Mama Salma Kikwete anusurika kupata ajali mkoani Mara

Mama Salma Kikwete anusurika kupata ajali mkoani Mara

Pole Mama Salma, mungu atakulinda na majanga yote.

"Ila cha kujifunza hapa ni kwamba maisha ya binadamu yoyote yule ni muhimu kuyalinda bila kujali nafasi yake kwani hilo ni Jukumu mama la serikali yoyote kuhakikisha usalama wa Raia wake, Matukio kama haya yapo mengi sana kila siku nchi nzima, daladala kuchomekeana wao kwa wao pamoja kuchomekea magari mengine, barabara mbovu, madereva wanapata leseni kwa rushwa badala ya qualifications" - Umefika wakati sasa kuwalinda Raia wote na ajali zinazoweza kuzuilika, Nina hakika kama vyombo vya habari vingekuwa vinatangaza matukio yote ya aina hii ya msafara wa FL basi 24hour hazitoshi. Law enforcement agents waache longolongo na Rushwa wafanye Kazi yao"

Well said. Hizi tunaziita "near miss". So hizi near miss kama ulivyosema zinatokea kila siku....isiwe tu an issue kwa viongozi au mamsapu wao.
 
Hivi ni mama Ridh ee?
..Ukipenda muite mama Halfan au Mama Rashid kama humtaki ridh...ingawa kweli sio mamaye wa damu.

Imagine kwa Zuma...five of them...inabidi siku nzima ukae kwenye foleni...luckily ni south africa miundombinu si haba

Dah! sipati picha hapo kwa JZ..ila nadhan watakuwa wanaratiba za matembezi si kila kukicha kiguu na njia.May b first lady yule aliyekuwa nae Juzi juzi kwa Gordon Brown ndo anakula vizuri bata na Prezida!
Pole yake mama wa Kwanza
 
Pole mama Salma. Lakini wanausalama wake wanapaswa kuwa makini zaidi inakuwaje lori lenye magendo linakaidi amri lilitakiwa liwe limewekwa pembeni mapema by any means
kuna cha kujifunza hapo!!. unakumbuka Late Sokoine aligongwa na Damisan Dube!!!!!Mwinyi alipigwa kelebu na mtu mmoja kwenye mkutano!!!na mengine mengi ya ndani na nje ya nchi.Wanausalama wanatakiwa kuwa makini zaidi ya walivyojifunza.
 
Simuombei mabaya ila lingegonga walau kidogo gari ya mama japo viongozi wetu wangeamka maana raia wa kawaida wanapoteza sna uhai!!!
 
Kwani naye amekuwa kiongozi wa serikali mpaka apewe uongozi wa traffick hizo taratibu zinazokiukwa kumfanya mke wa Raisi naye Raisi zingemponza manake angejikuta anagongwa na kuumia,vipi anapita mikoani anatowa maagizo utafikiri waziri au Raisi aw Waziri Mkuu,kama yeye anaangalia hali ya hewa ya chama chake na mumewe anavyokubalika asipotezee watu wengine muda wakujitafutia Riziki zao.
 
Ndo ivyo mie kimeniuma ile ya Kibamba kuna watoto wameachwa Yatima ndugu unajua uchungu wake!!!
 
Kwani naye amekuwa kiongozi wa serikali mpaka apewe uongozi wa traffick hizo taratibu zinazokiukwa kumfanya mke wa Raisi naye Raisi zingemponza manake angejikuta anagongwa na kuumia,vipi anapita mikoani anatowa maagizo utafikiri waziri au Raisi aw Waziri Mkuu,kama yeye anaangalia hali ya hewa ya chama chake na mumewe anavyokubalika asipotezee watu wengine muda wakujitafutia Riziki zao.
anapewa ulinzi kama FL1 wa nchi ...na si vibaya
 
anapewa ulinzi kama FL1 wa nchi ...na si vibaya

Sijuwi unamtetea kwa kuwa wewe pia ni FL au? Ni kweli anahitaji ulinzi lakini ulinzi huo usimaanishe kuwachelewesha watu waendeao kazini au akina mama wanaoenda kujifungia eti kisa wako kwenye foleni wanasubiri FL anapita kwenda saloon kinondoni. This is ridiculous jamani lets get serious japo kdg.

Halafu me sielewei hivi huyu mama kwenye structure ya serikali anafall wapi? Maana I'm sure pesa nyingi sana ya serikali inatumika kwa ajili ya mambo yake binafsi. Yes WAMA ni NGO taasisi binafsi kama zilivyo zingine. Sasa yeye akienda huko mikoani hiyo misafara yote ya askari na viongozi wengine mafuta per diems na mengineyo nani analipia kama sio kodi zetu? Jamani tukemeeni huu upuuzi ili ustop mara moja. It wont help tukijakusema wakishatoka madarakani. Nalinganisha hili na kitendo cha kufanyia vikao vya kamati kuu ya CCM ikulu jamani nani amewapa hicho kibali? Wanalipia huo ukumbi au? Dont they know kwamba hiyo ikulu ni watz wote wenye vyama na wasio navyo? We are tired of this jamani acheni kutunyanyasa kiasi hicho?
 
Kule kwenye saiti yangu niliandika hivi tarehe 26 na bado naamini tutakuwa na ajali kubwa ya kiongozi fulani.. isipokuwa kama tutawakinga kwa maombi:

kuanzia leo (March 26) kuelekea mwezi wa nne, tuwaombee viongozi wetu hasa wale wanaopanga kugombea nafasi mbalimbali. Tusije tukapata mshtuko wa kupoteza mtu maarufu au mwanasiasa maarufu katika ajali hasa ndani ya wiki hizi zinazokuja hadi mwishoni mwa mwezi wa nne. Tumpigie Baba magoti atuepushe na mshtuko wa kitaifa kwani machozi yamedondoka.
 
Kule kwenye saiti yangu niliandika hivi tarehe 26 na bado naamini tutakuwa na ajali kubwa ya kiongozi fulani.. isipokuwa kama tutawakinga kwa maombi:

Dr. Slaa chunga sana safari zako tafadhali. we still need you
 
Kule kwenye saiti yangu niliandika hivi tarehe 26 na bado naamini tutakuwa na ajali kubwa ya kiongozi fulani.. isipokuwa kama tutawakinga kwa maombi:

mhhh MK umejuaje? alafu kiongozi fulani.. does that mean unamjua ni kiongozi yupi? na kwamba hiyo ajali haitakuwa ajali ya kawaida? kuna uwezokano wowote wa kuepusha hiyo ajali? je uyo kiongozi fulani hawezi kutonywa awe careful?
 
Pole mama rais alikuwa taarime?Taarime kwa magendo mpaka wanataka kumgonga mke wa mkulu.Na Jukwaaa lililo tengenezwa kwa ajiri ya kuhutubia hawa wababe wa taarime wamelivunja...habari ambazo sio rasmi walikuwa wanataka ahutubie...wamzomee...lakini hao askari walivyo wengi naona na ubabe wao wameogopa..Kipigo.

hivi kuna wilaya mpya (ya taarime) imeanzishwa Tanzania?
 
Back
Top Bottom