the guardian 17
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 395
- 570
Mjane wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Mama Maria Nyerere, amekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuendelea kutimiza wajibu wake wa kuzisimamia Serikali zake zote mbili ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa na uwezo wa kujitegemea, hasa katika kujilisha.
Mama Maria ameyasema hayo alipokutana na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dk Emmanuel Nchimbi, aliyefika nyumbani kwa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, Msasani, jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kumjulia hali, leo Alhamisi, Februari 20, 2025.
“Naomba tu muendelee kusimamia sera ya msingi ya CCM kuhusu kujitegemea… Uhuru wa taifa unakamilika zaidi pale taifa linapojitegemea, hasa katika kujilisha na kuwa na chakula. CCM isiache wajibu wake wa kuzisimamia Serikali zake zote mbili ili nchi yetu iendelee kujitegemea,” amesema Mama Maria.
Source: Mwananchi
Soma pia: - Pre GE2025 - Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Mama Maria ameyasema hayo alipokutana na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dk Emmanuel Nchimbi, aliyefika nyumbani kwa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, Msasani, jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kumjulia hali, leo Alhamisi, Februari 20, 2025.
“Naomba tu muendelee kusimamia sera ya msingi ya CCM kuhusu kujitegemea… Uhuru wa taifa unakamilika zaidi pale taifa linapojitegemea, hasa katika kujilisha na kuwa na chakula. CCM isiache wajibu wake wa kuzisimamia Serikali zake zote mbili ili nchi yetu iendelee kujitegemea,” amesema Mama Maria.
Source: Mwananchi
Soma pia: - Pre GE2025 - Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025