Habari wana JF. Hii ni mara ya pili ninarudia kuandika kisa hiki kilichotokea kwa Marehemu profesa Mmoja kwa jina tunamhifadhi. NI vizuri kuandika hii hadithi ili Jamii iweze kutambua uzembe wa kina baba ambao hawaandiki wosia mapema matokeo yake wanaacha majanga kwa watoto.
Kuna Professa Mmoja hapa Dar alifariki Mwaka 2012. Katika Maisha yake Marehemu Alioa Mwaka 1984 na mwanamke mzungu na kuzaa naye watoto wawili. waliishi kwa pamoja mpaka walipotengana mwaka 1990. Huyo Mwanamke mzungu alirudi kwao ulaya na kumwacha Professa na watoto wake wote wawili wakiishi pamoja na mali walizokuwa nazo kipindi hicho ikiwemo magari nyumba mikocheni na viwanja .
Huyo profesa alioa tena mwaka 2005 na Mama mwingine. walizaa mtoto mmoja wa kike. Huyo Professa naye alimjengea Nyumba na Kumnunulia viwanja huyo Mke wa pili. Kwa bahati mbaya Huyo professa alifariki mwaka 2012. Migogoro ilibuka baina ya Ndugu wa upande wa huyo Mama wa kambo na ndugu wa marehemu wanaowatetea watoto kwanza wa Marehemu.
Kikao cha ukoo kilikaa na kumteua msimamizi wa Mirathi ambaye alikuwa ni bamdogo wa hawa watoto wa kwanza.Yule Mama wa kambo alienda moja kwa moja Mahakama kuu kufungua shauri Mahakamani kuhusu kesi ya mirathi na alitaka Mahakama imteue yeye Mama wa kambo awe Msimamizi wa mirathi.
Kesi imeenda miaka 2 na hatimaye Judge akaamua achague wasimamizi wawili yaani mke wa pili wa professa na Bamdogo wa watoto wa marehemu wamechaguliwa kuwa wasimamizi.
Ndugu wameoona kukata rufaa itachelewesha muda na gharama wakaona njia ya kutatua tatizo hili ni kwamba wakae kikao cha pamoja na yule mke wa pili na kujadili mgawo wa mirathi iende vipi. lakini ukweli ni kwamba yule mke wa pili hawezi kukubali mali za marehemu zigawanywe kihalali kwa sababu naye ni msimamizi wa mirathi na vile vile ana ndugu na marafiki ambao wanamsapoti kwa nguvu zote lazima atataka asilimia kubwa ya mali iende kwake. kwahiyo kasheshe ipo katika hichi kikao wajadili vipi?
Nasikitikia hawa watoto wa mke wa kwanza maana sijui haki yao wataipata vipi na tayari ni machokoraa wa mtaa na ndugu zao wameishiwa sera na wanaonekana hawana ubavu wowote wa kumzuia huyu Mama wa kambo.
Mnakaribishwa kwa ushauri wenu. asante
Hii ni nyumba ambayo marehemu professa alijenga miaka ya 1988 na alikuwa akiishi na watoto wake wa kwanza. Hivi sasa Nyumba hio watoto wamenyanganywa na mama wa kambo. Na Mama wa kambo amekuwa akiitumia nyumba hio kwa maslahi yake binafsi pamoja na ndugu zake.
View attachment 176935
Kuna Professa Mmoja hapa Dar alifariki Mwaka 2012. Katika Maisha yake Marehemu Alioa Mwaka 1984 na mwanamke mzungu na kuzaa naye watoto wawili. waliishi kwa pamoja mpaka walipotengana mwaka 1990. Huyo Mwanamke mzungu alirudi kwao ulaya na kumwacha Professa na watoto wake wote wawili wakiishi pamoja na mali walizokuwa nazo kipindi hicho ikiwemo magari nyumba mikocheni na viwanja .
Huyo profesa alioa tena mwaka 2005 na Mama mwingine. walizaa mtoto mmoja wa kike. Huyo Professa naye alimjengea Nyumba na Kumnunulia viwanja huyo Mke wa pili. Kwa bahati mbaya Huyo professa alifariki mwaka 2012. Migogoro ilibuka baina ya Ndugu wa upande wa huyo Mama wa kambo na ndugu wa marehemu wanaowatetea watoto kwanza wa Marehemu.
Kikao cha ukoo kilikaa na kumteua msimamizi wa Mirathi ambaye alikuwa ni bamdogo wa hawa watoto wa kwanza.Yule Mama wa kambo alienda moja kwa moja Mahakama kuu kufungua shauri Mahakamani kuhusu kesi ya mirathi na alitaka Mahakama imteue yeye Mama wa kambo awe Msimamizi wa mirathi.
Kesi imeenda miaka 2 na hatimaye Judge akaamua achague wasimamizi wawili yaani mke wa pili wa professa na Bamdogo wa watoto wa marehemu wamechaguliwa kuwa wasimamizi.
Ndugu wameoona kukata rufaa itachelewesha muda na gharama wakaona njia ya kutatua tatizo hili ni kwamba wakae kikao cha pamoja na yule mke wa pili na kujadili mgawo wa mirathi iende vipi. lakini ukweli ni kwamba yule mke wa pili hawezi kukubali mali za marehemu zigawanywe kihalali kwa sababu naye ni msimamizi wa mirathi na vile vile ana ndugu na marafiki ambao wanamsapoti kwa nguvu zote lazima atataka asilimia kubwa ya mali iende kwake. kwahiyo kasheshe ipo katika hichi kikao wajadili vipi?
Nasikitikia hawa watoto wa mke wa kwanza maana sijui haki yao wataipata vipi na tayari ni machokoraa wa mtaa na ndugu zao wameishiwa sera na wanaonekana hawana ubavu wowote wa kumzuia huyu Mama wa kambo.
Mnakaribishwa kwa ushauri wenu. asante
Hii ni nyumba ambayo marehemu professa alijenga miaka ya 1988 na alikuwa akiishi na watoto wake wa kwanza. Hivi sasa Nyumba hio watoto wamenyanganywa na mama wa kambo. Na Mama wa kambo amekuwa akiitumia nyumba hio kwa maslahi yake binafsi pamoja na ndugu zake.
View attachment 176935