Malaria kujirudiarudia nini sababu?

Grau

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2017
Posts
4,501
Reaction score
4,226
Habari zenu wakuu,

Mimi huwa ninatatizo la malaria kujirudia rudia kila baada ya miezi miwili au mitatu natumia dawa lakini baada ya miezi mitatu inarudi tena alafu huwa inaambatana na kikohozi kikali sana.

Nikajaribu kukifanyia uchunguzi hiki kikohozi nimepiga mpaka x ray na vipimo vingivingi naambiwa sina ugonjwa wowote.

Nimepima vipimo vingivingi lakini ndio hivyo hasa sijajua kama hiki kikohozi ni effect ya malaria inayojirudia rudia.

Wadau nisaidieni ili niondokane na hii malaria maana inaniathiri sana hata katika shughuli zangu.
 
Maambukizi ya malaria huchukua siku 14 mpaka dalili za ugonjwa jujitokeza, kuna uwezekano mkubwa kuwa unapata maambukizi mapya.

Kula vizuri nyama na mboga za majani pia fanya mazoezi kuimarisha immune system yako
 
Kiukwel hili tatzo lakuugua mara kwa mara ninalo tangu nipo namiaka 7 mpaka sasa ninamiaka 24 linanisumbua tu nikienda kupima naambiwa ni malaria natumia malafin baada ya miez mitatu hivyohivyo tu HIV nimeshapima kabisaaa.
 
Kiukwel hili tatzo lakuugua mara kwa mara ninalo tangu nipo namiaka 7 mpaka sasa ninamiaka 24 linanisumbua tu nikienda kupima naambiwa ni malaria natumia malafin baada ya miez mitatu hivyohivyo tu HIV nimeshapima kabisaaa.
Sio peke yako ndugu, binafsi nasumbuliwa na malaria mara kwa mara yaani kila mwezi ilikuwa ni lazima niingie hospitali, lakini kipindi hiki afadhali, maana mara ya mwisho nilisumbuliwa mwezi mwezi wa nane, dawa nilotumia siijui lakini nilitembeza mkuyenye sana hadi nikawa najihisi kama nimeishiwa nguvu za mwili. Mimi ni group O+ve.
Ushauri wangu kwako, fanya sana mazoezi ya mwili/viungo, walau kila siku usikose kutoka jasho, then kama hupendi kulala na neti basi hakikisha chumbani kwako unapulizia dawa ya kuua mbu, vile vile usisahau kuvaa t shirt ya mikono mirefu kuanzia jioni na soksi pia kama unapenda kukaa maeneo ya nje ya nyumba muda wa jioni.
 
Kweli ndugu mi mwenyewe group langu ni O ±ve lakin ndo ivyo tangu namiaka saba mpaka sasa sijui kwanini kunakipindi nilikuwa napiga mazoezi likaisha kabisaaaa yaan unaweza ambiwa unaukimwi hat maana jamii haichelewi.
 
Kiukwel hili tatzo lakuugua mara kwa mara ninalo tangu nipo namiaka 7 mpaka sasa ninamiaka 24 linanisumbua tu nikienda kupima naambiwa ni malaria natumia malafin baada ya miez mitatu hivyohivyo tu HIV nimeshapima kabisaaa.
Kama group la damu 0+ ni kawaida hakuna cha HIV hapo.
 
mi pia ni group O .....sasa kama ni hivyo kuna issue na group hili kwenye malaria maana kuna kipindi nilipo kuwa shuleni kanda ya ziwa nilikuwa na malaria kila siku hata siku nikihisi nipo poa na nikaenda kupima nakutwa malaria ila nilipo maliza na kurudi home niko tofauti ,sina malaria kama nilipo kuwa shuleni kanda ya ziwa sasa nahisi kuna kitu na group hili la damu na malaria
 
Mimi binafsi last year nmeumwa mara kwa mara lakini ni U.t.i

mm naamini unywaji wa dawa mara kwa mara unashusha Kinga ya Mwili kama wanasayansi wanavosema... kwahiyo kurudiwa na magonjwa ni rahisi zaidi ,hata kuanza magonjwa mengine pia.

nilivyoona hivo ,nikaachabkunywa dawa nikawa nakunywa maji na chakula mara moja moja matunda...
nmekuja kuumwa mwezi november juzi hapa, tena sio homa ni mkojo tu umechange ....nmekaa karibu mwaka sijaumwa na sijanywa dawa yoyote...
 
Kapimwe UKIMWI vizuri.
 
Kweli ndugu mi mwenyewe group langu ni O ±ve lakin ndo ivyo tangu namiaka saba mpaka sasa sijui kwanini kunakipindi nilikuwa napiga mazoezi likaisha kabisaaaa yaan unaweza ambiwa unaukimwi hat maana jamii haichelewi.
Pole sana mkuu,
Katika magonjwa hayanipati wala huwa sihofii ni malaria.
Lakini mbona group langu la damu ni O+v kama wewe!!!

Jaribu hospital mbali mbali.
 
Kweli ndugu mi mwenyewe group langu ni O ±ve lakin ndo ivyo tangu namiaka saba mpaka sasa sijui kwanini kunakipindi nilikuwa napiga mazoezi likaisha kabisaaaa yaan unaweza ambiwa unaukimwi hat maana jamii haichelewi.
Kuna kipindi hiyo ilikuwa mwezi wa 8 unaambiwa niliumwa hadi nikapima vipimo vyotekuanzia hiv, widal, malaria, fbp lakini mwisho wa siku nikaambiwa sina tatizo wajati najiskia naumwa mbaya, kwa akili yangu nilijua HIV [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji23] [emoji23] [emoji124] [emoji125] [emoji125] [emoji377] [emoji377] [emoji377] yaani niliposomewa vipimo nilifikiri utani, hadi nikamuuliza daktari " utani au kweli?"
But nilipotoka hapo nilijifunza kupenda sana kula matunda.
 
Ushauri wangu.Kama una uwezo wa kupata mzambarau chukua Yale magamb yake Au magombe make sure yasiwe yamekomaa Sana chukua.then safisha kw maji kuondoa uchafu wa juu juu kana then yachemshe Vizur.acha maj ya poa then Wek katka glass Kama nusu Lita unywe atlst kwa week moja.malaria utaiskia katika redio.navyokwambia nalala bila net takriban miaka nane sasa .na malaria ccjui.
 
Mkuu inaonekana wewe hutaki kuwa Rubani.
 
Pole sana mkuu,
Katika magonjwa hayanipati wala huwa sihofii ni malaria.
Lakini mbona group langu la damu ni O+v kama wewe!!!

Jaribu hospital mbali mbali.
Nimejaribu hospitali zaid ya tatu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…