Makosa yaliyowagharimu Simba leo Agosti 13, 2022

Makosa yaliyowagharimu Simba leo Agosti 13, 2022

Umeona goli la sakho lile licha ya simba kufungwa ila wametoa burudani safi kabisa derby hazitabiriki kama furaha ya Yanga nikuifunga simba halafu kimataifa mnatobolewa basi hongereni tukutane CAF kwa wakubwa huko.
Mbumbu x2
 
Mimi nimeangalia mchezo lakini sijaona kosa lolote la Beno. Hakuna kosa la kipa hata moja. Sheria ya ulinzi ni mabeki wakabe mtu asipige, akipiga na kama hajakulenga kwa size ya goli basi asilimia ya kufungwa inakuwa kubwa. Kaka unazungumzia kiwango cha Beno kivipi?
Hana kosa lakini hana ubora sana. Ubora wa kipa unaonekana mabeki wanapofanya makosa. Kuitwa kipa bora maana yake ni kufanya saves.
Hakuna kipa asiepigiwa mashuti lakini sio ukipigiwa iwe imo kisa eti mabeki wamefanya makosa. Magoli yote yamepita karibu yake na huyu angekuwa ndie kipa kule south dhidi ya Orlando hata penati tusingefika.

Ukweli ni kwamba Manula yuko mbali sana yaani kaimarika wakati Beno ni Manula wa zamani.
 
Simba wakiulizwa ni kwa nini huwa wanafungwa na Yanga kila siku👇😁😁😁
 
Simba viongozi wao wanajifanya wajuaji, usajili wanafanya wanavyojisikia wanasingizia mapendekezo ya kocha.
Unamtoa Thadeo umemsajili nani kuziba nafasi yake swala la ushambuliaji limeongelewa muda mrefu lakini wachezaji wanaoleta hawakidhi Bado wameendelea kujaza mawinga na viungo washambuliaji.
Kufanya mazoezi ya wazi hii imesemwa lakini wanajifanya hawasikii.
 
Simba imefungwa kwa makosa ya bench la ufundi sio uwezo wa mchezaji mmoja mmoja.Bench la yanga liliamua matokeo uku la simba likiamua kupoteza mchezo.Makosa madogo madogo uwanjani yapo na nikawaida ndo maana timu zinafungwa ila je baada ya kufungwa unakuja na mbinu gani za kurekebisha mambo ili nawewe ufunge hapo ndipo bench la ufundi la simba lilipokwama.Kakolanya ni mzuri ila ana tatizo lakukosea makadirio wakati wa kuruka.Ni golikipa ambaye hafatilii moves za mpira kwahiyo akipigiwa shuti ndo anakua kama anashtuka na kuruka ndo maana jana kafungwa magoli ya aina moja.
 
Footwork yake haipo sawa kuanzisha mashambulizi na mipira ya juu haruki.

Kwenye footwork nakuunga mkono na hili sio tatizo la Beni tu hata Manula footwork yake sio nzuri sana, yule kipa wa Yanga kaiva katika hili.
 
Simba viongozi wao wanajifanya wajuaji, usajili wanafanya wanavyojisikia wanasingizia mapendekezo ya kocha.
Unamtoa Thadeo umemsajili nani kuziba nafasi yake swala la ushambuliaji limeongelewa muda mrefu lakini wachezaji wanaoleta hawakidhi Bado wameendelea kujaza mawinga na viungo washambuliaji.
Kufanya mazoezi ya wazi hii imesemwa lakini wanajifanya hawasikii.
Ata mimi naona usajili wa kocha ni huyo mzungu tu ila wengine ni usajili na ujuaji wa viongozi wao wenyewe.
 
Ata mimi naona usajili wa kocha ni huyo mzungu tu ila wengine ni usajili na ujuaji wa viongozi wao wenyewe.

Mzungu na yule beki Outtara. Jana kocha kakosea mwenyewe tu kwa zile sub zake, pale ni bora angempumzisha mwenda akaingia kapombe basi.
 
