Malalamiko ya Upendeleo kwa wasimamizi wa Road Reserve Dar es Salaam

Malalamiko ya Upendeleo kwa wasimamizi wa Road Reserve Dar es Salaam

mzalendoalltz

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2015
Posts
828
Reaction score
709
Wananchi wengi wanalalamika hasa suala la upendeleo wa wazi unaoonyeshwa na wasimamizi wa eneo tengwa la barabara yaani (Road reserve) tunaona serikali inafanya jitahada za kuwaondoa wavamizi sawa ila idara hii imekuwa sugu kwa Rushwa maana kuna watu wengi wapo na hawaondolewi na wamekaa miaka na miaka, wengine tunaondolewa kwa nguvu kubwa na wengine tupo nje lakini wakija kupima wanatupa notice za kubomoa na ukienda wanakudai pesa ili wakusamehe.

Tunamuomba Mh Rais Samia kupitia kwa waziri Mbarawa afanye uchunguzi wa kina. ajiridhishe ili awawajibishe wahusika na zaidi aangalie idara yake pale Tanroads Dar (Meneja Mkoa) eidha anaesamia idara hiyo ndiye anamuangusha kwa kutokuwa makini na usimamizi. Tunawakilisha Kazi iendelee upendeleo wa kirushwa ufutwe kabisa.

Tunachotaka sisi ni haki kama mmesema eneo ni la Serikali bas asitumie mtu yeyote na kama litatumika tupewe hiyo haki wote.
 
Walishambiwa walambe asali wewe unaleta kelele tu

USSR
 
Hakuna mwenye Guts za kuwawajibisha hao watendaji hata mmoja.hii enzi iliishakwenda na sasa ni muda wa kula kwa urefu wa kamba.
 
Mbona ni kama kitendawili, ni vizuri ungetaja eneo maana Dar es Salaam ni kubwa na ina bararbara nyingi.
 
Back
Top Bottom