Mama hamtaki Mpenzi wangu

Mama hamtaki Mpenzi wangu

Hata mimi nisingekuozesha yaani mwanaume an a kunywa pombe, bangi ,sigara mie hapana wanakuaga malaya mno

Afu pia wewe umeishia olevel na yeye olevel watoto wenu nani atawafundisha? Tafta hata mkaka mwenye diploma mtoto enu awe inspired kusoma kwa bidii

Usitangulize hisia mbelembele
Walevi wanakuwa siyo Malaya.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Umesema mama hamtaki mpenzi wangu ,ushasema mpenz ni wako ila mama hamtaki ,hauoni apo mama anamtaka mpenz ambaye ata kuwa wake na wako kwa sababu huyo wako tu yeye hamtaki????
 
ni
Habari za saa hii wana Jf

Naomba msaada wenu wa mawazo juu ya swala hili, kama kichwa cha habari kinavyojieleza;
kwa miezi mi3 hii nmekua na mahusiano ya kimapenzi na kijana karibu na maeneo ninayoishi,
  • Mimi binti wa 28 yrs Mpenzi ana 38 aliwahi kuishi na mwanamke kwa miaka kadhaa zamani akaachana na mwanamke wake baada ya kuachishwa kazi ( kampuni ilifilisika)
  • Kwasasa ana biashara zake
-Wote tumeishia 0- level kielimu
-Anataka kunioa pale nikiridhia

Sasa tatizo linaanza baada ya mama kuhisi uhusiano baina yetu, anasema kijana hafai kwanza
-Ana vuta bangi/pombe
-Hajui kuvaa sio mtanashati
- Aliwahi kuishi na mwanamke
-Anatoka familia ya kawaida kama yetu kwahiyo hafai hatanisaidia chochote
- Hana mvuto mbele za watu
-Hana Cv nzuri hata nikimtambulisha
- Anahisi kaniroga ndo mana nmekua nae kimahusiano
-Kwanza anakaa maeneo ya karibu na nyumbani
-Hana hadhi ya kuwa na mimi

Sababu ni nyingi!!

Kwa kuliona hilo tukaamua basi ahame makazi tayari kashahama, mazingira yote tumeyafanya yawe mapya,kwa kila kitu cha hadhu anayoitaka mama,nmeshambadilisha huo muonekano kwa kiasi chake ili afanane na anavyotaka mama ila naona pamoja na kutaka aridhike ila kila siku anaanzisha sababu mpya ya kumkataa anasema anajitutumua tu ili anipate na pombe ameacha anipate akishanioa ntapata shida mana atarudi kwenye mambo yake yote!! Pia namdhalilisha kwa wamama wenzie kwa kuwa na mahusiano na jamaa

- Mama anasema yuko tayari kwenda kwa mganga yoyote akavunje mahusiano mana kwanza jamaa atakua kaniroga sio kawaida.

Sasa hapo nifanyaje wakuu? Maana naona nachanganyikiwa kila siku anaanzisha jambo jipya! ilihali nmemwambia mimi mwenyewe sijasoma! Kazi sina wala bishara yoyote na kijana wa watu ameridhia ana fanya kila jukumu lake bila kinyongo ila mama anasema anafanya mana hana hadhi ya kuwa na ww ndo mana inabidi afanye tu...

Kinachoniumiza ni hakuna siku amewahi niuliza changamoto za maisha yangu ya mahusiano. nmejaribu kumwambia wachumba wakija wakijua sijasoma/sina kazi wanagairi haelewi.. anasema umerogwa wewe
nikiomba space nitulize kichwa sipewi naambiwa mpaka utanielewa...

Nimepata feeling mama yangu ni Toxic /narcissistic mom ila nikieleza hisia zangu yeye ana cheka ndo ananiona kama mpuuzi..

Maana mimi nmemwambia kwanini tusimwachie Mungu tu kama Mungu hajapanga tutaachana tu ila kwa ridhaa yetu mengine tutarekebishana sitaki uwe kama unanipangia maisha ila haelewi kabisa , niko njia panda maana maisha nayaona machungu kabisa ni mimi ndo tatizo au mama? Nishaurini wakubwa kabla sijashuka presha nikazimika mana bi mkubwa kasema kama ntakufa nife mana ndo ilivyopangwa.
tumie namba yake niseme nae
 
Kama kuna kitu kitakachokuokoa apo ni kuingia kwenye dini yako mazima hakikisha unasali unabadilisha mwonekano wako kua muumini wa kweli usikubali mambo ya machafu ndani ya ndoa yako pia marafiki, tabia and etc, hata mambo ya ujana punguza au acha kabisa na hakikisha mume naye anaacha pia, jiunge kwenye magroup ya dini and etc alafu mwambie na uyo mchumba wako atubu na mfatane wote kwenye njia ya dini na mungu atawabarik mtatafta maisha polepole na mtapata amani ila kwa ivo ulivosema msipokua watu wa dini kuna uwezekano siku za mbeleni mkaja kupata shida sana.

