hahahahahah lol<br />
Sis kweli leo umeniacha hoi<br />
mie tangu jana nacheka tu daahh<br />
umenikumbusha sabena jinsi watu tulivyokuwa tuna banana<br />
Basi limesheena ile mabaya lakini utasikia kondactor anasema <br />
"panda mama basi sio ndoo ya maji halijai hili " Dereva ndo kauchuna....<br />
Zile ngozi za kimang'ati zinanuka, huyu anatapika mtoto kajinyea daaaahh<br />
mmhhhh Sintokaa nisahau sabena ukitaka kutapika unapita watu kama kumi hivi<br />
kufika dirishani kilicho kuwa kinaniudhi kuliko chote ni pale mtu anakula karanga na fanta<br />
dahhh kilicho fuatia tuache tu ... halafu sasa hiyo barabara basi lina linaenda juu chini, juu , chini <br />
ukifika uendako unahisi kama ulikuwa unapalilia heka 10 za mahindi , nguvu zimeisha ajili ya kutapika...