Makongoro Nyerere: Nimenusurika, kama ningeondolewa ningesikitika maana ndio kwanza nimeanza kuwazoea

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607


Saa chache baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kufanya mabadiliko ya Wakuu wa Mikoa na kuwaondoa tisa, leo Alhamisi Julai 28, 2022, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Makongoro Nyerere amemshukuru mkuu huyo wa nchi kwa kuendelea kuhudumu katika mkoa huo na kusisitiza kuwa amenusurika.

“Rais (Samia Suluhu Hassan) amefanya mabadiliko ya wakuu wa mikoa kwa nia njema, lakini mimi ndugu yenu nimenusurika, kama ningeondolewa ningesikitika maana ndio kwanza nimeanza kuwazoea,” - Makongoro Nyerere.

Makongoro ameyasema hayo leo hii wakati wa zaiara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Innocent Bashungwa akikagua ujenzi wa miundombinu ya Shule ya Sekondari Matui Wilayani Kiteto.
 
Mako muhuni sana, ananata na bit la Bi. Mkora
 
Hakumtendea haki baba yake, na yeye alitakiwa awe kwenye nafasi ya kuwa rais, ona sasa tunapata hadi marais waliosukumiziwa na wale wengine wa ngekewa.
 
hii inaitwa Defense mechanism.!
 
Huyu mipombe mikali imemuathiri sana kiafya ya mwili na akili pia.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…