Makusudi wanayofanya wahudumu wa afya kutoa dawa kwa watu wanaotumia bima za afya

Makusudi wanayofanya wahudumu wa afya kutoa dawa kwa watu wanaotumia bima za afya

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
1660137419147.png

Kumekuwa na hii tabia ambayo wahudumu wa afya wanaifanya sana kwa wagonjwa wanaotumia bima za afya. Unakuta mtu anaumwa ugonjwa fulani anaandikiwa dawa ambayo kwa makusudi kabisa wanajua dawa husika haipo kwenye orodha ya dawa kwenye fungu la bima alilopo mgonjwa husika na ni ngumu dawa hiyo kupatikana katika maeneo hayo.

Hivyo mgonjwa analazimika kulipia dawa hizo kutoka mfukoni kwake wakati kulikuwa na machaguo bora mengine ya dawa kuliko ambayo amemuandikia mgonjwa na inapatikana kwenye fungu la dawa zinazopatikana kwenye bima yake, lakini kwakuwa dawa hiyo ni ya gharama kubwa na itawapatia faida basi mgonjwa anaandikiwa dawa ambayo haipo kwenye kifurushi cha bima yake.

Hii inawapa nafasi wahudumu wa afya kijiongezea faida kinyume na utaratibu kwa kuwadhulumu na kuwapa hasara wananchi wanaolipia bima hizi. Waziri Ummy Mwalimu tafadhali liangalie hili ili wananchi wapate huduma wanazostahili kwa wakati na ubora.​
 
Kwann na ww ukubali kulipia kama unajua kuna alternative ya dawa
 
Mhudumu wa afya,anamdhulumuje mteja?
Duka utakaloenda kununua dawa siyo lake,anakudhulumuje tena?
 
Hapo unawalaumu wahudumu wa afya Bure wakati wa kumlaumu ni NHIF ambao wanalipana posho za vikao by bodi na seminar kwa mabilioni huku wakipunguza dawa anazotakiwa mchangiaji Kila uchao.

Hii nchi Kuna raia maiti!
 
Mhudumu wa afya,anamdhulumuje mteja?
Duka utakaloenda kununua dawa siyo lake,anakudhulumuje tena?
Dawa unayoandikiwa siyo rahisi kupatikana kwenye eneo husika, hivyo utanunua tu hapo hapo ulipopewa matibabu.
 
Back
Top Bottom