Simba kipindi cha kwanza mmecheza mchezo mzuri lakini binafsi nadhani ni sababu ya wrong selection ya kikosi kwa kocha wa Yanga.

Aziz alianzia pembeni ambapo sio mzuri sana akitokea pembeni hivyo alichezeshwq off position pia Farid Musa anapenda sana kuchezea mpira na kufanya beki line ya Simba i recove position kwa haraka.

Alipoingia moloko ana kasi na Aziz ki akarudi kati kule pembeni hapo ndipo Yanga wakarudi mchezoni.

Mzungu siwezi kumlaumu ameingia tayari Simba mmeshapoteana mipira haifiki kwa wingi mbele.
 
Simba wana bahati kufungwa magoli mawili tu, ilitakiwa yawe manne. Wanaudhaifu mkubwa sana, wajitathmini kama kweli wanataka kufika mbali.
 
MAKOLo....... TAABU IPO PALE PALE
FB_IMG_16604208994671057.jpg
 
Shida kubwa ya Simba ni kiungo mkabaji ambaye yuko fiti na active uwanjani kwa dk 90 sio unamtegemea mkude anae duwaa hana spidi hajui kukaba na akikaba anakabia matako,magoli yote yalifungwa huku mkude akimuangalia Mtoa pasi bila kumdistab.
Bila kumsajili Kiungo wa ukabaji katili au inonga apandishwe sita pale nyuma wacheze Onyango na Outtara tutaendelea kupigwa.Yote kwa yote Kuna kitu kimebadilika kwenye tm tumpe mwalimu muda
Habari za wakati huu wadau,

Ndugu zangu wa simba poleni sana na hongereni sana yanga mabingwa wa kihistoria kwa ushindi wa leo.

Karikoo derby imemalizika kwa ushindi wa goli 2 kwa 1 kwenye mchezo huo ilaUkiangalia mechi jinsi ilivyokuwa team ziligawana umiliki wa mpira na uchezaji katika vipindi tofauti kwa maana ya yanga kipindi cha pili na simba kipimo cha kwanza na kila team ilitumia kipindi chake vizuri na matokea kumalizika kwa yanga kushinda kwenye mechi hyo.

Licha ya simba kucheza vizuri kipindi cha kwanza ila walipoteza nafasi nyingi ambazo zingeweza kuwa magoli lakini kiyombo na kibu denis walikosa utuliku kama waliokuwa nao sakho na chama wanapoingia kwenye box au karibu na lango la mpinzani.

Izrael Patrick mwenda hakutakiwa kurudi kipindi cha pili alifanya makosa mawili kipindi cha kwanza baada ya kupiga back pass zilizoishia njiani na kuishia kwa wachezaji wa team pinzani lakini hata kwenye kushambulia na kukaba kwa wakati hakuwa na kasi na kusababisha inonga kufanya kazi yake alipokosekana kapombe alihitajika kipindi cha pili.

Simba wanahangaika na usajili ila eneo la goal kipa hawalipi kipao mbele licha ya kuwa na changamoto pale simba ukimtoa manula hakuna kipa mwenye consistency kucheza iwe kwenye league au kimataifa kakolanya ana shida ya mipira ya juu na ile ya kurudishiwa mingi anapiga nje badala ya kuanzisha mashambulizi mbadala wa manula unahitajika wasipokuwa serious simba kwenye eneo hlo yajayo yana furahisha kakolanya hafai kwenye league wala kimataifa kiwango kimeshuka huenda kukaa benchi mda mrefu kumemuathiri.

Enonga ni beki mzuri ila ana masikhara sana iwe mechi za kimataifa au za league kuu viongozi huenda wanaliona hlo tatizo ila wanalipuuzia na leo athari yake imeonekana kuna siku atakuja kuigharimu team kwenye mechi muhimu zaidi ya leo tshabalala alitakiwa aongee naye wakati mchezo ukiwa unaendelea kama captain ila badala yake mkude ndo huwa ana ongea mara kwa mara enonga asipoacha utoto yajayo yanafurahisha.

