Makubaliano ambayo ni mkataba kwa mujibu wa Sheria ya Mikataba ya 2018

Makubaliano ambayo ni mkataba kwa mujibu wa Sheria ya Mikataba ya 2018

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
1609750505463.png

Makubaliano yote ni mikataba kama yatakuwa yamefanywa kwa hiari na watu wanaostahili kufanya makubaliano, kwa malipo ya kitu halali na ambayo hayajatajwa waziwazi na sheria hii kuwa ni batili:

Mikataba yote inatakiwa iwe kwenye maandishi au ifanywe mbele ya mashahidi, au sheria yoyote ihusuyo usajili wa nyaraka.

Sheria hiyo inabainisha kuwa kila mtu mwenye umri wa mtu mzima na mwenye akili timamu, ambaye hajazuiwa na sheria yoyote, ana uwezo wa kuingia mkataba.

Makubaliano yanayofanywa na mtu ambaye hajatangazwa na sheria hii kuwa na uwezo wa kufanya mkataba, makubaliano hayo kisheria ni batili.

Katika kufanya mkataba, mtu anasemekana kuwa na akili timamu wakati wa kufanya mkataba ikiwa ana uwezo wa kuelewa na kutafakari maslahi yake katika mkataba husika.

Sheria inaongeza kuwa mtu ambaye mara nyingi anakuwa na matatizo ya akili, lakini muda mfupi anakuwa timamu, anaweza kufanya mkataba wakati anapokuwa na akili timamu.

Na mtu ambaye mara nyingi anakuwa na akili timamu, lakini muda mfupi anakuwa na matatizo ya akili, hawezi kufanya mkataba muda anaokuwa na matatizo ya akili.
 
Upvote 2
Je kuwa katika influence ya alcohol,drugs,au emotional distress au depression kunaweza fanya mkataba kuwa batili?Kama jibu ni ndio je inathibitikaje kwamba katika wakati wa kufanya uamuzi/mkataba huu mhusika alikuwa katika ahali isiyofaa kufunga mkataba.Na kama jibu ni hapana je ni vigezo gani vinatumika kuamua iwapo mtu hayuko katika hali sawa ya kiakili ya kumruhusu kuingia katika mkataba hasa ukizingatia kwamba uhalali wa mkataba huwa unahojiwa after the fact?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom