Mama Terry yuko wapi?

Alhamis ukimwi radio one alikuwa hakosagi mara akaja kuibuka tbc na kipindi cha ndoto mara kimyaaaa.
 
Uongo na ulaghai hauwezi kudumu milele

huyo mama kawalisha sana watu majani ya michongoma, majani tofautitofauti mara anawambia watwange mkaa waule yaani balaaa ...ukienda kwake kurasini kulikuwa na watu kibao
 
Huyu mama nasikia alikuwa na ngoma sasa inawezekana alisha tangulia mbele za haki
 
Niliwahi kusikia kuwa alienda Nigeria kufuatilia mirathi ya marehemu mme wake ambaye alikuwa ni raia wa nchi hiyo. Sina hakika kama alisharudi au atakuwa alijiunga na bongo movie ya Nigeria manake kwa kuigiza yule mama yuko juu.
 
Ni mtangazaji wa radio moja Nigeria kwa mume wake, na ana kipindi kama kile cha radio one, yuko vizuri sana
 
Naangalia TBC1 muda huu. Namuona mama Teri na Marin Hassan na mtu mwingine. Wanaongelea Al Shabaab, kuuwawa kiongozi wao, wananchi wa Nigeria kaskazini kuwakubali hao AS, etc.

Hata hivyo, nimewaza kuhusu ilim ya lishe alokua akitoa Mama Teri. Mbona ye haonekani kama ana afya? Kajaziana sana (muniwie radhi kama na-attack personality).

Wakati ule akiongelea tiba ya mkojo alikua anatuingiza chaka?
 
Alizuiwa na Taasisi ya chakula na lishe Tanzania (TFNC) kuwalisha watu sumu kwani yeye siyo mtaalamu wa lishe bali ni muokotaji wa vitaarifa kutoka source isiyojulikana na kuwadanganya watanzania. mwaka 2010 alitaka kugombea Kigamboni kwa tiketi ya CCM lakini akaangushwa vibaya kwenye kura ya maoni...hivyo nikagundua kwamba ule uwongo aliokuwa anatupatia ni kwa ajili ya siasa. Ila kwa upande mwingine nampongeza kwa kuweza kutuletea taarifa za machangudoa waliokuwa wanafanya uhuni wao kwenye makaburi ya kinondoni. na jambo jema jingine alilowahi kufanya ni kutengeneza bustani za jiji la Dar es Salaam hasa kwenye round about enzi hizo, alikosa ushirikiano kutoka serikalini na hata halmashauri ya jiji...alisumbuliwa akaiacha shughuli hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…