Makundi ya wanawake na watoto wapiga hodi nyumba kwa nyumba kuomba unga na chakula kutokana na Uhaba wa chakula

Makundi ya wanawake na watoto wapiga hodi nyumba kwa nyumba kuomba unga na chakula kutokana na Uhaba wa chakula

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Baadhi ya wakazi Wilaya ya Arumeru, Arusha wameomba Serikali kuingilia kati hali ya uhaba wa chakula ambayo sio ya kawaida inayoendelea katika mkoa huo.

Hali hiyo imesababisha makundi ya kina mama na watoto kutembea umbali mrefu wakitafuta chakula kwa kuombaomba maeneo tofauti, ambapo mara kadhaa wameshuhudiwa wakifanya hivyo katika nyumba za watu mbalimbali wakiomba unga na chakula.

Hali hiyo kwa sasa imedumu zaidi ya miezi miwili kutokana na ukame wa kukosekana kwa mvua.

Baadhi ya Kata zilizokumbwa na hali hiyo ya ukosefu wa chakula ni zile zilizopo katika vijiji vya Oldonyo Sambu, King'ori, Ngwansio, Malula, Kata ya Ngaramtoni, Kata za Tindigani na baadhi ya Kata za Wilaya ya Hai

Dora Mollel ni mmoja wa wanawake wanaozunguka mtaani kutafuta msaada wa chakula anasema analazimika kufanya hivyo kwa kuwa hawana hela ya kununua vyakula huku akidai kuwa bidhaa za sokoni zipo bei ya juu, kwa hiyo unafuu waliouona ni kuja mjini kupiga hodi katika mageti ya watu na kuomba unga au chochote kile.

Upande mwingine, baadhi ya wakazi wanaoshuhudia kadhia hiyo wameelezea kusikitishwa na kinachoendelea wakidai kuna wamama ambao wanafikia hatua ya kuomba hata pumba ili wakawapikie watoto wao.

Hali ya wanawake na watoto hao wanaoomba chakula pia ipo katika masoko ya Tengeru na Kisongo ambapo wahusika wanazunguka wakiwa na viroba mgongoni kwa ajili ya zoezi hilo.

Aidha, majira ya usiku wahusika hao wamekuwa na kawaida ya kuokota mabaki ya vitu sokoni kisha wengine wanaomba nauli za kurudi makwao na wanapokosekana wanalazimika kutembea umbali wa kilomita zaidi ya 6.

Siku chache zilizopita Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongela akiwa katika ziara Kata ya Kikatiti, mmoja wa akina mama aliyekuwa katika mkutano huo alimlalamikia kuhusiana na suala la njaa, ambapo kiongozi huyo alitoa kauli kuwa viongozi wafuatilie wahanga wa janga la njaa kutokana na ukame.


==================

UFAFANUZI WA DIWANI
Diwani wa Tarafa ya King’ori, Rosemary Mtalo amesema: “Nimeona hiyo taarifa mtandaoni, kweli kuna watu wana njaa ila siyo kama ilivyoripotiwa, lakini hatujasikia watu waliokufa kwa njaa.

“Michakato ya kuwasaidia imeshaanza, hata hapa tupo mezani tunaijadili, tumeshaongea sana, Serikali iiangalie Wilaya ya Meru na hata Mkuu wa Wilaya anayo hii taarifa.

“Tayari tumeshaandika majina ya kaya na tumependekeza wananchi wapewe chakula.”
 
Baadhi ya wakazi Wilaya ya Arumeru, Arusha wameomba Serikali kuingilia kati hali ya uhaba wa chakula ambayo sio ya kawaida inayoendelea katika mkoa huo.

Hali hiyo imesababisha makundi ya kina mama na watoto kutembea umbali mrefu wakitafuta chakula kwa kuombaomba maeneo tofauti, ambapo mara kadhaa wameshuhudiwa wakifanya hivyo katika nyumba za watu mbalimbali wakiomba unga na chakula.

Hali hiyo kwa sasa imedumu zaidi ya miezi miwili kutokana na ukame wa kukosekana kwa mvua.

