Makosa ya miaka mitano ya Hayati Magufuli yanasahihishwa sasa. Hongera CHADEMA kwa kuongoza hili kwa ufundi mkubwa

Makosa ya miaka mitano ya Hayati Magufuli yanasahihishwa sasa. Hongera CHADEMA kwa kuongoza hili kwa ufundi mkubwa

Kumekuwa na mijadala mikubwa ikiendelea nchini sasa kuhusu yale yanayoitwa maridhiano ya kisiasa. Kimsingi ni maridhiano kati ya chama tawala na vyama vya upinzani. Lakini haikupaswa kuwa hivyo tu, wapo watu binafsi, mashirika na makampuni binafsi na hata baadhi ya nchi ambazo kipindi cha utawala wa Magufuli walivurugwa na kusababisha maumivu makubwa. Tanzania ilipoteza sifa yake ya kimataifa kama taifa la haki na amani.

Nayaunga mkono maridhiano yanayoendelea hivi sasa. Rais Samia ameonesha utayari kwa kiasi kikubwa na nina imani yapo mengi sana yatafunguka na hii itaifanya nchi yetu kurudia tena kuwa taifa lenye kuaminika katika medani za haki na amani.

Zaidi sana nawapongeza viongozi wa CHADEMA kwa ufundi mkubwa wa kuongoza na kuleta maridhiano yenye kuleta haki na amani. Wale msiopenda maridhiano ni watu wasioitakia mema nchi yetu na mtabaki kuponda jitihada hizi kwani mlifaidika na dhuluma zilizokuwepo. Hongera Samia, Mbowe na wote wenye mapenzi mema.
Kisa JPM hakuhudhuria kikao cha CDM?. Hata JPM angeenda ila hakuwa mtu wa asali.

Mbona Mbowe alihudhuria mikutano ya JPM ikiwemo ya wafanyakazi na alipewa nafasi ya kusema?

Mambo ya kulambishana Asali na kusahau shida za wananchi ndio unayasifu?

Sasa Kilo ya Unga na Mchele havishikiki. Siku hizi kula maharage ni anasa. Tembele kwenda mbele.
 
Na ndio tatizo lilipo yani bado tunaangali makosa yaliyopita tukija kushtuka haya makosa ya sasa yashakomaa. Samia hawezi kuwa Rais kwa kuondoa makosa tu yaliyopita.
"Sijaona makubwa zaidi", haya yaliyopo yanafanyiwa kazi kwa sababu nia ipo kati ya pande mbili, tofauti na wakati ule, kutekana na kuuana na ukitaka make chini mzungumze muuaji hana huo muda.
 
Wanasiasa wakimalizana tofauti zao wananchi wanafaidika nini, kwamba kila mmoja atapatiwa mbolea ya ruzuku? Au unadhani kila mwananchi anahangaikia nafasi za kisiasa?
Wanasiasa wakipatana hapo patakuwepo na nia ya kufanya kazi kwa pamoja na kusikilizana, hivyo itakuwa rahisi kwa upande mmoja kusikiliza hoja za upande wa pili na kuzifanyia kazi kwa maslahi ya taifa, nchi na wananchi wataneemeka kwa hilo.
 
Kisa JPM hakuhudhuria kikao cha CDM?. Hata JPM angeenda ila hakuwa mtu wa asali.

Mbona Mbowe alihudhuria mikutano ya JPM ikiwemo ya wafanyakazi na alipewa nafasi ya kusema?

Mambo ya kulambishana Asali na kusahau shida za wananchi ndio unayasifu?

Sasa Kilo ya Unga na Mchele havishikiki. Siku hizi kula maharage ni anasa. Tembele kwenda mbele.
Huu wimbo wa asali mnapenda kuuimba sana, lakini mkiambiwa mtoe ushahidi wa hilo hakuna yeyote kati yenu anayeweza kufanya hivyo.

Kwenu mtu kupewa haki zake mnakereka, mnaumia, hamkumbuki maumivu waliyopitia wakati wa huyo JPM mnaemsifu, leo wanapewa kile walichonyan'ganywa mnawaita wanalamba asali.

Mlitaka waendelee kuonewa miaka yao yote, kuteswa miaka yao yote, ndio mridhike muwaone wapambanaji, hiyo ilikuwa ni mentallity ya kikatili iliyopandikizwa vichwani mwa watanzania na kiongozi mshamba.

Wakati wenu ndio huu, utoeni huo ujinga vichwani mwenu, kwasababu naamini hamkuwa nao kabla ya Magufuli, msiendelee kuishi kwenye fikra za kikoloni, hii nchi ni yetu sote, na wote tuna haki sawa.
 
Huu wimbo wa asali mnapenda kuuimba sana, lakini mkiambiwa mtoe ushahidi wa hilo hakuna yeyote kati yenu anayeweza kufanya hivyo.

Kwenu mtu kupewa haki zake mnakereka, mnaumia, hamkumbuki maumivu waliyopitia wakati wa huyo JPM mnaemsifu, leo wanapewa kile walichonyan'ganywa mnawaita wanalamba asali.

Mlitaka waendelee kuonewa miaka yao yote, kuteswa miaka yao yote, ndio mridhike muwaone wapambanaji, hiyo ilikuwa ni mentallity ya kikatili iliyopandikizwa vichwani mwa watanzania na kiongozi mshamba, wakati wenu ndio huu, utoeni huo ujinga vichwani mwenu, kwasababu naamini hamkuwa nao kabla ya Magufuli.
Tunawazoom tu mkilambishana asali.
 
Haya ni malidhiano ya wanasiasa wala hayana matokeo yoyote chanya kwa wananchi!!, Wanasiasa wa Tz ni wabinafsi na wenye roho mbaya Sana!.
 
Kwa hiyo mmemuarika Samia ili kumnanga mtemi wetu wa SUKUMA GANG Mzee JPM?
 
Hii move ni nzuri lakini upande wa Chadema wafanye kwa tahadhari sana. Alichofanyiwa Maalim Seif Zanzibar na alichofanya JK kwenye katiba mpya ni funzo
Hapo katiba mpya na tume huru zinatafutwa.

Zikipatikana utaona habari tofauti na sasa.

Na istoshe wapo kwenye maridhiano. Huwezi attack adui yako wakati mnapatanishwa.
 
Hapo katiba mpya na tume huru zinatafutwa.

Zikipatikana utaona habari tofauti na sasa.

Na istoshe wapo kwenye maridhiano. Huwezi attack adui yako wakati mnapatanishwa.
Ili Katiba nzuri ipatikane lazima Chadema wawe na wawakilishi Bungeni, hivyo Uchaguzi wa 2025 Chadema hawana budi kushiriki....

Kuna ile hali ya Toa hiki Upate hiki
 
Kwenu mtu kupewa haki zake mnakereka, mnaumia, hamkumbuki maumivu waliyopitia wakati wa huyo JPM mnaemsifu, leo wanapewa kile walichonyan'ganywa mnawaita wanalamba asali.
2024 na 2025 mtapata haki zenu zengine kutoka kwa CCM na vyombo vya dola.
 
Ili Katiba nzuri ipatikane lazima Chadema wawe na wawakilishi Bungeni, hivyo Uchaguzi wa 2025 Chadema hawana budi kushiriki....

Kuna ile hali ya Toa hiki Upate hiki
Kwa hiyo tume huru tayari imepatikana ?
 
Back
Top Bottom