Elections 2010 Makosa ya CCM, JK ni mzigo usiobebeka

Elections 2010 Makosa ya CCM, JK ni mzigo usiobebeka

Joined
Jan 16, 2007
Posts
721
Reaction score
178
Kama kuna kosa amabalo imelitenda CCM kwa mwaka huu wa uchaguzi,ni kumchagua JK kugombeea nafasi ya Uraisi kupitia CCM.Inaeleweka hii ni kutokana na mazoea kwamba mtu anaepitishwa na CCM inabidi agombee vipindi viwili.Sasa nashindwa kuielewa kama ndio hivyo walivyoamua kwanini wawe wanapoteza pesa katika mchakato wa kumpata mgombea urais katika chama chao?Kama ccm wangelikua makini wangetumia kipindi cha miaka mitano kumpima mgombea wao ni kwa kiasi gani ametimiza sera ya chama.Kama alivurunda nibora wakamuweka mgombea mwingine.Naimani katika CCM kunawatu wengi makini amabao wanaweza kufanya vizuri zaidi ya huyu msanii Kikwete.Lakini kutokana na mazoea mchakato wa kumpata mgombea kutoka ccm inabaki kama formality,vurunda usivurunde miaka kumi ni yako.Hii inaondoa changamoto kwa mgombea na kutokua na dhamana kwa aliyoyatenda katika kipindi chake.TENDA UTAKAVYO FANYA UTAKAVYO MIAKA KUMI NI YAKO.Kwa bahati mbaya CCM wameshindwa kusoma mishale ya wakati.Watatumia pesa nyingi,watatumia mbinu chafu,wataiba kura,watawanunua wapiga kura n.k ukweli unabaki palepale KIKWETE NI MZIGO USIOBEBEKA,MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
wandugu nipeni data sheria inasemaje kama mgombea amepima maji akagundua ni mazito na akataka kujitoa? nikimwangalia Jk naona maji yamemfunika kichwa na anashindwa kupumua
 
Anachofaya sasa hivi ni kutoa ahadi ambazo anajua fika hana mpango wa kuzitekeleza kwa sababu anajua hiki ni kipindi chake cha mwisho kwake kugombea na baada ya hapo atakua na kinga ya kutoshitakiwa.

Sijui sheria inasema nini kwa mgombea anaetoa ahadi halafu asitekeleze, Hivi hakuna sheria ya kumuadabisha kiongozi wa aina hii au kuadibisha chama chake? Maana ahadi anazotoa huyu jamaa sijui kama ametumemwa na chama chake kuziahidi au anaahidi chochote tu kinachomjia kichwani? Mwaka 2005 alitoa ahadi chungiu nzima lakini nyingi hakuzitekeleza na nashangaa kwanini hajafunguliwa mashitaka kwa kuwadanganya watanzania.

Kuna haja ya kuadabisha watu au chama kinachoropoka tu ahadi bila ya kuzitekeleza.
 
CCM haina jipya. Walidhani wataendelea kuwadanganya watanzania kwa kuiba kura. mwaka huu hatudanganyiki.........
 
Tukapige Kura tukumbushane jamani KURA NI MUHIMU!
 
Habari njema ni kuwa kuna watanzania ndani ya CHADEMA ambao wana unchungu na nchi na wanaitakia mema. CCM na vibaraka wao tatizo lao kubwa ni kufikiri kuwa wao ni watanzania zaidi ya wengine. Nyote ambao mnauelewa walelimisheni wadau wengine kwamba kura ni kwa upinzani ili waongoze taifa hili.
 
Back
Top Bottom