Malalamiko ya TP MAZEMBE kuelekea mechi na SIMBA SC

Malalamiko ya TP MAZEMBE kuelekea mechi na SIMBA SC

Katika barua pepe iliyotumwa na TP Mazembe kwa CAF, ambayo tovuti ya timu hiyo imeiweka bayana, inasema kuwa:

Uongozi wa TPM umeianisha njia kadhaa ambazo si za kimichezo ambazo Simba SC inawafanyia wapinzani wake pamoja na malalamiko kadhaa kutoka kwa timu zilizocheza Dar es Salaam katika Ligi ya Mabingwa zimefikia CAF.

Nkana, JS Saoura, Al Ahly na hivi karibuni Vita Club, wapinzani wote wa Simba SC walilalamika juu ya kupewa mabasi mabovu yenye harufu ya ajabu; Pia imeelezwa kuwa huwa kuna unyanyasaji kwa timu wakitembelewa na wafuasi wa Simba SC wakati wa mazoezi rasmi katika uwanja na siku ya mechi wakati wa kuwasili kwenye uwanja huo.

Zaidi ya malalamiko haya kwa klabu ya Tanzania, imeidhinishwa kuwa wafuasi wa Simba SC wanajaribu, siku ya mechi, kuzuia timu ya TP MAzemb kuwasili kwenye uwanja kupitia milango/mageti halali na kwamba "harufu ya ajabu" bado iko katika chumba cha kubadilishia nguo cha timu ngeni, harufu chafu siku ya mechi itakuwepo.

Pamoja na timu ya TP Mazembe kuwasili Dar es salaam siku ya Jumatano usiku, TPM imeamua kutoa tahadhari kwa CAF, FECOFA na Shirikisho la Soka la Tanzania juu ya mapungufu haya. Al Ahly, Saoura na Vita Club wanajua kitu fulani: wamepewa viwanja vya kufanyia mazoezi ambavyo ni duni sana.

TPM haikuwa na chaguo bali kuomba kuingilia kati kwa CAF. Uongozi wa Club hiyo umeitaka Simba SC kutoa ushirikiano wa kiwango cha juu ili mechi ya Jumamosi ijayo iweze kuchezwa amani na kwa mujibu wa kanuni za kucheza haki.

View attachment 1063181


Wengine wanatabiri vingine.

 
Mbona wanalialia kwani simba ndio wanajukumu la kuwapa basi,uwanja wa mazoezi na vyumba vya kubadilishia nguo vipo chini ya management ya simba!?
 
simba mkienda lubumbashi mtanyanyasika sana hiyo ni tahadhar wametoa kwa madudu mnayowafanyia timu pinzani
 
Hatutishwi na lawama zao.Tunataka kuwaharibia historia yao kama ambavyo Daudi alivyoharibu historia ya Goliath.
Hatuwezi kukaa kuwaogopa miaka yote safari hii tutawaonyesha ubabe kwa mchina na kongo nako tunaonyesha ubabe.Simba itabaki kuwa juu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahahahaa... perfume ya Chibu wanasema ni madawa ya usingizi ehehee... waje na vifaa vya kubaini hizo dawa...
 
mikia na kupuliza dawa ni chanda na pete


Hofu yangu ni hatua zinazoweza kuchukuliwa na CAF dhidi ya klabu/soka ya Tanzania...CAF huwa hawana haraka kutoa maamuzi...wanaweza wakatoa maamuzi muda na wakati usiotarajia...sina hakika kama soka yetu ina uwakilishi katika vyombo hivyo vya juu...Kama Souara, Al Ahly na Vita wamelalamika basi ni vema tuwe na mkao wa kujihami
 
Back
Top Bottom