeni mapema, alitoa rushwa, alikivuruga Chama, hata upate kura za Wajumbe wote hutapita, je ulitoa rushwa, ulizingatia kanuni, uliwachafua Viongozi wenzako walioko madarakani? Kwa hiyo unaweza ukawa wa kwanza lakini ukawa wa mwisho”
Screenshot_20230906_195546_Instagram.jpg
 
Ili kulinda ukuaji uchumi na kuepuka athari za kupanda kwa gharama za maisha, Tanzania imejadiliana na Benki ya Dunia juu ya namna itakavyosaidiwa kukabiliana na athari za upungufu wa Dola ya Marekani katika mzunguko wa fedha.

Majadiliano hayo yanakuja, katikati ya wimbi la kupungua kwa sarafu hiyo duniani kunakotajwa kuchagiza ongezeko la bei ya baadhi ya bidhaa muhimu yakiwemo mafuta.

Tayari uhaba wa sarafu hiyo, umeacha makovu katika bei ya mafuta kulingana na taarifa ya jana ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura).

Taarifa hiyo, imeeleza katika Jiji la Dar es Salaam bei ya Petroli imepanda kwa Sh14 huku dizeli ikipanda kwa Sh324.

Pamoja na majadiliano ya kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na benki hiyo, msaada wa kukabiliana na kupanda kwa sarafu hiyo ni jambo lingine lililojadiliwa.

Majadiliano hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam leo, Septemba 6, 2023 ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Fedha, Dk Mwigumu Nchemba, huku Benki ya Dunia ikiwakilishwa na Mkurugenzi wake anayesimamia kanda ya mashariki na Kusini mwa Afrika, Hassan Zaman.

Katika majadiliano hayo ameiomba benki hiyo, kuharakisha upatikanaji wa zaidi ya dola za Marekani 500 milioni ifikapo Novemba mwaka huu.

Ameeleza fedha hizo zitaisaidia nchi kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa sarafu hiyo katika mzunguko wa fedha nchini hali inayochangia mfumuko wa bei na kukwamisha uagizaji wa bidhaa muhimu kutoka nje ya nchi yakiwemo mafuta.

Pia, alitumia fursa hiyo, kuishukuru Benki ya Dunia kwa kuidhinisha upatikanaji wa fedha kwenye miradi nane yenye thamani ya zaidi ya Dola za Marekani 2.16 bilioni.

Akizungumza katika majadiliano hayo, Zaman amepongeza hatua za Serikali za kukuza uchumi licha ya uwepo wa janga la Uviko-19.

Screenshot_20230906_200008_Instagram.jpg
 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amekutana na kuzungumza na Waziri wa Viwanda na Tekinolojia ya Juu wa Serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Sultan Ahmed Al Jaber jijini Nairobi, Kenya.

Waziri Makamba amekutana na Al Jaber pembezoni mwa mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi unaofanyika Nairobi, Kenya.

Pamoja na mambo mengine, Waziri Makamba ameihakikishia UAE kuwa Tanzania itashiriki Mkutano wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi (COP 28) Disemba 2023, ambapo miongoni mwa masuala itakayoyatilia mkazo ni ufadhili wa miradi ya nishati safi ya kupikia kwa akina mama vijijini.


Aidha, Waziri Makamba amesisitiza Tanzania itaungana na nchi za Afrika na nchi nyingine zinazoendelea duniani, kuhimiza Nchi Wanachama, hususani zilizoendelea kutekeleza ahadi za kupunguza hewa ukaa, kuchangia fedha kwa ajili ya uhimilivu na kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi na upatikanaji wa teknolojia kwa ajili ya jitihada hizo.

Kwa upande wake, Sultan Ahmed Al Jaber, aliishukuru Tanzania kwa kuahidi kushiriki mkutano wa COP 28 na kwamba Umoja wa Falme za Kiarabu umejipanga kuhakikisha mkutano huo unaleta matokeo chanya katika jitihada za kukabiliana na athari za mabadiliko ya Tabianchi Duniani.

Al Jaber aliahidi kuunga mkono masuala ya kipaumbele ya Tanzania katika mkutano huo kwa kuzingatia uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na UAE.

Screenshot_20230906_200124_Instagram.jpg
 
Inafahamika kuwa katika ulimwengu wa sasa mawasiliano yamekuwa kitu kirahisi sana ikiwa ni pamoja na kumtumia mtu picha, ujumbe, wimbo, video, nyaraka na vitu vingine kwa njia rahisi.

Hayo yote yamewezeshwa na ulimwengu wa teknolojia ambayo ndani yake kuna vitu kama vile kumuhamishia mtu kwa njia ya mtandao bila kutumia ‘waya’, upande huohuo teknolojia hizo zimekuwa zikitajwa majina yake na watumiaji bila kufahamu nini hasa chimbuko la majina hayo.

Kama ulikuwa unatumia Bluetooth bila kufahamu kuhusiana na asili ya neno hilo lilipotokea wapi, basi fahamu kuwa ni jina la mtu ambaye alikuwa mfalme Denmark na Norway.
Screenshot_20230906_200252_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom