LGE2024 Makosa Matatu ya Mdude Nyagali: Kujeruhi, Matusi na Kuvuruga Uchaguzi, Wakili Boniface Mwabukusi kumtetea

LGE2024 Makosa Matatu ya Mdude Nyagali: Kujeruhi, Matusi na Kuvuruga Uchaguzi, Wakili Boniface Mwabukusi kumtetea

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Imeelezwa kuwa kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mdude Nyagali Mdude anayeshikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Songwe anatuhumiwa kutenda makosa matatu (3) ikiwemo kujeruhi, kutoa lugha ya matusi na kuvuruga ratiba ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2024

Hayo yameelezwa na Wakili wake Boniface Mwabukusi kupitia chapisho aliloweka kwenye mtandao wake binafsi wa kijamii wa X Novemba 24.2024 ambapo ameeleza kuwa yeye binafsi akiwa ameambatana na Mbunge wa zamani wa Mbozi (CHADEMA) Paschal Haonga na mtu mmoja aliyemtaja kwa jina la Abdulkareem kwa pamoja wamefika kwenye kwenye kituo cha Polisi Itumba, Ileje anachoshikiliwa Mdude na kusimamia mahojiano yake

Kupata nyuzi za kimkoa Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Amesema licha ya kwamba Jeshi la Polisi limeanza kumuhoji lakini Mdude yeye amegoma kutoa maelezo ya ziada kituoni hapo badala yake ametaka afikishwe Mahakamani ili akatolee huko maelezo hayo, jambo ambalo Wakili Mwabukusi amesema ni haki yake ya kisheria.
1732511425236.png
Kupitia chapisho hilo, Wakili Mwabukusi ambaye pia ni Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) ameendelea kufafanua kuwa makosa anayoshtakiwanayo mteja wake yanadhaminika hivyo waliomba apatiwe dhamana hiyo lakini hata hivyo jambo hilo liligonga mwamba kutokana na kile walichoelezwa kuwa maafisa wengine wa Polisi wanataka kumuhoji kutokana na makosa mengine anayodaiwa kuyatenda mkoani Mbeya

Kutokana na hilo, Wakili Mwabukusi ameahidi kurudi kituoni hapo leo, Jumatatu Novemba 25.2024 ili kuendelea kumsimamia mteja wake na kwamba dhamira ni kuona haki za kisheria na Kikatiba za Mdude Nyagali zinapatikana.
1732509300126.png
 
Haya ndiyo yatavunja heshima ya rais wa TLS, kukaa desk moja na wahuni ambao wanatakiwa kuchapwa bakora kwa utovu wa nidhamu, nashauri atume wakili mwingine!
 
Haya ndiyo yatavunja heshima ya rais wa TLS, kukaa desk moja na wahuni ambao wanatakiwa kuchapwa bakora kwa utovu wa nidhamu, nashauri atume wakili mwingine!
CCM akili kiduchu sana, kusema kumtetea sio lazima yeye aende physically, anaweza kutumavwakili
 
Mdude Nyagali,

Mungu amsaidie Sana misukosuko anayopitia tangu nianze kumsikia ni mingi mno
 
ccm akili kiduchu sana, kusema kumtetea sio lazima yeye aende physically, anaweza kutumavwakili
Rais wa TLS, Kukitaja kiroboto kama Mdude is a big shame, tulitaraji awe anahoji mambo mazito mazito hasa ya kimikataba, tujifunze kukaa kwenye position zinazoendana na cheo fulani.
 
Tupate lidubwana levi linaloropoka ropoka hovyo halina strategic frame work useme Tutaendelea sana mimi na mch. Mwamakula tunastaajabu sana!
Hilo dubwana levi limekuacha mbali sana kiakili, ambacho wewe unalizidi ni upambavu tu, hicho ndiyo unalizidi
 
Back
Top Bottom