LOTH HEMA
JF-Expert Member
- Dec 6, 2015
- 18,611
- 27,615
Hivi serikali ilishawahi kujiuliza maswali ya kielimu kuhusu raia wake wengi wanaohitimu ngazi mbalimbali za elimu huwa wanaishia wapi ikiwa lengo la kusoma ni kufaulu mtihani na kuajiriwa? Ianzie na hao wanaofeli wanaishia wapi? Au inafikiri ndio hawa bodaboda, wamachinga na wengine wengi wa aina hii? Serikali ina mkakati gani kuboresha stadi za kazi kwa raia ambao si wanafunzi wa vyuo na shule? Au wakimaliza ngazi za elimu wao huchukua wafanyakazi wake na hao wanaobaki wapotelee kusikojulikana wakitafuta maisha bora? Elimu haina serikali inatakiwa iwe na mipango na programu nyingi za kukuza na kuendeleza stadi za kazi kwa raia wake nje na mfumo rasmi wa elimu