Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 577
- 2,595
Wakuu.
Awali ya yote nitoe pongezi kwa kila Raia wa nchi hii aliye bahatika kuhesabiwa. Wengine hatukupata bahati ya kufikiwa siku ya jana, natumani kwa muda muafaka, tutapata pia fursa hii ya kuingia kwenye rekodi ya takwimu muhimu za wakazi wa nchi hii.
Baada ya kutoa pongezi hili naomba sasa nielezee wasiwasi wangu.
Nimepitia maswali yote yanayoulizwa lakini nimepata wasiwasi sana. Inakuwaje zoezi la kuhesabu watu lihusishe uchukuaji wa taarifa zungine nyeti zinazohusu maisha ya mtu binafsi?
Nauliza hivi kutokana na nature ya nchi yetu. Tumepitia kwenye kadhia nyingi sana hapo nyuma hasa tunapotoa taarifa zetu nyeti kwa watu tunao waamini. Makarani hawa ni watu kama sisi, tunaishi nao mtaani. Usalama wa taarifa zetu upoje? Wakizitumia kwa mambo ya uhalifu tutawawajibisha vipi wakati nchi haina sheria inayolinda faragha na taarifa binafsi za watu?
Achilia mbali kuzitumia kwa mambo ya kihalifu, vipi kama wataamua kuziuza kwa mtu yoyote au hata kuzitumia kwa mambo ambayo serikali haikupanga?
Kwanini Serikali imeamua kufanya sensa pasipo kutunga kwanza sheria hii? Ikitokea taarifa zangu zimetumika vibaya nitamuwajibisha nani? Nitalindwa vipi?
Nipo tayari kuhesabaiwa lakini nina wasiwasi mkubwa wa nini kitaanza kutokea baada ya kukamilika kwa zoezi hili.
Awali ya yote nitoe pongezi kwa kila Raia wa nchi hii aliye bahatika kuhesabiwa. Wengine hatukupata bahati ya kufikiwa siku ya jana, natumani kwa muda muafaka, tutapata pia fursa hii ya kuingia kwenye rekodi ya takwimu muhimu za wakazi wa nchi hii.
Baada ya kutoa pongezi hili naomba sasa nielezee wasiwasi wangu.
Nimepitia maswali yote yanayoulizwa lakini nimepata wasiwasi sana. Inakuwaje zoezi la kuhesabu watu lihusishe uchukuaji wa taarifa zungine nyeti zinazohusu maisha ya mtu binafsi?
Nauliza hivi kutokana na nature ya nchi yetu. Tumepitia kwenye kadhia nyingi sana hapo nyuma hasa tunapotoa taarifa zetu nyeti kwa watu tunao waamini. Makarani hawa ni watu kama sisi, tunaishi nao mtaani. Usalama wa taarifa zetu upoje? Wakizitumia kwa mambo ya uhalifu tutawawajibisha vipi wakati nchi haina sheria inayolinda faragha na taarifa binafsi za watu?
Achilia mbali kuzitumia kwa mambo ya kihalifu, vipi kama wataamua kuziuza kwa mtu yoyote au hata kuzitumia kwa mambo ambayo serikali haikupanga?
Kwanini Serikali imeamua kufanya sensa pasipo kutunga kwanza sheria hii? Ikitokea taarifa zangu zimetumika vibaya nitamuwajibisha nani? Nitalindwa vipi?
Nipo tayari kuhesabaiwa lakini nina wasiwasi mkubwa wa nini kitaanza kutokea baada ya kukamilika kwa zoezi hili.