Makosa tunayofanya kwenye 20s

Makosa tunayofanya kwenye 20s

Beberu

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2017
Posts
4,548
Reaction score
9,740
Jisalimie mwenyewe mi nipo busy bana 😂😂

Ujana hususani miaka ya 20-35 ni miaka muhimu sana kwenye maisha, hapo ndipo watu huajiriwa na kuanza kuzishika pesa, huwa huru, huoa/olewa, humaliza masomo etc, ila kipindi hiki ndicho chenye makosa mengi sana kwa kuwa huwa kunakuwa na trial and errors nying sana hapa, sasa bas leo KENSHOP wauzaji wa TV tunakuletea makosa ambayo wengi wetu huwa tunayafanya katika umri huo,

#1. Kutowekeza mapema
Wengi tunashika pesa lakini hatuwazi future, unalipwa 700k let's say ila unaitumia bila kusave, (si itakuja nyingine), ila leo wacha nikuume sikio, ukiwa na mazoea ya kusave japo 100k kwa mwezi kupitia UTT (Ndo ninayoijua ipo vizuri kwa savings) ambapo utapata riba ya 14% kwa mwaka bas ndani ya miaka 10 utakuwa na kama 25M, ( Hii pesa mikoa mingi hapa nchi unasimamisha nyumba ya familia ya kuishi kabisa, vitabaki vitu vichache sana,

Ukiweka 200k kila mwezi, bas jiandae kwenye 50M hiv baada ya miaka 10, vipi ikiwa 20 je 🤔 inakaribia 200M (wazee kibao wenye 45 hawana utajiri wa 200M), ila sio lazima iwe UTT, nunua Viwanja, panda miti, nunua hisa za makampuni mbali mbali, fanya vyote lakini weka malengo yako ya mbele, ukianza mapema hutaumia mana utajikuta unawekeza kidogo dogo then ukifika 35 unaweza jikuta una 100M kama utani tu
Nb. Msiseme kuporomoka kwa thamani ya pesa mana 100M ya 2013 na 100M ya sasa bado zote ni ngumu tu same na ya 2033

#2. Kutokuwa na bima, weka siasa za Ummy mwalimu kando, ndugu zangu kuwa na bima ni muhimu sana, ukiingia hospital ukitoka hujaacha 50k shukuru Mungu, ukilazwa hospital usipotoa bill ya 1M nenda kasali, Ndugu zangu gharama za matibabu ni kubwa sana, kata bima yako ya 192, au ile ya 350, kwa wenye familia nako bima ya mama baba na mtoto ni 600k nadhani, ukiwa na bima hata ukipata mgonjwa ndani ya familia yako haitakuyumbisha kiuchumi tofauti na ukiwa huna,
Wote ni mashahidi ya ndugu zetu waliofirisika kisa ugonjwa, hata usipoumwa wew lipa na kata bima kama mjinga, Ya Mungu mengi hujui lini utaumwa ikusave, siku hizi ajali ni nje nje tu.

#3.Kutofanya mazoezi, sio lazima uwe kibonge kama Amina bonge ndio ufanye zoezi, wew anza hata saizi, gharama za ubonge ni kubwa sana, Gharama za kutibiwa magonjwa yasiyo ambukizwa ni kubwa, halafu ukifanya zoezi hata kunyanduana unaenjoy zaidi 😋😋😋😋

#4. Kuparty sana, hakuna maelezo hapa, ni matumizi mabovu ya pesa, nenda club mara moja kwa mwezi, kama unapata ulabu heb pata kwenye glocery bia zako tatu urudi ndani kulala, hakikisha unakuwa na balance kati ya Bata na Kuwekeza kwa ajiili ya future yako

#5. Kununua vitu visivyo na msaada kwao na vya gharama, mfano mtu ananunua gari lakin ukicheki hilo gari sio la ulazima kwake kutokana na mazingira yake, na mbaya zaidi wengine tunakopa kabisa ili kupata gari la kutembelea, wekeza kwanza ukipata pesa au ukiwa na ulazima wa kununua gari ndio ununue gari unaloweza limudu, gharama za kutunza gari zipo vizuri sana, zinaweza fika hadi 200k kwa mwezi, sasa si bora ungekuwa unapanda mwendokasi kisha pesa ukaweka UTT ndani ta miaka miwili ukasimamisha mjengo wa maana

Ahsante kwa kuwa nami, mpaka wakati mwingine
Mm ni yule yule Beberu J,
Alamsik
pexels-photo-6192328.jpeg
 
Ngoma ingia ucheze ndio utaijua!? Hii ya kuweka 200000 Kisha baada ya miaka kumi kuwa na 50m !? Hizi Huwa ni nadharia theory!! Tekelezaji wake ni mgumu mno!!!
Hakuna kisicho wezekana mkuu,anza sasa usingoje kesho. Mi nmeanza kusave 250k kila mwezi,kuanzia mwaka 2018..ni pesa ambayo inakatwa moja kwa moja kwenye mshahara baada ya kujaza fomu maalumu Nmb na kuingia kwenye account ambayo siwezi ku access kwenye 🏧 labda kwa kutolea ndani. Sijawahi kuigusa hyo pesa mpka sasa.
 
Hakuna kisicho wezekana mkuu,anza sasa usingoje kesho. Mi nmeanza kusave 250k kila mwezi,kuanzia mwaka 2018..ni pesa ambayo inakatwa moja kwa moja kwenye mshahara baada ya kujaza fomu maalumu Nmb na kuingia kwenye account ambayo siwezi ku access kwenye [emoji763] labda kwa kutolea ndani. Sijawahi kuigusa hyo pesa mpka sasa.
Unafanya vema mkuu.

Mimi nasave 200k kila mwezi NBC Bank bila kuigusa.
 
Sasa miaka 10 yote hiyo nangoja 25m, nikikufa sasa, ngoja ngoja yaumiza matumbo acha zikwishe tupige sarakasi na ulimwengu.

Miaka kumi michache sana mkuu, Ni juzi tulikuwa tunaruka na Lowasa majukwaani 2015, mwakani ni 2025 tayari
 
Kukumbushana ni kuzuri.
Ninyi ndio member mlonifanya nikaipenda jf maana ni postive tuu na mkikosoa mnakosa haswaaa kwa fact.

Barikiwa sana mkuu

Kwa nyongezaaa sikuhizi unaweza kufungua akaunt kwenye benk flan na ukafanya kitu inaitwa standing order kama sijakosea wao wakawa wanachukua kiasi ulichotaka kwenye account yako ya benk

Pia hizi account zinakuwa na riba flan kwa mwaka

Mkuu shukran sana kwa kutukumbusha
 
Back
Top Bottom