KERO Maktaba ya Vitabu Zanzibar haina Huduma ya Maji, Watumishi na Wanachama tunateseka, tupo hatarini kupata magonjwa

KERO Maktaba ya Vitabu Zanzibar haina Huduma ya Maji, Watumishi na Wanachama tunateseka, tupo hatarini kupata magonjwa

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

NBica

Member
Joined
Sep 13, 2010
Posts
39
Reaction score
36
WhatsApp Image 2025-01-21 at 08.05.23.jpeg
Mimi ni mmoja wa Wanachama wa Maktaba ya Vitabu ambayo ipo hapa Mjini Unguja, changamoto kubwa iliyopo hapa Maisara, Mkoa wa Mjini Magharib ni kukosekana kwa huduma ya maji.

Naomba Wizara ya Elimu pamoja na Bodi ya Huduma za Makataba Zanzibar kushughulikia changamoto hii haraka iwezekavyo, tunapata wakati mgumu sisi Wanachama pamoja na Watumishi wa hapo ambao asilimia kubwa ni Wanawake.

Hii changamoto imekuwepo kwa muda mrefu na hata leo hii Januari 21, 2025 hali ni hiyohiyo kiasi kwamba wale tuliohitaji kupata huduma tumelazima kuondoka hapo ili kwenda maeneo ya jirani kupata huduma.

Wanawake wanashindwa kufanya huduma zao binafsi kwa kuwa hakuna maji, wapo wengine wanaolazimika kwenda na maji kwenye madumu ili wakihitaji huduma waipate.

Unakuta mtu upo hapo kwa kutwa nzima kutokana na aina ya kazi iliyokupeleka pale, ukitaka kwenda kujisaidia unalazimika kwenda kwenye vyoo vya maeneo ya jirani.

WhatsApp Image 2025-01-21 at 08.05.24.jpeg
Changamoto zaidi ni kwa dada zetu, wanashindwa kuswali, pia wakiwa katika mahitaji yao ya kubadilisha au kutumia taulo za kike ni changamoto, wanashindwa kufanya hivyo kwa kuwa maji hakuna.

Wengine ambao wanateseka ni Watoto, wanakuja hapa kusoma ila hakuna maji, wanawezaje kuvumilia kukaa na haja kubwa au ndogo?

Malalamiko yamekuwa mengi, tunaishi kwa kulalamika lakini hakuna hatua ambazo zinachukuliwa, hata Watumishi pia wanalalamika kwa kuwa nao ni sehmu ya wanaoteseka, tunaomba hili lifanyiwe kazi haraka.

UONGOZI WA MAKTABA
JamiiForums
imewasiliana na Mkurugenzi wa Bodi Ya Huduma Za Maktaba Dkt. Ulfat Abdul-Aziz Ibrahim kuhusu suala hilo amesema:

“Ni kweli kulikuwa na changamoto ya maji hapo Maktaba lakini tayari tumenunua mtambo mpya na imetatuliwa na huduma ya Maji inapatikana.”
WhatsApp Image 2025-01-21 at 10.27.04_c6ab16f4.jpg

WhatsApp Image 2025-01-21 at 10.39.37_30502cbf.jpg
 
Wenzako wa huku bara wanakunya kabisa nyumbani kabla hawajafika kazini , vioo vimekufa
 
Mimi ni mmoja wa Wanachama wa Maktaba ya Vitabu ambayo ipo hapa Mjini Unguja, changamoto kubwa iliyopo hapa Maisara, Mkoa wa Mjini Magharib ni kukosekana kwa huduma ya maji.

Naomba Wizara ya Elimu pamoja na Bodi ya Huduma za Makataba Zanzibar kushughulikia changamoto hii haraka iwezekavyo, tunapata wakati mgumu sisi Wanachama pamoja na Watumishi wa hapo ambao asilimia kubwa ni Wanawake.

Hii changamoto imekuwepo kwa muda mrefu na hata leo hii Januari 21, 2025 hali ni hiyohiyo kiasi kwamba wale tuliohitaji kupata huduma tumelazima kuondoka hapo ili kwenda maeneo ya jirani kupata huduma.

Wanawake wanashindwa kufanya huduma zao binafsi kwa kuwa hakuna maji, wapo wengine wanaolazimika kwenda na maji kwenye madumu ili wakihitaji huduma waipate.

Unakuta mtu upo hapo kwa kutwa nzima kutokana na aina ya kazi iliyokupeleka pale, ukitaka kwenda kujisaidia unalazimika kwenda kwenye vyoo vya maeneo ya jirani.

Changamoto zaidi ni kwa dada zetu, wanashindwa kuswali, pia wakiwa katika mahitaji yao ya kubadilisha au kutumia taulo za kike ni changamoto, wanashindwa kufanya hivyo kwa kuwa maji hakuna.

Wengine ambao wanateseka ni Watoto, wanakuja hapa kusoma ila hakuna maji, wanawezaje kuvumilia kukaa na haja kubwa au ndogo?

Malalamiko yamekuwa mengi, tunaishi kwa kulalamika lakini hakuna hatua ambazo zinachukuliwa, hata Watumishi pia wanalalamika kwa kuwa nao ni sehmu ya wanaoteseka, tunaomba hili lifanyiwe kazi haraka.

UONGOZI WA MAKTABA
JamiiForums
imewasiliana na Mkurugenzi wa Bodi Ya Huduma Za Maktaba Dkt. Ulfat Abdul-Aziz Ibrahim kuhusu suala hilo amesema:

“Ni kweli kulikuwa na changamoto ya maji hapo Maktaba lakini tayari tumenunua mtambo mpya na imetatuliwa na huduma ya Maji inapatikana.”
mimi ningekuwa nyinyi,ningekuwa nakunya humohumo maktaba au maeneo ya viwanja vya hiyo maktaba,alafu nachambia nyasi!!,,hamna haja ya kkulalamika,ningetawanya vinyesi mpaka serikali ingejirekebisha!!
 
Back
Top Bottom