Elections 2010 Malecela aangukia pua kwa mara nyingine...

Elections 2010 Malecela aangukia pua kwa mara nyingine...

Mazee kama wabunge wenyewe ndio type hizi tunazoziona hapa (CHADEMA Regia Mtema, CCM Hamis Kigwangala ) basi tumekwisha.

Hamna CHADEMA wala CCM, kwa mtaji huu wote waganga njaa tu.
Huyu ni yule daktari wa binadamu aliyeutosa udaktari na kuchangamkia ulanguzi wa pamba. Niliwahi kuhoji digrii zake hapa maana niliona kama zina utata, lakini baada ya uchunguzi nikagundua ni kweli alihitimu udaktari pale Muhimbili. Zaidi ya hiyo digrii ya udaktari, ana digrii nyingine mbili za magirini ambazo kazipatia oline kwenye vile vyuo feki maarufu kama 'degree mills'. Katika uchunguzi wangu niligundua mengine mawili:

Kwanza, ndiye aliyekuwa kiongozi wa ule mgomo maarufu wa madaktari Muhimbili ambapo walialika bendi ya matarumbeta kuwaburudisha wagomaji wakati wagonjwa wakiendelea kufa kwa kukosa tiba. Baada ya hapo, baraza la madaktari lilimwekea sanctions kwa kitendo hicho cha kukiuka maadili ya kitaaluma, amefutiwa usajili kwa hiyo haruhusiwi kufanya kazi ya tiba popote duniani, na ndiyo maana amejikita kwenye biashara ya pamba.

La pili nililogundua ni kwamba huyu ni mmojawapo wa vibaraka wa Rostam Aziz, na pesa yote aliyotumia kwenye kampeni ni ya Rostam kwa lengo la kumuadhibu Lucas Selelii. Ndiyo maana Selelii hajateuliwa licha ya kushika nafasi ya pili, wakamchukua huyu wa nafasi ya tatu!
 
Ila hii ya Dr HAMIS NAONA MBELEKO YA WAZI KABISA!! Kweli NEC kuna maamuzi ya Ajabu..

...jamani sasa si mnajuwa kuwa huyu kijana ni mtu wa karibu kwenye taasisi ya kutembeza bakuli....ya MAMA????
afteral huyu selelii sio mwenzetu na ameshatupiga mkwara kuwa anaenda CHADEMA ....wote wanaoenda CHADEMA tutawapiga chini????
 
Huyu ni yule daktari wa binadamu aliyeutosa udaktari na kuchangamkia ulanguzi wa pamba. Niliwahi kuhoji digrii zake hapa maana niliona kama zina utata, lakini baada ya uchunguzi nikagundua ni kweli alihitimu udaktari pale Muhimbili. Zaidi ya hiyo digrii ya udaktari, ana digrii nyingine mbili za magirini ambazo kazipatia oline kwenye vile vyuo feki maarufu kama 'degree mills'. Katika uchunguzi wangu niligundua mengine mawili:

Kwanza, ndiye aliyekuwa kiongozi wa ule mgomo maarufu wa madaktari Muhimbili ambapo walialika bendi ya matarumbeta kuwaburudisha wagomaji wakati wagonjwa wakiendelea kufa kwa kukosa tiba. Baada ya hapo, baraza la madaktari lilimwekea sanctions kwa kitendo hicho cha kukiuka maadili ya kitaaluma, amefutiwa usajili kwa hiyo haruhusiwi kufanya kazi ya tiba popote duniani, na ndiyo maana amejikita kwenye biashara ya pamba.

La pili nililogundua ni kwamba huyu ni mmojawapo wa vibaraka wa Rostam Aziz, na pesa yote aliyotumia kwenye kampeni ni ya Rostam kwa lengo la kumuadhibu Lucas Selelii. Ndiyo maana Selelii hajateuliwa licha ya kushika nafasi ya pili, wakamchukua huyu wa nafasi ya tatu!
kwanza nashukuru kwa uchambuzi makini, pili naona uteuzi wake ni zaidi ya vile tunavyo ona na macho yetu ya kawaida.
kwa sababu haruhusiwi kugfanya tiba ya uganga, wameona ngoja tumeokoe ndugu yetu, unajua wanyamwezi wana nasaba na wazaramo
 
Hiki chama cha mafisadi ama kweli hakina mwelekeo, itakuaje umuengue Mwakalebele kwa shutuma za kutoa rushwa na hata bado hajafikishwa mahakamani halafu in the same breath ukawapitisha [Mramba na Chenge] watu waliofikishwa mahakamani kwa shutuma za rushwa babu kubwa[ MEGA_ CORRUPTION]!! Double standard ya namna hii haijawahi kutokea.Hii lack of consistency itakiyumbisha sana hiki chama.

Kweli CCM inachekesha kweli, hii ni double standard......Mwakalebela hajafikishwa mahakamani, lakini leo hii unamrudisha Mramba, Chenge na hata Rage ambaye alitoka jela kwa msamaha wa JK. Kwa ninavyooelewa, Rage hajawahi kusafishwa au kuondolewa yale mashtka na mahakama yoyote nchini na wala sina hakika kama alishawahi kutafuta njia za kisheria kuondoa yale makosa yaliyomfanya aende jela.
Anyway, that's what they call SISIEMU.
 
Sahihisho kwa Bulesi;

Mheshimiwa Andrew Chenge HAJAWAHI kufikishwa mahakamani kwa kosa lolote linalohusiana na rushwa;kesi yake iliyopo kwenye mahakama moja ya Jijini Dar inahusiana kuendesha gari vibaya na hivyo kusababisha vifo,anashtakiwa pia kwa kosa la kuendesha gari bila kuwa na BIMA!

Ni kawaida kwa binadamu kusahahu!

Chama makini kinajali hisia za wanachama wake na jamii kwa jumla, sawa hajafikishwa mahakamani lakini mbele ya jamii huyu bwana ANANUKA; kwahiyo katika nchi yenye viongozi makini a' la enzi ya mwalimu na leo hii Rwanda ya Kagame huyu bwana angekuwa ananyea ndoo wacha kugombea nafasi ya kuteuliwa!! Nimekusoma kuwa umeshinda kura za huko kwenu usokile, Hongera; nadhani sasa mtakuwa wastaarabu ngwe ijayo mtaacha kugombana wenyewe kwa wenyewe na kuacha wivu wenu wa kijinga kwa kila mmoja wenu kujifanya Malafyale!!
 
Back
Top Bottom