Mama mwenye umri mkubwa zaidi duniani amefariki akiwaacha mapacha wake wa miaka 3 wakiwa yatima

Mama mwenye umri mkubwa zaidi duniani amefariki akiwaacha mapacha wake wa miaka 3 wakiwa yatima

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
1661893017689.png

1661893718107.png

Maria alifanya utaratibu wa kupandikiza mbegu ili apate watoto (IVF) akiwa na umri wa miaka 67. Aliingia kwenye kitabu cha Guineas Book of Records kwa kuwa mama aliyepata watoto akiwa na umri mkubwa zaidi.

Maria alipunguza umri wake kwa miaka 12 wakati akipata matibabu yake. Madaktari walimuuliza kama yuko kwenye ndoa na aliwajibu kuwa kuolewa na kuoa ni hiari ya mtu.

Maria alijifungua watoto mapacha wakiume Christian na Paul na aliwalea mpaka alipogundulika na saratani. Watoto wamerithiwa na mdogo wake ambae hana mtoto. Mdogo wake amemuahidi Maria atawalea watoto na kuwaeleza ukweli kuwa mama yao alifariki na alihatarisha maisha yake ili awape uhai.

Mama yake Maria alifariki akiwa na miaka 100 na Maria alikua na matumaini ya kuishi na kufika umri huu.
 
nafsi yangu imejaa maneno mengi kiasi kuwa nashindwa kuandika!
wakati wengine wakipata misiba kwa kukusudia ya watoto wao lakini wengine wakipambana kuhakikisha wengine wakizaliwa RIP MARIA
 
Back
Top Bottom