Makonda: Suala la Pauline Gekul, CCM ina taratibu na kanuni zake kuanzia Ngazi ya Tawi, hivyo kama likifika Taifani tutalitolea taarifa

Makonda: Suala la Pauline Gekul, CCM ina taratibu na kanuni zake kuanzia Ngazi ya Tawi, hivyo kama likifika Taifani tutalitolea taarifa

Nilikuwa nafikiri tu kwa CAPITAL LETTERS!
Hivi, mchujo wa viongozi umetupa watu kama Gekul!
Pauline Gekul alikuwa waziri mdogo wizara ya Katiba na Sheria.

Watu kama Gekul, ambao si tu hawana maadili, lakini wamediriki kitendo usichoweza kuhadithia mbele ya watoto na mkweo!
Mwanamke kshiriki kumwingiza chupa makalioni mtoto anayeweza kumzaa mwenyewe.

Watu wa aina hiyo, Baraza la Mawaziri wanaweza kutupatia Katiba Mpya kweli?

Wallahi, hili butwaa la Karne.
Swali ni je, kuna mfumo wa kuaminika wa uteuzi? Au ni mtu anaupiga mwingi hata kwenye mambo muhim ya kitaifa?! Kutokana na simulizi tlizosoma, huyu mdada ni kama vile aliokotwa porini na kuukwaa uwaziri, hakufaa hata
 
Mwenezi wa CCM Komredi Makonda amesema kuhusiana na swala la mbunge wa Babati mh Gekul, CCM ni Chama kikubwa na kina taratibu makini

Kuna Vikao Vya nidhamu na Maadili kuanzia Tawini na kuendelea hivyo kama kuna lolote litathibitika Vikao husika vitachukua hatua stahiki na kama litafika Ngazi ya taifa tutalitolea Taarifa

Source: Ayo TV
tawi la GEKULI NI LIPI WAKATI ALIPEWA KADI AKIWA LUMUMBA
 
Vipi na lile sakata lake la kipindi kile la kuvamia Clouds na watu wake wasiojulikana alipokuwa RC wa Dar! Lilifikia ngazi ipi katika chama? Maana tuliona tu Nape Nnauye akitumbuliwa!!
Nape badae basitola shingoni ....kisa kulazimisha Jiwe aangalie Shilawandu wa Gwajima.
 
Swali ni je, kuna mfumo wa kuaminika wa uteuzi? Au ni mtu anaupiga mwingi hata kwenye mambo muhim ya kitaifa?! Kutokana na simulizi tlizosoma, huyu mdada ni kama vile aliokotwa porini na kuukwaa uwaziri, hakufaa hata
Kimaadili ,huyu dada hajafunzwa kabisa public conduct adherence.
Kuna mambo kiongozi haruhusiwi hata kuona, achia kushiriki.
 
Mwenyewe picha ya uyo mama atuwekee tumuone
 
. ChoiceVariable FaizaFoxy Pascal Mayalla kinachoitwa vetting huwa kinafanyikaje??
Vetting inafanyika kama ifuatavyo
Hatua ya kwanza ni
1. Data collection kuanzia birthdata, parents, education, employment. Kila mtu kila mahali uliposajiliwa kuna file lako.
Trail, unafuatiliwa public & private life, kila mkoa, kila wilaya, kila kata kila mtaa, kila ofisi kuna wale "jamaa zetu"
2. Hatua ya pili ni security clearance, kama ulifanya jinai yoyote.
3. Hatua ya tatu ni Data processing, wanazichakata data zako na kutoa recommendation
4. Mamlaka ya uteuzi inapelekewa majina plus recommendation.
5. Mamlaka ya uteuzi inafanya uteuzi.

JPM aliupuuza huu utaratibu, alipotaka kumteua Antony Mtaka, Recommendations zili reccomend hafai hata kuwa katibu kata!. JPM akaipuuza recommendations yao akamteua!, ikaja ku happens ndio the best RC, JPM akampeleka Dodoma.

Jaji Mkuu Othman alipofikia kustaafu, JPM alipopelekewa majina, akawaona wote hawafai, akampick mtu nje ya recommended na kumkaimisha u CJ!.

Haya madudu yote ya teua tumbua ya Rais Samia, sio yeye ni hao jamaa wa vetting hawatimizi wajibu wao kikamilifu Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda

Ila pia kuna baadhi ya hawa vetting imefanyika vizuri kabisa, wakati wanateuliwa they were good, baada ya uteuzi wanaota mapembe!, wanabadilika wanakuwa ma beasts!.

P
 
Bro Paskali, y're a good source of valuable info. only that you mix that with personal values. Suala la yy kuwa binadamu pia, wkt makosa yanarudiwa rudiwa, linakosa uhalali. Ajitutumue, aende na itifaki za ki-managementi alizozikuta na za wakati. Nje ya hapo ni kamari tu
 
Mwenezi wa CCM Komredi Makonda amesema kuhusiana na swala la mbunge wa Babati mh Gekul, CCM ni Chama kikubwa na kina taratibu makini

Kuna Vikao Vya nidhamu na Maadili kuanzia Tawini na kuendelea hivyo kama kuna lolote litathibitika Vikao husika vitachukua hatua stahiki na kama litafika Ngazi ya taifa tutalitolea Taarifa

Source: Ayo TV
Kiswahili ni suala siyo swala (mnyama)
 
Acha uzushi na uongo, je hatua zikichukuliwa utauficha wapi uso wako

Sent from my Infinix X656 using JamiiForums mobile app
Kama ilishindikana kuchukua hatua dhidi hata ya yeye mwenyewe, kwa nini iwe dhidi ya wengine? Kuna usanii mwingi ndani ya CCM. Kama angekuwa ametoa kauli za kukosoa viongozi au Serikali, hapo lazima hatua zingekuwa ni mara moja.
 
Back
Top Bottom