Miss Madeko
JF-Expert Member
- Apr 30, 2014
- 4,364
- 5,609
nikisema 80 naanza 80 hadi 89
Mwaka 1977 unapelekwa UDSM...! Shikamoo. Sikutanii tena. Nashika adabu yangu. Na kama utapendezwa utakuwa unanituma dukani kibiriti au hata jagi la Maji ya Kunywa ndani, nitaleta!Ninakumbuka mkutano wa UWT mwaka 1977 ulifanyika UDSM, mama yangu alikuwa mjumbe. Sikumbuki mengi zaidi ya kuwa tulikuwa tunapelekwa jioni UDSM kumuona kwani alitumia muda mwingi kwenye shughuli za chama.
Mama Sofia alipita Tena bila kupingwa nafasi ya uwenyekiti
ebu tusaidie majina ya walioandika katiba hii ya ovyoo enzi hizo, napenda niwafahamu japo kwa majinaUlidhani ni mtoto mwenzio?
Usikae kimya, kampe shikamoo yake bhana...
Duh 1977?Ninakumbuka mkutano wa UWT mwaka 1977 ulifanyika UDSM, mama yangu alikuwa mjumbe. Sikumbuki mengi zaidi ya kuwa tulikuwa tunapelekwa jioni UDSM kumuona kwani alitumia muda mwingi kwenye shughuli za chama.
Mama Sofia alipita Tena bila kupingwa nafasi ya uwenyekiti
Alikuwa na wawili, Wa kwanza alikuwa na matatizo ya uzazi, so akamuoa Sofia ili amzalie, na baadhi ya watoto Wa Sophia walilelewa na bimkubwa1977 hata sijazaliwa,Hivi Kawawa alikuwa na wake wangapi ?Huyu Sophia Kawawa alikuwa na fani gani ?
Shukran mkuu, inawezekana humu jukwaani kuna atakaekuja na jina lake.
John...UWT:
1. Bibi Titi
2. Mama Mchauru 3. 3. Mama Sofia Kawawa.
Alitoa hotuba yake nzuri sana akiwa Mbeya yenye lengo la kuwahamasisha wanawake wa UWT.
Hutuba yake iliwataka Wamama kushirikiana katika shughuli za kuzalisha Mali (ujasiria Mali)
kwa vile wao ndiyo hubeba mzigo mkubwa wa kualea watoto pia kuweka family zao vizuri kimaisha.
Alishauri kuwepo kuweka sheria ya kuwa na mke mmoja kwa wakati mmoja (Yaani mtu akioa basi awe na mmoja hadi watakapofarakana au kutalikiana).
Alisisitizia Kwa kusema hata kitabu cha Qur'an tukufu haijasema NI LAZIMA WANAUME WAONE WANAWAKE ZAIDI YA MMOJA ILA ANAPOONA INAFAA NA ANA UWEZO WA KUWAHUDUMIA WOTE NA AOE VINGINEVYO ABAKI NA MMOJA .
Na kwa vile hii hasa iliwahusu sana Waislam ambao huweza kuwa na wake 4 kwa wakati mmoja.
Alisema wanawake wanashindwa kushirikiana vyema kwa vile huchukiana kiwivu ya kugombea Mme wao.
Matamshi ambayo yalipingwa vikali sana na Mashekhe wa Zanzibar na kusababisha sintofahamu na maandamano makali wakidai mama kakashifu Qur'an.
Mzee Kawawa na Mzee Aboud Jumbe ndiyo walisawazosha na kumaliza hilo vyema
Mwenyezi Mungu awaweke mahali pema peponi Amina
Ilipita miaka mingi ndipo alifariki na sio albadili kama mmoja Wetu alivyosema
Tena nywele zimebanwa na ribbon unajiona ni wewe tuMwaka 1977 unapelekwa UDSM...! Shikamoo. Sikutanii tena. Nashika adabu yangu. Na kama utapendezwa utakuwa unanituma dukani kibiriti au hata jagi la Maji ya Kunywa ndani, nitaleta!
Asante sana mzee Mohamed Said kwa habari hii, wengi hatukuyafahamu haya.John...
Hotuba ile ya Sophia Kawawa ni moja katika misiba mikubwa iliyowafika
Waislam wa Tanzania.
Baada ya Sophia Kawawa kusema maneno yale katika ile hotuba yalifanyika
Maandamano makubwa Zanzibar ya kumpinga na mtu mmoja aliuawa na askari
walioamrishwa kuyazuia na wengine kadhaa katika waandamanaji kubakia vilema.
Baadhi ya washtakiwa 15 walisindikizwa na askari kwenda Chuo Cha Mafunzo
kutumikia kifungo chao.
Waandamanaji hawa walifikishwa mahamani na ilifanyika kesi iliyogusa
hisia za Waislam wengi Tanzania.
Mshtakiwa aliyetia fora kwa majibu yake mahakamani alikuwa Sheikh
Said Gwiji ambae alikuwa katika wakati ule ni mwanafunzi wa Sheikh
Nassoro Bachu kati ya masheikh vijana maarufu Zanzibar wakati ule.
Sheikh Gwiji na wenzake walihukumiwa kifungo sikumbuki miaka mingapi
lakini ni zaidi ya mwaka na walitumikia kifungo kile.
Nilifanya mahojiano na Sheikh Gwiji nyumbani kwake Zanzibar mwaka wa
2012 kwa ajili ya kipindi cha TV Imaan Zanzibar na kisa hiki cha Sofia
Kawawa alikieleza kwa kirefu.
Kushoto Sheikh Said Gwiji akifanya mahijiano na Mwandishi
Ni kweli kabisa mkuu, kwa mafanobhistoria ya Bi Titi Mohamed nilihadithiwa na mama yangu lakini mwaka 1964 sikuwepo duniani.Wengine si wakubwa kihivyo ni kutokana na juhudi za wazazi wao kuwaelezea historia ya nchi yao, juhudi zao wenyewe kujisomea na kufuatilia mambo. Utashangaa mtu anakwambia wewe utakuwa mtu mzima sana kwa sababu tu unafahamu mambo mengi ya zamani. Tatizo siku hizi na hii internet watu hawasomi kabisa vitabu hivyo hawayajui mengi kuhusu nchi yetu na wala hawayafuatilii.
CC: sky Éclat
Kiku Mzumbe ipo Hostel inaitwa Sophia!Ninadhani UWT hawajafanya ya kutosha kuwa enzi watu hawa. Kukuta kuwa kuwe na kitu kama hosteli ya Sofia Kawawa pale UDSM kusaidia wanafunzi wa kike