Baadhi ya Kata zilizokumbwa na hali hiyo ya ukosefu wa chakula ni zile zilizopo katika vijiji vya Oldonyo Sambu, King'ori, Ngwansio, Malula, Kata ya Ngaramtoni, Kata za Tindigani na baadhi ya Kata za Wilaya ya Hai

Dora Mollel ni mmoja wa wanawake wanaozunguka mtaani kutafuta msaada wa chakula anasema analazimika kufanya hivyo kwa kuwa hawana hela ya kununua vyakula huku akidai kuwa bidhaa za sokoni zipo bei ya juu, kwa hiyo unafuu waliouona ni kuja mjini kupiga hodi katika mageti ya watu na kuomba unga au chochote kile.

Upande mwingine, baadhi ya wakazi wanaoshuhudia kadhia hiyo wameelezea kusikitishwa na kinachoendelea wakidai kuna wamama ambao wanafikia hatua ya kuomba hata pumba ili wakawapikie watoto wao.

Hali ya wanawake na watoto hao wanaoomba chakula pia ipo katika masoko ya Tengeru na Kisongo ambapo wahusika wanazunguka wakiwa na viroba mgongoni kwa ajili ya zoezi hilo.

Aidha, majira ya usiku wahusika hao wamekuwa na kawaida ya kuokota mabaki ya vitu sokoni kisha wengine wanaomba nauli za kurudi makwao na wanapokosekana wanalazimika kutembea umbali wa kilomita zaidi ya 6.

Siku chache zilizopita Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongela akiwa katika ziara Kata ya Kikatiti, mmoja wa akina mama aliyekuwa katika mkutano huo alimlalamikia kuhusiana na suala la njaa, ambapo kiongozi huyo alitoa kauli kuwa viongozi wafuatilie wahanga wa janga la njaa kutokana na ukame.
Waandamane kwenda Kwa mkuu wa Wilaya hadi Mkoa. Huu ni ujinga wananchi wanakuwa ombaomba ndani ya nchi yao na huku wenye nchi mkikamua asali na safari Lukuki achilia mbali tume za kipuuzi!!
 
Si Bashe ameshupaza shingo
Mkuu kuna mambo ya kufanyia kazi kwa serikali kukomesha hili.
Wale ndugu zetu wamasai wafugaji ambao hawalimi, miaka ya hivi karibuni pakitokea ukame wanahangaika sana kupita nyumba kwa nyumba kuomba vyakula.
Hili la ufugaji halina tija tena kutokana na ukame wa mara kwa mara.
Ni wengi mno mtaani wakiomba chakula
 
Mkuu kuna mambo ya kufanyia kazi kwa serikali kukomesha hili.
Wale ndugu zetu wamasai wafugaji ambao hawalimi, miaka ya hivi karibuni pakitokea ukame wanahangaika sana kupita nyumba kwa nyumba kuomba vyakula.
Hili la ufugaji halina tija tena kutokana na ukame wa mara kwa mara.
Ni wengi mno mtaani wakiomba chakula
Looooh[emoji2815]
 
Acha utoto na maoni ya kijinga

Wamasai wameanza kufuga jana? Unataka kila raia alime itawezekana?

Chakula kisingetoka nje ya nchi wala njaa usingekuwepo
Mkuu kuna mambo ya kufanyia kazi kwa serikali kukomesha hili.
Wale ndugu zetu wamasai wafugaji ambao hawalimi, miaka ya hivi karibuni pakitokea ukame wanahangaika sana kupita nyumba kwa nyumba kuomba vyakula.
Hili la ufugaji halina tija tena kutokana na ukame wa mara kwa mara.
Ni wengi mno mtaani wakiomba chakula
 
Acha utoto na maoni ya kijinga

Wamasai wameanza kufuga jana? Unataka kila raia alime itawezekana?

Chakula kisingetoka nje ya nchi wala njaa usingekuwepo

Mtoto ni wewe usiyekubali uiweli.
Kila mwaka imekuwa ni kawaida wamasai kuzunguka mtaani wanawake na watoto wakiomba chakula.
Hii sio siri na wala siwasingizii
 
Ungeshauri wafuge kisasa ningeheshimu mawazo yako
Mtoto ni wewe usiyekubali uiweli.
Kila mwaka imekuwa ni kawaida wamasai kuzunguka mtaani wanawake na watoto wakiomba chakula.
Hii sio siri na wala siwasingizii
 
Back
Top Bottom