Makonda anasema hatomsaliti Hayati Magufuli hata kwa bastola, ilihali tayari kashamsaliti kama ifuatavyo

Makonda anasema hatomsaliti Hayati Magufuli hata kwa bastola, ilihali tayari kashamsaliti kama ifuatavyo

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Katibu mwenezi akiwa ziarani mkoani geita kasema hivi!

Yeye siyo mnafiki kama CCM wengine waliomsaliti Magufuli na kumkana, Yeye Paul Makonda kasema Magufuli ndiye kiongozi wake ambaye hatoweza kumsaliti hata kama atawekewa bastola kichwani"

HAYO MANENO KAYATAMKA Mbele ya umati, pia kaenda kutamka kwa mama Magufuli!

Ukweli ni kwamba Makonda tayari kashamsaliti Magufuli hadi muda huu kama ifuatavyo!

Katika dini anayoiabudu Yeye Makonda ya kikristu; Ukisoma kitabu cha Mathayo 26:33-35 na 69-70 kuhusu ufuasi wa mtu!

Andiko linasema hivi!
33 Petro akasema, “Hata kama wote watakuacha, mimi sitaku acha.”

34 Yesu akamjibu, “Ninakuambia kweli, usiku huu huu, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” 35 Lakini Petro akasema, “Hata kama itabidi nife pamoja na wewe, sitakukana.” Na wana funzi wote wakasema hivyo hivyo.

Hapo tuondoe Petro tuweke Paul Makonda akiwa kama mwanafunzi mteule wa Magufuli kati ya wale wanafunzi 12, akiwemo Makonda, Chalamila , Ally Happi na kina Yuda wengine wa sampuli yake!..

Kabla ya kuteswa kwa Yesu waliahidi kwamba HAWATAMSALITI HATA KWA BASTOLA! Lakini baadaye mateso yalipokuja waligeuka!

...andiko linaendelea linasema hivi;

69 Wakati huo Petro alikuwa amekaa uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia akamwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.” 70 Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui usemalo.”

Magufuli alisema ni kichaa peke yake anaweza kubali mkataba wa hovyo kama ule wa bandari kupewa mwarabu au muwekezaji sehemu nyeti ya nchi kwa miaka yote hiyo ....wanafunzi wateule wake akiwemo makonda na wengine wakashangilia!

CCM ikiwa ndiyo serikali, na Paul makonda akiwa ndiye katibu Mwenezi na mwanafunzi wa Magufuli!
Mkataba wa bandali unapitishwa na Paul makonda anazunguka kuinadi CCM!
Na hataki waandishi wamhoji kuhusu maoni yake kwenye ule mkataba (SIMJUI MTU HUYO MAGUFULI KUHUSU MKATABA)

Makonda anasema HATAMSALITI Magufuli hata kwa bastola lakini anazunguka nchi nzima kwenda KUITETEA ILANI ya chama kilichogawa bandari! (Simjui mtu yule)
 
Magu alisemea bandari ipi?
 
Tundu na Mbowe wakapambanie watoto wao ambao ni raia wa Marekani
 
Navokumbuka jpm aliongelea bandari ya bagamoyo?
"Simjui mtu huyu". Kwahiyo Magufuli akataze bandari ndogo ya bagamoyo kupewa mwarabu, halafu angeitoa bandari kuu ya DSM,

Yaani akataze kidogo halafu aje agawe kikubwa!?
 
"Simjui mtu huyu". Kwahiyo Magufuli akataze bandari ndogo ya bagamoyo kupewa mwarabu, halafu angeitoa bandari kuu ya DSM,

Yaani akataze kidogo halafu aje agawe kikubwa!?
Kwani masharti ni yaleyale kuna uthibitisho gani masharti ni yale yale?
 
Kwani masharti ni yaleyale kuna uthibitisho gani masharti ni yale yale?
Mikataba iliyopitishwa bungeni na bunge likaridhia inathibitisha hilo, IGA na mengineyo
 
Mikataba iliyopitishwa bungeni na bunge likaridhia inathibitisha hilo, IGA na mengineyo
So jpm aliongelea hiyo theory ya miaka 100 kule kwenye bandari ya bagamoyo kwa muda wote huo tra haitakiwi kwenda kuchota mapato pale , wewe umeiona wapi mapaka sasa hiyo theory kwenye huu mkataba wa bandari hii ya dar es salaam.?


Na kwanza tuwekane sawa sio kwamba nasapoti hili kataba lililopo la hii bandari ya dar

Nachojaribu kusema huyu jpm mwenyewe alikua chenga tu
 
So jpm aliongelea hiyo theory ya miaka 100 kule kwenye bandari ya bagamoyo kwa muda wote huo tra haitakiwi kwenda kuchota mapato pale , wewe umeiona wapi mapaka sasa hiyo theory kwenye huu mkataba wa bandari hii ya dar es salaam.?


Na kwanza tuwekane sawa sio kwamba nasapoti hili kataba lililopo la hii bandari ya dar

Nachojaribu kusema huyu jpm mwenyewe alikua chenga tu
Chenga Leo wakati CCM mlipigia makofi kuunga hoja ya kutogawa bandari
 
Katibu mwenezi akiwa ziarani mkoani geita kasema hivi!

Yeye siyo mnafiki kama CCM wengine waliomsaliti Magufuli na kumkana, Yeye Paul Makonda kasema Magufuli ndiye kiongozi wake ambaye hatoweza kumsaliti hata kama atawekewa bastola kichwani"

HAYO MANENO KAYATAMKA Mbele ya umati, pia kaenda kutamka kwa mama Magufuli!

Ukweli ni kwamba Makonda tayari kashamsaliti Magufuli hadi muda huu kama ifuatavyo!

Katika dini anayoiabudu Yeye Makonda ya kikristu; Ukisoma kitabu cha Mathayo 26:33-35 na 69-70 kuhusu ufuasi wa mtu!

Andiko linasema hivi!
33 Petro akasema, “Hata kama wote watakuacha, mimi sitaku acha.”

34 Yesu akamjibu, “Ninakuambia kweli, usiku huu huu, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” 35 Lakini Petro akasema, “Hata kama itabidi nife pamoja na wewe, sitakukana.” Na wana funzi wote wakasema hivyo hivyo.

Hapo tuondoe Petro tuweke Paul Makonda akiwa kama mwanafunzi mteule wa Magufuli kati ya wale wanafunzi 12, akiwemo Makonda, Chalamila , Ally Happi na kina Yuda wengine wa sampuli yake!..

Kabla ya kuteswa kwa Yesu waliahidi kwamba HAWATAMSALITI HATA KWA BASTOLA! Lakini baadaye mateso yalipokuja waligeuka!

...andiko linaendelea linasema hivi;

69 Wakati huo Petro alikuwa amekaa uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia akamwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.” 70 Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui usemalo.”

Magufuli alisema ni kichaa peke yake anaweza kubali mkataba wa hovyo kama ule wa bandari kupewa mwarabu au muwekezaji sehemu nyeti ya nchi kwa miaka yote hiyo ....wanafunzi wateule wake akiwemo makonda na wengine wakashangilia!

CCM ikiwa ndiyo serikali, na Paul makonda akiwa ndiye katibu Mwenezi na mwanafunzi wa Magufuli!
Mkataba wa bandali unapitishwa na Paul makonda anazunguka kuinadi CCM!
Na hataki waandishi wamhoji kuhusu maoni yake kwenye ule mkataba (SIMJUI MTU HUYO MAGUFULI KUHUSU MKATABA)

Makonda anasema HATAMSALITI Magufuli hata kwa bastola lakini anazunguka nchi nzima kwenda KUITETEA ILANI ya chama kilichogawa bandari! (Simjui mtu yule)
Kuna mtu alimtambulisha makonda kwa jiwe na kumsisitiza kuwa huyo ni wa kuaminika na wa nyumban


Huyo mtu ndie aliyemtoa makonda umoja wa vijana na kumuwezesha kupata ukuu wa wilaya baadae ukuu wa mkoa wakat makonda akiwa hana umaarufu wowote


Na hata huu ujio wa sasa wa makonda kuna watu wameuratibu haujatokea hivihivi tu


Ktk siasa kila mtu anamasta wake hata jiwe alikua na masta wake
 
Chenga Leo wakati CCM mlipigia makofi kuunga hoja ya kutogawa bandari
CHa kwanza mimi si mwanaccm

Chapili kataba linapitishwa bungeni chini ya bunge la miujiza ya jpm ya uchaguzi wa 2020, kama kataba hili la bandari litatugharimu kama nchi dhambi hii mtu wa kwanza kwenye listi ni jpm hawa wengine watafata baada yake
 
CHa kwanza mimi si mwanaccm

Chapili kataba linapitishwa bungeni chini ya bunge la miujiza ya jpm ya uchaguzi wa 2020, kama kataba hili la bandari litatugharimu kama nchi dhambi hii mtu wa kwanza kwenye listi ni jpm hawa wengine watafata baada yake
Kosa la jpm ni nini wakati alisema waziwazi kwamba ni kichaa peke yake atakuja kukubali kugawa bandari
 
Kosa la jpm ni nini wakati alisema waziwazi kwamba ni kichaa peke yake atakuja kukubali kugawa bandari
KAtaba limefika bungeni wabunge wa ccm wamepitisha kataba kwa kishindo. Hawa wabunge sengi sana hawakushinda kwenye box la kura 2020, kama hadi hapa unajitoa ufahamu sina la kucomment
 
Back
Top Bottom