Striker za simba ni tatizo jingine aina ya uchezaji wa kibu na kiyombo unafanana ni wachezaji ambao hawana utulivu wakiwa na mpira sehemu wanayo takiwa watoe pasi wanapiga sehemu ya kupiga wanapiga chenga zisizo na maana hawana utulivu kwenye eneo la mwisho yule mzungu hafai hata ndondo cup maana hata fitness yake haipo sawa ndo maana leo ilikuwa wanakosa nafasi za wazi za kufunga na kutoa pasi.

Simba imebadilika ikiwa haina mpira inacheza vizuri kwa ku retains possession haraka na kuziba nafasi zilizo wazi mpaka pale alipotoka sadio kanoute, chama na mkude ndo hali ikaanza kubadilika maana Aziz Ki na Feisal walikuwa free na kutengeneza nafasi za magoli labda kocha wa simba kuna kitu alitaka kujaribu lakini hakikufanikiwa na simba kupoteza mchezo.

Kocha wa simba anaonekana anapenda soka la kasi team ikiwa na mpira ila katika vitu vitakavyomuondoa haraka simba ni sakata lake la kumkataa phiri na kumchezesha mzungu na kumuamini zaidi mwenda kuliko kapombe na chama anavyowaamini akiendelea hvyo hamalizi msimu hata derby ijayo anaweza asifike.

NB:Tatizo kubwa la yanga hawajui kucheza kipindi wakiwa hawana mpira kwa walivyocheza leo wakikutana na team yenye kasi kama ilivyokuwa vipers watapata tabu wanachelewa kurudi kwenye eneo la ulinzi na ku retains possession kwa haraka.

Huu sio uchambuzi ni mtazamo na maoni yangu na wewe unaruhusiwa kuweka ya kwako.
 
Umeona goli la sakho lile licha ya simba kufungwa ila wametoa burudani safi kabisa derby hazitabiriki kama furaha ya Yanga nikuifunga simba halafu kimataifa mnatobolewa basi hongereni tukutane CAF kwa wakubwa huko.
Goli la Sakho ni offside ya wazi kabisa
 
Goli la Sakho ni offside ya wazi kabisa
Mh mh basi mbili bila na bora mmeshinda yanga maana lingebaki lile moja lawama zote zingeenda kwa tff.
 
Hata kumuanzisha Kibu na Kyombo ni makosa hawa wote wanafanana ni watumia nguvu na papara,ni sawa na Kanoute na mkude sio wazuri kunusa hatari na mkude ndio hajui kabisa art ya kukaba
Mzungu na yule beki Outtara. Jana kocha kakosea mwenyewe tu kwa zile sub zake, pale ni bora angempumzisha mwenda akaingia kapombe basi.
 
Shida kubwa ya Simba ni kiungo mkabaji ambaye yuko fiti na active uwanjani kwa dk 90 sio unamtegemea mkude anae duwaa hana spidi hajui kukaba na akikaba anakabia matako,magoli yote yalifungwa huku mkude akimuangalia Mtoa pasi bila kumdistab.
Bila kumsajili Kiungo wa ukabaji katili au inonga apandishwe sita pale nyuma wacheze Onyango na Outtara tutaendelea kupigwa.Yote kwa yote Kuna kitu kimebadilika kwenye tm tumpe mwalimu muda
Mpira wa Bongo bado sana kiungo mkabaji sio lazima awe katili kuna watu wanakaba soft na ni bora wana cut pass lines tu mfano Busquets na Rodri ushawaona wana ukatili?

Mpira umechange sana hufikurii kwanini viungo wakatili wana fail kotei alikuwaje anakaba sana ila team ikiwa na mpira hana faida vivyo hivyo kwa Lwanga anakaba ila team ikiwa na mpira ni useless.

Kocha wa simba alikosa plans na usajiri wa okwa sjui Okra naona ni kamari tu wazee

Kama wapo serious wamchukue manzoki haina ata haja ya kuwa na kiungo mvunja kuni
 
Back
Top Bottom