Isanga family
JF-Expert Member
- Feb 25, 2015
- 17,080
- 33,076
Noma sana aiseeNilikuwa sijui kama mtu anaweza kuwa na kilo 210
Kwa unene huo anapafikiaje HQHajashindwa kulea.Anaomba mumewe arudi home.
Mbona wanasema aliitukana rangi ya vegetablesShida watu wanamchukulia poa yule mama ila ana hela sio kitotoView attachment 2628862
Hata Duka lake aliuza nakumbuka kipindi kile alikuwa anaingiza vipodozi kutoka Congo na Uganda Ila magufuli alivyoanza kupiga Pini mipakani watu wengi walianguka kibiashara akiwemo huyu mama..Sinyaa mpambanaji sana TRA kariakoo walimfanya kama kibubu chao bila jeuri yake angerudi kijijini aisee maana pana kipindi karibu wiki nzima walikua wanashinda kwenye store yake hata kinachotafutwa hakieleweki wakila mpunga wanatulia wakitaka hela wanamtafuta tena...ila huyo ni kiboko pana siku aliwahi wafungia maofisa na kufuri kubwa store akaondoka zake sijui ile kesi iliishaje msala juu ya msala...ilibidi kufuri livunjwe na baadhi ya wazee wa kazi waliopata taarifa ila bila ubishi huyo dada naamini angerudi kijijini kitambo mno yupo saba saba jengo la Sauli huyo dada namkubali sana ni Jembe la mkono kweli hana woga hata Chembe..
Sawa,Tra walikuwa wanasheria tofauti na sasa?Kama walilala waanze taratibu.Mbona alipokuwa anaingiza milioni 1 mpaka 2 kwa siku alikuwa halalamiki?TRA si walikuwepo?Hakuweka akiba?Ni ujinga kutojiandaa wakati ukiwa na kipato kizuri na kuja kulalama na kutafuta wa kulaumiwa mambo yakibadilika.Asiangalie alipoangukia aangalie alipojikwaa.
Kassim Majaliwa alijichekea sana"Naomba namba nije chembaaaa"
"Naomba pointment"
Mchaga km mchagaaa, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Bhalaa Kubwa Hao Wawili Wakipanda Vitz Mwezi Mmoja Gari Inagonga ChiniNilikuwa sijui kama mtu anaweza kuwa na kilo 210
Ni dada ila anaonekana mtu mzima sana kwa sababu ya mwili wake ila mtu poa sana sana alikua jirani yangu kwenye duka lake la la hiyo mitaa ni mzungu wa roho sana sana na wala sio mzurumati kawasaidia Wachaga kibao ndio maana nae hawezi kupata tabu na wala haesabu akimsaidia mtu akichukua mzigo akisema wiki ijayo ni wiki ijayo kweli sema TRA wamemrud8sha nyuma sana maana hawataki watu wawe matajiri kupitia Kariakoo anatuma mizigo Zimbabwe mpama DRC na watu wengi anafanya nao kazi kama kiwanda wengine watu wazima ila wakimwona heshima za kutosha mimi nilimkubali kwenye life yake ya Uzungu wa roho....Hata Duka lake aliuza nakumbuka kipindi kile alikuwa anaingiza vipodozi kutoka Congo na Uganda Ila magufuli alivyoanza kupiga Pini mipakani watu wengi walianguka kibiashara akiwemo huyu mama..
