Mama mkwe ana mwezi hana dalili ya kuondoka, chumba kimoja, nimemmisi mume wangu

Mama mkwe ana mwezi hana dalili ya kuondoka, chumba kimoja, nimemmisi mume wangu

Siyo kosa la mama mkwe. Ni kosa la hao wanandoa. Hivi mwanaume mzima unaoa alafu unaenda kujibanza kwenye chumba kimoja? Hakuna cha binti wa kazi wala dharura ikitokea akaja mgeni muhimu hakuna pa kumweka? Hainiingii akilini. Namsifu rafiki yangu fulani alikuwa amepanga chumba kimoja, alipokaribia kuoa alifanya kila aliwezalo kuondoka hapo, alinifuata kuomba ushauri, nikamwambia aamue either akapange sehemu nyingine apate vyumba viwili au kama ana ubavu afanye finishing ya nyumba yake haraka, kweli jamaa akajilipua na mkopo benki. Mara baada ya kuoa ndani ya mwezi mmoja alihamia kwake. Huo ndo uanaume, siyo kuvaa suruali tuu.
 
yaani hayo ni maajabu kwakweli.........

usikute hata wameshamtafutia mwanamke mwingine na wanampango amuache huyu wamuozeshe huyo mwingine........

usione binadamu anakuchekea, wakati mwingine inakuwa usoni tu ila moyoni ni majanga.
Mkuu mambo vipi/ kesho uta kua wapi? nimekumiss sana. Kesho inabidi tukacheze dats
 
Pole sana dada yangu ila huyo mama hana aibu kwani alitakiwa kusoma mazingira kama yana ruhusu au ra! Au yaweza kuwa anafanya makusudi ila ushauri wangu huyo dada aongee na mume wake kuhusu hilo suala aone atamjibu nini.
 
Ushauri wangu ni ajaribu kushirikisha wazee waliomzidi umri ili wamwambie aondoke na ni tabia gani hiyo..ila ipo sana amekomaa hapo na anaona chumba ndio hicho hicho..tabia mbaya sana hiyo..
 
Mmmh........hapo pagumu. Aongee na mumewe watafute nyumba yenye vyumba kama vitatu hivi ili kuweza ku-accomodate wageni kama hao.

Tatizo lipo kwa uyo mama, utaendaje kulala wakat unajua mwanao ana mke halafu chumba ni kimoja tena ni cha kupanga?
 
Kuna vipengele vingi vya kuangalia kabla hujachukua hatua ,1. Huyo ni Mkwewe . Kama Mamake Mumewe ni Mama yako . Heshima iwepo .2. Inaweza kuwa yeye anashida zake yakumfanya akae pale , shida zake binafsi au jumla .3.Ilikuwa afanye maarifa mumewe asiende kwengine . Mgeshauriana mkae vipi nyumba moja lakini mka pamoja .Awasiliane na mumewe kuhusu Shida inayopatikana katika Nyumba asipokuwa Mwanaume . Itakuwa kama nyumba haina mwongozo .Vizuri zaidi kuwa karibu na mama , jadiliana nae kuhusu swala la mwanawe kuacha nyumba , Mkwewe na Mke waweza Kulala chumbani mumewe alale sebulini . Kama ni matatizo ya budget .Lakini kama uwezo anao akodi vyumba viwili hata vidogo vya kumstiri huyo Mama .Kuna uwezekano kuwa huyo Mama anaona aibu lakini kuna kitu kinamlazimu kukaa kwa mwanawe 1. Baba Mkwe amefarika , hana mtu wa kukaanae hapo kwake [Mkwewe] .2. Matatizo yasiyowezekana kufunua mbele ya mwanawe.Kosa ni ya Mumewe kuenda kwa marafiki zake . Kama bado mapema amwite nyumbani waongee wajadiliane baina mume na mke .
 
Ndo maana niliuliza kabila. Hao jamaa wenye tochi kwenye paji la uso ni wa kuogopwa.
 
Ushauri wangu ni ajaribu kushirikisha wazee waliomzidi umri ili wamwambie aondoke na ni tabia gani hiyo..ila ipo sana amekomaa hapo na anaona chumba ndio hicho hicho..tabia mbaya sana hiyo..

MGENI HUWA HAFUKUZWI. Wakati mwanaume anaoa hakutafakari kama familia inaonngezeka, huwwezi kuoa halafu usiwe na chumba cha dharura wakati unapokaa masaa 6 tu kutoka kwenu lazima utembelewe. Bora angeekuwa anaishi pembezoni kama Kwangu MUSOMA au kule KIGOMA. Maana mpaka mtu aje KUKUSALIMIA KAZAMIRIA.
 
Wewe komaa nae tena uzidishe upendo wahali ya juu huenda ikawa ndio wanakupima
 
namshauri huyo mume asimwambie chochote mama mkwe wake, ila wakati wa kwenda kuoga avue nguo zote na apite mbele yake akiwa kama amezaliwa, afanye hivyo kila siku bila kuongea chochote wala kumkasirikia mtu then atapata matokeo mazuri tu


Huyu ni mama wa mwanaume hivyo hawezi kuvua nguo mbele ya mama mzazi au mimi ndo sijaelewa?
 
Sijui umenielewa au ni umefanya generalization!!

...I see, nimeshangaa hadi mdomo umebaki wazi!! Mnatamani mama zetu wawe six feet under kisa hamtaki kero zao? Oooh my goodness, wasingekuwa hao mama zetu tungeonana? Kweli baadhi ya wanawake ni vitumbua.
 
dah kuna mitihani mingine kama hiyo inahitaji ujasiri. sasa hapo tunaona mwanaume anashindwa kuongea na mama yake mzazi. mkewe anahamu na mumewe, ila anashindwa kuongea sabu hataki kuonekana mbaya. inahitajika hekima kidogo kutatua hii ili asipatikane wa kulalamika
 
Pagumu sana hapo,dah vitu vingine bhana mtu unajishtukia mwenyewe,ina maana huyo maana hata hajishtukii!

Wewew shida yako ni nini,au shemejio maswala ya porosoo shida,siwaende lodge wakapigane para tu manake naona kama kama mdogo wako midadi imempanda
 
Hahahahaahaha....sasa kwani waliojenga guest houses, motels na lodges walijenga za kazi gani? Mwambie uyo bibie alalamike nyege, they get a room, burudaaan! Iyo ni short term solution lakini.....
 
Back
Top Bottom