Makonda alivyonusurika kumwagiwa maji na watangazaji wa Clouds

Ilikuwa ni kwenye birthday yake 15/02 jana


RC Makonda kwingine nakuunga mkono ila nakuomba tafuta ' Mshauri ' kwani kiukweli kwa jinsi Tanzania tulivyochelewa Kimaendeleo halafu na Wewe Mheshimiwa Rais alivyokuamini na kukuteua kwa hiyo nafasi ningekuwa ni Wewe sidhani kama hata huo muda wa kusheherekea Birthday kwa ' Mbwembwe ' kama hizi ningekuwa nazo. Sometimes huwa unaniangusha mno Comrade halafu hata kwa Umri wako na ' Utoto ' uufanyao haviendani kabisa. Nahisi hata Mheshimiwa Rais kwa kiasi fulani atakuwa amesikitika japo anaweza asikuambie.

Mkoa unaouongoza wa Dar es Salaam una ' changamoto ' nyingi na zinahohitaji ufumbuzi wa haraka sana. Ningekuwa Mimi ndiyo Wewe ningeitumia hiyo siku kwanza kwa kwenda Kusali kisha nafanya mazungumzo ya Kiufumbuzi na Walimu au Sekta zingine zenye matatizo ili nipate ufumbuzi wake.

Nasisitiza tena bila uwoga kuwa Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Paul Makonda unaniangusha sana na unasababisha sasa hata Mamlaka ya Ukuu wa Mkoa kuanza kudharaulika na sidhani kama ni jambo jema na lenye afya Kiutawala na Kiuongozi. Punguza SIFA na ULIMBUKENI leo ni Mkuu tu wa Mkoa una ' mashauzi ' hivi hivi ukiteuliwa kuwa Mbunge au Balozi au Waziri tutakunywa maji kweli?

Nimesikitika sana na huwa sipendi UNAFIKI na nimekusema wazi wazi ili ubadilike. Umeshaniharibia ' mood ' yangu.

Mwisho nakuomba sana anza sasa kuvipenda Vyombo vyote vya Habari na acha ' Kuvibagua ' vingine kwani kuna siku utavihitaji hivyo unavyovidharau na ' vitakutosa ' kwa kukuharibia mipango yako yote ya Kiutendaji unless uniambie kuwa labda kuna faida fulani unaipata kwa Wewe kuwa Kipenzi cha Clouds Media Group na ndiyo maana unawang'ang'ania au yawezekana pia hao Clouds Media Group labda wanajua SIRI zako na ' madhaifu ' yako hivyo unawaogopa na ndiyo maana unalazimika kuwanyenyekea.

Upendo wako wa Clouds Media Group umeshawajengea chuki kwa Wanahabari wenzao na kumbuka Watu wa Media wanategemeana hasa Kiutendaji je unadhani hiki Kiburi ulichowajengea Clouds Media Group siku ukitoka ' Madarakani ' watapa ushirikiano kwa wenzao ( media zingine? )

Badilika upesi Kaka hujachelewa!
 
Hayo maji aliyomwagiwa mbona hajalowa au kaloweshwa wapi hapo mi sijaona.
 

Umeongea points tupu hapo, itafika kipindi vijana watakuwa hawaaminiki tutarudi kulekule kijana ni taifa la kesho.
 
Sijaona amwagiwe maji mwilini hapo au makomenti ya aliowaorodhesha kwenye list ya 'wambia' na 'wauza' haya teh teh teeeeh
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mbona masuala ya kumwagiana maji ni ya kike na mara chache kwa wanaume wa Dar es Salaam.
ukweli Ngosha umeni disappointment kabisa.
Alafu birthday huwa ni kwa wanawake na watoto bhana.
hilo undi lingine watafanyia wapi mkuu hahahahah
 
Magufuli muangalie huyu bwana makondo aisee...
Utakuja ushtukie when it's too late..

Mtafute angalau anaejielewa au hata luteni mstaafu sio unawapeleka vijijini huko,makonda anafaa kuwa mkuu wa mkoa wa katavi huko au mkuu wa wilaya ili apata uzoefu fulani hivi...

Maybe mnayo ajenda moja aisee.
 
makonda anaipenda clouds kinafiki sababu ya magufuli
 
Aisee raha sana....upendo na furaha very beautiful indeed
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…