Namjua huyu mama kitambo mitaa ya jangwani/mafia ni MTU maarufu kipindi kile anatembelea magari ya kishua
Mimi ni Mjasiriamali wa vipodozi na niko Kariakoo kwa muda wa miaka 20 na zaidi, kero tunazokutana nazo hapa Kariakoo ni nyingi sana na zinavunja moyo, kero ya kwanza hatufanyi biashara kwasababu ya (TRA), Wateja sasa hivi wananunua mizigo nje ya Kariakoo wanaogopa TRA, kwa mana hiyo sisi tunashinda tu vibarazani maana hakuna biashara wala wateja"
"Watu wa TRA na watu wa Taka wanatuumiza sana, mimi mpaka nilishapiganaga na vitoto vya TRA ndiyo maana nilivyosikia Waziri Mkuu anakuja nikasema leo lazima niende nikatoe nyongo iliyonikaa kwa muda mrefu, nilivyoenda pale mkutanoni bahati nzuri Waziri Mkuu akaniita nikaenda kutoa baadhi ya kero zangu, nasema baadhi kwasababu bado sijamaliza nina mengi ya kumwambia Waziri Mkuu, bado naitafuta namba yake"
"Tumefirisika hatuna kitu, mimi nilikuwa na pesa yani hapa sina kitu, ili kujisukuma inatubidi tujiingize kwenye mikopo ya "kausha damu" ambayo kwa mimi binafsi mkopo wa "kausha damu" umevunja ndoa yangu, nimeachana na mume wangu kwasababu ya "kausha damu", "kausha damu" imeniharibu sura, sikuwa hivi, mimi ni natural sijajichubua hata kidogo hii ni ngozi ya Kichaga Og, ila kulia kila saa na mikopo ya kausha ndiyo imeniunguza sura"
"Hapa nimepungua sana watu wanaonijua wanashangaa sana, nina kg 198 ila nilikuwa na kg 210, natamani sana kupungua, natamani niwekewe puto hata sasa hivi, Peter Msechu siyo wa kuwekewa puto, mimi ndio natakiwa niwekewe hilo puto.
"Hakuna biashara Kariakoo, TRA wameua biashara yaani tumekaa tu lakini biashara hakuna, wateja wanaokuja wananunua kopo la mafunzo elfu 10, kwa siku unatoka na elfu 20 ya mauzo, hapo unalipa kodi, TRA na Taka, kuna biashara hapo?, zamani nilikuwa nauza milioni moja, moja na nusu mpaka milioni mbili kwa siku, nyumbani kwetu mimi ndio kama Bhakresa, ndugu wote wananitazama mimi lakini awamu hii nimeshindwa hata kuwapeleka watoto shule".
Aidha Bi Sinya amesema anavutiwa sana na Mbosso, kila anaposikiliza wimbo wa Mbosso moyo wake unakwatuka anajisikia raha burudani, hadi kufikia sasa hivi mama huyo anaendelea kujizoea maelfu ya followers huko Instagram, ambapo jana alikuwa na followers elfu mbili pekee na hadi kufikia leo sasa hivi ana followers elfu 15 na zaidi.
Credit: FB
View attachment 2628823
Msanii huyo hashindwi.Anataka papaa ya bana a-alee mundako na ndako!
Najuta kutooa mchagaa!Sinyaa mpambanaji sana TRA kariakoo walimfanya kama kibubu chao bila jeuri yake angerudi kijijini aisee maana pana kipindi karibu wiki nzima walikua wanashinda kwenye store yake hata kinachotafutwa hakieleweki wakila mpunga wanatulia wakitaka hela wanamtafuta tena...ila huyo ni kiboko pana siku aliwahi wafungia maofisa na kufuri kubwa store akaondoka zake sijui ile kesi iliishaje msala juu ya msala...ilibidi kufuri livunjwe na baadhi ya wazee wa kazi waliopata taarifa ila bila ubishi huyo dada naamini angerudi kijijini kitambo mno yupo saba saba jengo la Sauli huyo dada namkubali sana ni Jembe la mkono kweli hana woga hata Chembe..
... na anakuambia kapungua sana to 198 hadi anaogopa! Duh!Nilikuwa sijui kama mtu anaweza kuwa na kilo 210
Alikua anauza zaidi ya 10 m kwa siku wameambiwa 1m wanaona nyingi huyu alikua anaenda China kama anaenda Magomeni...Najuta kutooa mchagaa!
... Ni wapambanaji aisee!
π