Mama Samia ni Kiongozi Mnyenyekevu sana kwa Wananchi, Wanasiasa wengine tujifunze

Master Legendary

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2013
Posts
576
Reaction score
876
Wanabodi sijui ni mimi peke yangu au na nyie mnaona, huyu Mama toka ametwaa madaraka amekuwa Kiongozi Mnyenyekevu sana kwa Wananchi wake.

Hotuba ya Mei Mosi imejaa unyenyekevu wa hali ya juu sana kiasi cha kuleta Matumaini na kuzidi kupendwa na Wafanyakazi.

Cha kujifunza sometimes how to speak inaweza kukusaidia pia kueleweka na kukubalika.

Nilichokiona Mama ana Matamanio ya kumeet Matamanio ya Watanzania ila Serikali aliyoachiwa haina uwezo huo, tumpe muda.
 
Bi Mkubwa kasetiwa na awamu ya 4 because anajua influence ya JPM ni impeccable. Anatafuta kijimwamba cha kusimamia ili kuirudisha awamu ya 4 madarakani
 
Ni kweli, Umasikini wa nchi ndio unamkwamisha. Maana hadi nimemshangaa eti anawaomba radhi Wafanyakazi kwa kutoongeza mshahara na kutoa sababu kuwa Covid imetuathiri na uchumi umeshuka.

Angekuwa mtangulizi wake wala asingekuwa na haja ya kutoa hizi sababu, angesema tu kama kawaida yake hakuna nyongeza. Uchumi unakuwa kwa kasi sana, tupo kwenye uchumi wa kati.
 
Nyongeza hakuna na anaeona haridhishwi Aache kazi hata sasa hivi, namnukuu hahahaa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…