Mshobaa
JF-Expert Member
- Apr 7, 2013
- 1,714
- 677
Wakuu salaam
Kumekua na tabia ya madereva wa malori kuegesha magari yao sio pembezoni bali katikati ya hii barabara muhimu kuanzia eneo la urafiki hadi ubungo darajani. hali hii imekua kero kubwa sana kwa watumiaji wa barabara hii, kwani husababisha foleni kubwa hasa wakati wa jioni kwani hulazimika kutumika njia moja na muda huo matumizi yanakua makubwa.
Naomba wahusika waliangalie hili kwa uzito wake kama ni kuwashushia mizigo yao waharakishe ili kuondokana na kadhia hii,, kwenu Tanroads tz, Halmashauri ya manispaa ya Ubungo, nawaomba mkae chini na na hawa wamiliki wa malori ili kuwe na utaratibu mzuri wa kupaki bila kuadhiri shughuli nyingine au muwatengee eneo la kupaki wakati wakisubiri kushusha mizigo yao..
Kumekua na tabia ya madereva wa malori kuegesha magari yao sio pembezoni bali katikati ya hii barabara muhimu kuanzia eneo la urafiki hadi ubungo darajani. hali hii imekua kero kubwa sana kwa watumiaji wa barabara hii, kwani husababisha foleni kubwa hasa wakati wa jioni kwani hulazimika kutumika njia moja na muda huo matumizi yanakua makubwa.
Naomba wahusika waliangalie hili kwa uzito wake kama ni kuwashushia mizigo yao waharakishe ili kuondokana na kadhia hii,, kwenu Tanroads tz, Halmashauri ya manispaa ya Ubungo, nawaomba mkae chini na na hawa wamiliki wa malori ili kuwe na utaratibu mzuri wa kupaki bila kuadhiri shughuli nyingine au muwatengee eneo la kupaki wakati wakisubiri kushusha mizigo yao..