Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
MAKATO YA MIAMALA YAPO POA! YANALANDANA NA UCHUMI WETU WA KATI
Kwa Mkono wa, Robert Heriel
Nimefurahishwa na mambo yaendavyo, mwaka Jana tulipigiwa mbiu kuwa tumeingia uchumi wa Kati. Watu walifurahia hasa wenye mrengo wa kuishabikia CCM na Wanachama wa CCM pamoja na Watanzania WA kipato cha chini na wenye elimu duni.
Wengi walishangilia na kumsifia Hayatti Magufuli aliyekuwa Rais wakati huo, ambaye naye kujigamba hakukuisha mdomoni mwake kujitukuza namna alivyoupaisha uchumi kufikia uchumi wa Kati.
Mimi nilishajua hatari ya kukuambia taifa lipo uchumi wa Kati ilhali wananchi wake wapo uchumi wa mwisho kabisa huko chini.
Katika uchunguzi wangu WA kimkakati, Vijana wengi nilipowauliza kuhusu uchumi wao, nilibaki kuwaonea huruma. Wengi ni dhoofu, choka mbaya, Apeche Alolo, kuingiza 5000 Kwa siku ni kitendawili. Lakini wenyewe wanakuambia wapo uchumi wa Kati.
Sasa nikasema nisibishane nao, maana wengi wape, Ila nikasema hawa nawasubiri kwenye tuta(Bump) kwani lazima wapunguze mwendo, na Kama watakaidi basi chamoto watakiona.
Sasa tumeshalifikia tuta, waliositi za mwisho kwenye Gari chamoto wanakiona, mrusho wake wakwenda,
Na Jambo la uhakika ni kuwa barabara tunayopitia kuna Matuta mengi(bumps) za kutosha.
Waliokaa siti za mbele mpaka siti za Kati wao hawawezi ona athari za mwendo huu, Ila Wale Watanzania waliositi za nyuma chamoto watakipata.
Tupo uchumi wa Kati, makato ya kwenda,
SERIKALI ongezeni kasi, ongezeni makato kila Nyanja yanayoendana na Uchumi wa Kati.
Tunajiweza, tunamudu, tunafurukuta.
Uchumi wa Kati, makato ya Kati.
Hongera serikali,
Hongera wananchi, nimeamini tupo uchumi wa Kati.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Dumila, Morogoro
Kwa Mkono wa, Robert Heriel
Nimefurahishwa na mambo yaendavyo, mwaka Jana tulipigiwa mbiu kuwa tumeingia uchumi wa Kati. Watu walifurahia hasa wenye mrengo wa kuishabikia CCM na Wanachama wa CCM pamoja na Watanzania WA kipato cha chini na wenye elimu duni.
Wengi walishangilia na kumsifia Hayatti Magufuli aliyekuwa Rais wakati huo, ambaye naye kujigamba hakukuisha mdomoni mwake kujitukuza namna alivyoupaisha uchumi kufikia uchumi wa Kati.
Mimi nilishajua hatari ya kukuambia taifa lipo uchumi wa Kati ilhali wananchi wake wapo uchumi wa mwisho kabisa huko chini.
Katika uchunguzi wangu WA kimkakati, Vijana wengi nilipowauliza kuhusu uchumi wao, nilibaki kuwaonea huruma. Wengi ni dhoofu, choka mbaya, Apeche Alolo, kuingiza 5000 Kwa siku ni kitendawili. Lakini wenyewe wanakuambia wapo uchumi wa Kati.
Sasa nikasema nisibishane nao, maana wengi wape, Ila nikasema hawa nawasubiri kwenye tuta(Bump) kwani lazima wapunguze mwendo, na Kama watakaidi basi chamoto watakiona.
Sasa tumeshalifikia tuta, waliositi za mwisho kwenye Gari chamoto wanakiona, mrusho wake wakwenda,
Na Jambo la uhakika ni kuwa barabara tunayopitia kuna Matuta mengi(bumps) za kutosha.
Waliokaa siti za mbele mpaka siti za Kati wao hawawezi ona athari za mwendo huu, Ila Wale Watanzania waliositi za nyuma chamoto watakipata.
Tupo uchumi wa Kati, makato ya kwenda,
SERIKALI ongezeni kasi, ongezeni makato kila Nyanja yanayoendana na Uchumi wa Kati.
Tunajiweza, tunamudu, tunafurukuta.
Uchumi wa Kati, makato ya Kati.
Hongera serikali,
Hongera wananchi, nimeamini tupo uchumi wa Kati.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Dumila, Morogoro