Kumbuka ili historia ya mtu ibadirike kabisa inabid yankute ajute na achukie kabisa alikokua ila sio kubadirika kwa kua tu kakuona wewe ilikua ni vyema akabadirika bila hata uwepo wako yani sababu isiwe kisa wewe iyo ni WEAK REASON kumbuka alishawahi kua na mwanamke na wakaachana na wewe age yako siyo yakujaribu maisha unatakiwa uingie kwenye ndoa ukiwa unatambua unachokifanya usichukulie maskhara maana effects utazopata ndani yandoa kwa sasa zinaweza determine maisha yako yote yatayofata yatakua vipi mf MIMBA, MAGOJWA, SIFA MBAYA, ANGUKO, MUDA, UZEE. Ila kwa mwanaume ye vyakupoteza ni vichache kuliko upande wako.

KUMBUKA ANAVYOKUONESHA MAPENZI SAIVI HAITOKUA IVO MIAKA YOTE KWENYE NDOA YENU, usije ukawaza kwenye ndoa ndo mambo yatakua ivo ivo NO.

Dini itawasaidia sana kuwaongoza mtapokua mnakwazana na kukosana na mtapokua chini kimaisha haitowapa shida maana mtakua na amani na imani mungu ndo alieyetenda na ndo atawatoa kwenye ayo matatzo.

Byee.
niko WAWATA
lakini pia nmemwambia hiki kitu badilika kwa sababu umeamua kubadilika sio kisa mimi, maana mimi leo nipo kesho sipo utarudia njia zako
ila ukibadilika kwasababu umeamua kubadilika itakujenga kimsingi hii namwimbia daily na namwambia ibada ibada ibada yani hakuna mawaidha simpi kwakweli.
.Yeye anasema lazima kwenye maisha angebadilika tu na mabadiliko ndo haya kwahiyo atapambana abadilike moja kwa moja
 
Aiseh!
Sema mama ako anaonekana ana matarajio makubwa sana juu yako
Mnooo
yani kuna nambo alipanga kwangu sasa kuwa na huyu kunamfanya aone matarajio yanakufa kisa mtu mmoja... inamuumiza
japo nmemwambia uliowataka sijapata na hawana mapenzi kama haya
 
niko WAWATA
lakini pia nmemwambia hiki kitu badilika kwa sababu umeamua kubadilika sio kisa mimi, maana mimi leo nipo kesho sipo utarudia njia zako
ila ukibadilika kwasababu umeamua kubadilika itakujenga kimsingi hii namwimbia daily na namwambia ibada ibada ibada yani hakuna mawaidha simpi kwakweli.
.Yeye anasema lazima kwenye maisha angebadilika tu na mabadiliko ndo haya kwahiyo atapambana abadilike moja kwa moja

Okey mungu awatangulie.
 
Je ni kweli?

Katika maisha cha kuangalia ni 'Mindset' ya mhusika.

Je ana uwezo wa kuwa na familia?, Je ana uwezo wa kuhudumia familia?, Haya ni baadhi ya maswala ya msingi.

Na sio eti "mavazi" , "Mtanashati"

Ye wewe mtazamo wako ni upi?

Je unaelewa maana ya "materialistic"
Mindset yake ndio naitaka na nmeona inafaa tunamatch hatutasumbuana sana japo yeye kidogo msahaulifu huwa ni wakukumbushwa ila ukikumbusha ni mtekelezaji mzuri pia ana mipango na anajua majukumu yake safi.
utanashati sio tatizo kwangu kabisa.
Materialistic hizo anataka mama
 
Narcissistic mom/toxic mom!!O level!!nani Kama Mama?
 
Na wanawake wa humu wengi wao status za mahusiano yao ni za hovyo mnoo. Inawezekana wanamuonea wivu tu mwenzao. Princess Ariana wewe kama vipi endelea na mshikaji tu kama yatakuja kutokea yasiyo tarajiwa mbele ya safari basi utajiandaa kukabiliana nayo. Dunia hii ina

kutokea yasiyo tarajiwa mbele ya safari basi utajiandaa kukabiliana nayo tu, Kimsingi
ni kweli na ndo mana mm sijasema nna matarajio makubwa au hatabadilika.
ni hizi ramli za watu wa humu mpaka nashangaa hivi watu hawawezi kuwa positive muda wote ni negativity tu
Yakitokea ni mipango ya Mungu na kwasababu nmechukua tahadhari basi ntajitahidi yasiwe makubwa
 
Hapo ndiyo walipotufikisha mama zetu wa zama hizi,
KUWA MAKINI USHAFIKISHA MIAKA 28 HAPO JUA LISHAANZA KUZAMA UKICHEZA ZAIDI YA HAPO JIANDAE KUWA SINGO MAMA,,,

KAMA ANATAKA MWENYE PESA YEYE BABA YAKO ALIMKUTA ANAZO?

TUNAISHI ZAMA NGUMU SANA
 
Back
Top Bottom